Je, Serikali inahusika na taharuki, ili watu wasijadili mambo muhimu?

Je, Serikali inahusika na taharuki, ili watu wasijadili mambo muhimu?

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869

Majasusi wa kiserikali duniani huzua taharuki mashimo yenye miili ya binadamu, watu kunyofoa viungo vya binadamu, pipi kutumika kuteka watoto. Pia kesi ya Deus Soka inatumika kuogopesha raia . Nitafafanua mbeleni

Je, kwa hapa kwetu matukio haya nayo yana nasaba hizo hapo juu?

Mashirika ya kijasusi hutumika kuzua taharuki ili watu wasitulie kiakili, kiroho na kijamii kujadili mustakhabali ya nchi yao mfano :
  • Kuna uchaguzi 2024
  • Uchaguzi mkuu 2025
  • TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI
  • Ardhi za Wananchi kutwaliwa
  • Watu Kuhamishwa kwa nguvu
  • Hali ngumu ya maisha
  • Huduma za maji, bima ya afya
  • Kutekwa watu
  • Waganga wa kienyeji na mafuvu/ miili ya watu Dodoma Singida n.k
  • Kukuacha katika sintofahamu je serikali inasema kweli haihusiki maana sasa miili na utatubulisho wa marehemu taarifa zake sasa zinatoka kule Singida, Dodoma n.k
 
Kwanini kesi ya Deus Soka inatumiwa na dola isisikilizwe mapema

Ni kwamba inatumika na dola kutishia raia kuwa usishiriki siasa. Kwa Deus Soka na wenzie kutokuwa mikononi mwa polisi serikali inasema haihusiki na inajiburuza kufanya uchunguzi.

REJEA MWAKA 2023

MAHAKAMA YAIBANA POLISI KWA KUKAA NA MTUHUMIWA SIKU 18
Mahakama Kuu, Masjala ya Dar es Salaam imeliamuru Jeshi la Polisi nchini kumfikisha mahakamani Mkurugenzi wa Kampuni ya Nezak Investment Limited, Zakaria Kapama ambaye yuko mahabusu kwa siku 18 bila kufikishwa kortini.

Kifungu cha 32 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) ya mwaka 1985 na marekebisho yake, kinataka mtuhumiwa kufikishwa mahakamani ndani ya saa 24, isipokuwa kwa makosa yale ambayo adhabu yake inakuwa ni kunyongwa hadi kufa.

Kwa mujibu wa kifungu hicho, ikiwa haiwezekani, basi mtuhumiwa aachiwe kwa dhamana, lakini kumekuwa na kilio katika vituo mbalimbali vya polisi kuwa, baadhi ya watuhumiwa husota muda mrefu mahabusu za polisi bila kufikishwa kortini kwa wakati.

Amri hiyo ilitolewa jana na Jaji Wilfred Dyansobera, baada ya maombi ya jinai yaliyowasilishwa mahakamani na Kapama dhidi Mkuu wa Kituo cha Polisi (OCS) cha Oysterbay, Kamanda wa Polisi Kinondoni na Inspekta Jenerali wa Polisi.

Katika maombi hayo namba 132 ya 2023, Kapama alimuunganisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kama mjibu maombi wa nne na aliiomba Mahakama kuwaagiza wajibu maombi hao kumwachia wanavyomshikilia au kumweka kizuizini isivyo halali.

Pia, aliomba kama hawatamwachia, basi Mahakama iwaamuru wajibu maombi kufika mahakamani kueleza sababu za kumnyima uhuru wake, kumzuia, kumuweka kizuizini nje ya muda wa kisheria na kuwataka kutimiza majukumu kwa mujibu wa sheria.

Kupitia kwa wakili wake, Deogratias Butawantemi, Kapama ambaye pia kampuni yake inamiliki KP Motors inayohusika na uagizaji wa magari, anaeleza Septemba 29 mwaka huu 2023 alikamatwa na polisi na kuwekwa mahabusi Kituo cha Oysterbay.

