Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Wanahabari wamelalama kuwa wanadai serikali jumla ya bilioni 18 za kitanzania. Haya malimbikizo ya madeni kwa miaka kadhaa ambayo yametajwa kuathiri uchumi wa vyombo vya habari.
Suala la madeni sio tu kwa sekta ya habari, nimesikia wadau kadhaa wakilalamika kutolipwa na serikali kiasi cha madeni hayo kukua au wakati mwingine kuathiri uchumi wa waliotoa huduma husika kwa serikali.
Kama serikali iko serious kwenye kukuza uchumi wa watu na haitaki kulipa madeni yake, je inakuwa serikali ya kitapeli kama wahuni wanaokopa benki na baadae hawalipi? Je, kuwe na utaratibu wa kuishtaki serikali na kuvishikilia baadhi ya vitu vya serikali ikiwa imeleta shida ya kutolipa kwa wakati?
Suala la madeni sio tu kwa sekta ya habari, nimesikia wadau kadhaa wakilalamika kutolipwa na serikali kiasi cha madeni hayo kukua au wakati mwingine kuathiri uchumi wa waliotoa huduma husika kwa serikali.
Kama serikali iko serious kwenye kukuza uchumi wa watu na haitaki kulipa madeni yake, je inakuwa serikali ya kitapeli kama wahuni wanaokopa benki na baadae hawalipi? Je, kuwe na utaratibu wa kuishtaki serikali na kuvishikilia baadhi ya vitu vya serikali ikiwa imeleta shida ya kutolipa kwa wakati?