Kwa mujibu wa hati ya kiapo chake, hadi anawasilisha maombi hayo juzi alikuwa bado anashikiliwa kituoni hapo bila kupewa dhamana wala kufikishwa mahakamani, kama sheria za nchi zinavyoelekeza.

Akitoa uamuzi wa maombi hayo jana, Jaji Dyansobera aliwaagiza Mkuu wa Kituo cha Polisi Oysterbay na wajibu maombi wenzake, kuhakikisha mleta maombi huyo anafikishwa mbele ya Mahakama na amri hiyo itekelezwe sio zaidi ya siku ya leo (Jumatano).

(Imeandikwa na Daniel Mjema)

Soma Hukumu : Ya Jaji Wilfred Dyansobera, wa Mahakama Kuu ya Tanzania

Source : Zakaria Anthony Kapama vs. Officer Commanding Station Oyterbay (OCS) & 3Others) (Misc. Criminal Application No. 132 of 2023) [2023] TZHC 21830 (17 October 2023)
 
DOLA KUGONGANISHA BONGO ZA RAIA KWA MAKUSUDI, KIASI KILA MMOJA ANAJIPINGA MWENYEWE NDANI YA NAFSI YAKE NA KUISHIA KTK MKWAMO
1724965351067.png

Kugonganisha maoni ya raia kwa kuwapa taarifa nzuri za mafanikio ya serikali kupata waliopotea na kuendelea kukanusha hakuna wanaoshikiliwa mikononi mwa vyombo vya dola vya serikali


NDIMI MBILI (Doublethink) ni mchakato wa makusudi kufanya raia ambapo wahusika katika nchi wanatarajiwa kukubali kwa wakati mmoja dhana mbili zinazokinzana kuwa ukweli, mara nyingi kinyume na kumbukumbu zao au hisia za ukweli.

Kufikiri mara mbili kunahusiana na matukio katika jamii, lakini wakati huohuo akili yako hutofautiana na, unachosikia kweli au si kweli hivyo kuishia kulipuuza jambo .

George Orwell alibuni neno doublethink kama sehemu ya lugha ya kubuniwa ya mkakati maalum waliobuni lugha yao ya kipekee yaani Newspeak katika riwaya yake ya dystopian ya 1949 ya Nineteen Eighty-Four . Katika riwaya, chimbuko lake lugha hii mpya ya walio katika mamlaka kwa,ndani ya raia halieleweki; ilhali inaweza kuwa kwa kiasi fulani zao la programu rasmi za mamlaka kufubaza bongo za raia Big Brother za uoshaji ubongo , [ i ] riwaya hiyo inaonyesha kwa uwazi watu wakijifunza kufikiri mara mbili wenyewe na lugha mpya ya Newspeak kutokana na shinikizo la mamlaka huwa taarifa zao ni za kweli na nia za "kufaa", au ukikubali basi kupata hisani ya hadhi ndani ya Chama—Tawala . kuonekana kama Mwanachama mwaminifu wa Chama.

Katika riwaya hii, kwa mtu hata kutambua—achilia mbali kutaja—mkanganyiko wowote ndani ya muktadha wa mstari wa msimano wa bunge, mahakama, serikali na Chama kongwe dola tawala ni sawa na kukufuru , na inaweza kumfanya mtu huyo kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kutoidhinishwa papo hapo kijamii na Wanachama wenzake.
 

29 August 2024

Who Kidnapped, Forcibly Disappeared These Tanzanians? Nani Aliyewateka, Kuwapoteza Watanzania Hawa?


View: https://m.youtube.com/watch?v=i6j0yPOzdnY

This documentary covers incidents of abductions and disappearances, events that are increasingly occurring in many parts of Tanzania, with the fate of those who have disappeared remaining uncertain.


Makala hii inaangalia matukio ya watu kutekwa na kupotezwa, matukio yanayoendelea kushika kasi katika maeneo mengi ya Tanzania huku hatma ya waliopotezwa ikiwa mashakani.......

Source : The Chanzo
 
Meya wa zamani Boniface Jacob kuhusu hukumu ya wasiojulikana kuteka watu, maamuzi ya bunge kukaa kimya, serikali kushindwa kuwapata watu watekaji wasiojulikana kilichobaki ni wananchi kuchukua hatma yao kujilinda ...

1724998004639.png
 

Majasusi wa kiserikali duniani huzua taharuki mashimo yenye miili ya binadamu, watu kunyofoa viungo vya binadamu, pipi kutumika kuteka watoto. Pia kesi ya Deus Soka inatumika kuogopesha raia . Nitafafanua mbeleni

Je, kwa hapa kwetu matukio haya nayo yana nasaba hizo hapo juu?

Mashirika ya kijasusi hutumika kuzua taharuki ili watu wasitulie kiakili, kiroho na kijamii kujadili mustakhabali ya nchi yao mfano :
  • Kuna uchaguzi 2024
  • Uchaguzi mkuu 2025
  • TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI
  • Ardhi za Wananchi kutwaliwa
  • Watu Kuhamishwa kwa nguvu
  • Hali ngumu ya maisha
  • Huduma za maji, bima ya afya
  • Kutekwa watu
  • Waganga wa kienyeji na mafuvu/ miili ya watu Dodoma Singida n.k
  • Kukuacha katika sintofahamu je serikali inasema kweli haihusiki maana sasa miili na utatubulisho wa marehemu taarifa zake sasa zinatoka kule Singida, Dodoma n.k
HAYA unayoyasema ni ukweli mtupu..
Kuna nadharia mbili
1. Let it happen on purpose
2. Make it happen on purpose...
Majasusi kote ulimwenguni wanajua hizi mbinu za kufanya mambo Yao yatokeee. Wanajua fika kuwa Kuna jambo la hatari lakn waanaacha litokee Ili wapate sababu ya kufanya wanayoyanua..
 
30 April 2024

MADAI YA INTELEJENSIA YA JESHI LA POLISI

Akizungumzia na Mwananchi leo, Mwenyekiti wa CHADEMA , mheshimiwa Freeman Mbowe amesema taarifa ya Jeshi la Polisi ni ya uongo.


“Tuko concerned (tunaguswa) kuhusu usalama na haki za viongozi wetu wanaoendelea kutekwa na kupotezwa, lakini hiyo taarifa kwamba sisi tulifaya kikao cha Zoom ni uongo.


“Ninasikitika kwamba Jeshi la Polisi, taasisi muhimu kama hiyo, linaweza kutoa taarifa ya uongo kama hizo mitandaoni na hebu watupe huo ushahidi, hao waliofanya hiyo Zoom ni kina nani, saa ngapi na wakati gani?” amehoji Freeman Mbowe.


Amesema kwa sasa yeye yuko nje ya nchi na hakuna kikao walichopanga kukifanya.
“Hao waliofaya Zoom ni kina nani? Mimi kama mwenyekiti sina taarifa, kina nani wanaamua jambo kama hilo?


“Tuko concern na tunawasiliana si viongozi mmoja mmoja kuhusu hali ya usalama wa viongozi wetu, lakini kwamba kimefayika kikao kikaweka maazimio kwamba tutavamia vituo vya polisi huo ni ujinga tu kwa Jeshi la Polisi lililokosa weledi na linaweza kutoa taarifa kama hizo za uongo,” amesema.


Freeman Mbowe amesema taarifa hiyo ya polisi inalenga kukwepa maswali ya msingi ya walipo Deusdedith Soka na wenzake ambao amesisitiza kuwa jeshi hilo ndilo linawashikilia.

“Watoe ushahidi kama wanao lakini la msingi watueleze, Deus Soka na wenzake wako wapi, maana polisi wanajua, waliwachukua na wamewapeleka wapi, waache kutoa kisingizio cha kitoto kama hicho.”


Alipoulizwa kama watawashtaki polisi kwa kuwazushia taarifa za kikao hicho, Mbowe amesema, “hayo ni mambo mengine, lakini kwa sasa nakwambia hizo ni taarifa za uongo na uzushi na kitu kibaya kwa chombo muhimu kama hicho kukisingizia uongo chama cha siasa muhimu kama CHADEMA.


“Warudi kwenye hoja ya msingi kwamba, Deus Soka, Mlay na Mbise wako wapi? Hii ya kusema CHADEMA imefanya mkutano kupitia Zoom meeting ni ujinga usio na kipimo, hatujawahi kufanya na hatujaweka mpango wowote wa kushambulia kituo cha polisi,” amesisistiza.
 

27 August 2024​

Masauni Akutana na Uongozi wa Jeshi la Polisi Kujadili Hali ya Amani na Usalama​

Dodoma. Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwandisi Hamad Masauni leo amekutana na viongozi wa juu wa Jeshi la Polisi Tanzania kujadili hali ya amani na usalama ikiwemo matukio ya uhalifu yanayotkea nchini na hatua zilizochukuliwa.

1725025489127.png

Kikao hiko pia kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani, Daniel Sillo, ambapo kwa upande wa Jeshi la Polisi ujumbe wake uliongozwa na Inspekta Jenerali wa Polisi, Camillus Wambura.


Kikao hiki kinakuja ikiwa ni siku chache tangu Jeshi la Polisi kupitia kwa msemaji wake kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu yanayohusu watu kupotea na mauaji ambayo Polisi ilieleza yalitokana na sababu mbalimbali ikiwemo masuala ya kujichukulia sheria mkononi, wivu wa mapenzi na imani za kishirikina.


Lakini pia wadau mbalimbali ikiwemo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Asasi za Kiraia na vyama vya siasa wamekuwa wakipaza sauti kufuatia kuripotiwa kwa matukio ya utekaji na mauaji ya watu wazima na watoto.

Baadhi ya wadau hao ikiwemo vyama vya siasa wamewatupia lawama Jeshi la Polisi wakiwashtumu kuhusika jambo ambalo wamelikanusha.


Kikao hiko cha Waziri Masauni kilihudhuriwa na viongozi wote wa kamisheni za Polisi ikiwemo Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimaliwatu, Suzan Kaganda, Kamishna wa Fedha na Lojistiki, Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Awadh Juma Haji, Kamishna wa Sayansi ya Uchunguzi wa Jinai, Shabani Hiki.


Wengine ni Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai CP Ramadhani Kingai, Msemaji wa Jeshi la Polisi, ACP David Misime, Naibu Kamishna kutoka Kamisheni ya Intelijensia na Jinai, Kheriyangu Khamis Mgeni, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro
 
Uchafuzi wa uchaguzi 2019 na 2020.

Je wizara ya TAMISEMI uchaguzi wa 2024 mheshimiwa Mohamed Mchengerwa ataweza kutenda haki
1725206143375.png
 
Kesi inayomkabili mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Tanga, aliyepotea kwa mwezi mzima.

View: https://m.youtube.com/watch?v=tEAy82_-uWw
Kisha baadaye akapandiahwa kizimbani na Jeshi la Polisi mkoani Tanga, Kombo Mbwana Jumanne, leo inaendelea katika Mahakama ya Wilaya ya Tanga.Kesi hiyo ya jinai namba 19759 ya mwaka 2024, ilipangwa leo Jumanne Julai 30, 2024 kwa ajili ya kutajwa kuangalia kama upelelezi umekamilika, pamoja na utaratibu wa dhamana kama mshtakiwa huyo atakuwa ametimiza masharti.....
 

29 August 2024

Who Kidnapped, Forcibly Disappeared These Tanzanians? Nani Aliyewateka, Kuwapoteza Watanzania Hawa?


View: https://m.youtube.com/watch?v=i6j0yPOzdnY

This documentary covers incidents of abductions and disappearances, events that are increasingly occurring in many parts of Tanzania, with the fate of those who have disappeared remaining uncertain.


Makala hii inaangalia matukio ya watu kutekwa na kupotezwa, matukio yanayoendelea kushika kasi katika maeneo mengi ya Tanzania huku hatma ya waliopotezwa ikiwa mashakani.......

Source : The Chanzo

This is dangerous more than a war
 
Back
Top Bottom