Je, shetani/ibilisi anatoka koo zipi miongoni mwa koo za majini? Wazazi waliomzaa ni akina nani?

Mkuu hilo swali la sita nimekuuliza je ibilisi na uzao wake wote hawatakufa mpaka mwisho wa dunia au ni ibilisi mkuu pekee ndiye aliyepata nafasi ya kuishi mpaka mwisho wa dunia,

sijakuuliza kama ataingia motoni peke yake au na vizazi vyake

tofautisha baina ya maswali hayo mawili.
 
MKUU SOMA YALE MAJIBU YA AWALI KABISA...IBILISI MWANZO ALIKUWA UPANDE WA MUNGU TENA MCHAMUNGU.....IBILISI SIO KWAMBA NI WAKWANZA KUUMBWA AYA INSEMA MAJINI WALIUMBWA KWA MOTO AKIWA YEYE NI MMOJA WAPO NA WALIENDELEA KUZALIANA KAMA BINADAM YAN YY KUITWA IBILISI NI BAADA TU KUASI AMRI YA MUUMBA
 
Siyo tu siamini uwepo wa majini, sitaki kuamini, nataka kujua.
Bahati nzuri elimu ya majini ni ya kawaida sana hata leo hii ukitaka kuwaona utawaona ,kikubwa tu ufuate masharti yanayotakiwa.

Je upo tayari leo ukutane na majini?
 
IBILISI PEKEE
 
Kwa hiyo unamaanisha majini waliumbwa kwa mkupuo?
 
Mungu anajua zaidi.tutosheke na machache aliyotujaalia kuyajua kuhusu yeye.na matukio makubwa yaliyotokea kabla binadamu hakuwepo.
mungu ndo wa kwanza na wa mwisho.
 
NDUGU NIMEKUAMBIA MAJINI YANAZALIANA KAMA BINADAM
Mkuu unaelewa unachokizungumza?

Nilikuuliza kuhusu kuzaliwa kwa ibilisi pia nikakuuliza kuhusu wazazi wake na anatoka katika aina gani ya majini.

Ukanijibu kwamba Ibilisi pamoja na majini wengine waliumbwa kwa moto ,

Nikaendelea kukuswalika je Ibilisi ndiye jini wa kwanza kuumbwa au waliumbwa na majini wengine kwa mkupuo kabla ya kuanza kuzaliana?
 
Mkuu unaamini kuna shetani ?
Ni stiri za kutunga tu sawa a hadithi za kusadikika
 
MKUU NINAELEWA NINACHOKIZUNGUMZA LABDA WEWE NDIO UELEWI NINACHO KUAMBIA
ACHA JIBU ILI LIWE LA MWISHO BAADA YA HILI SITAKUWA NA NYONGEZA ELIMU YANGU ITAKUWA NDIO UKOMO WAKE
MUNGU ALIWAUMBA MAJINI KUTOKA NA NDIMI ZA MOTO YANI ME NA KE NAO WAKAZALIANA....KTK HAO MAJINI KUNA WALIOKUWA WAASI NA WACHAMUNGU...JINI MIONGONI MWA HAO WACHAMUNGU ALIKUWA NI IBILISI NAE ALIISHI MBINGUNI PAMOJA NA MALAIKA (ALIPEWA CHEO ICHO KUTOKANA NA UCHA MUNGU WAKE MANA ALIWEZA KUSUJUDU KTK ARDHI YOTE YA DUNIA YANI KILA UNAPOGUSA ARDHI YEYE ALISHAWEKAGA PAJI LA USO(SIJDA).....KWAMBA IBILISI ALIZALIWA KATIKA MAJINI ILA KWAMBA WAZAZI NI NANI NA NANI ILO SIYO SWALI LA MSINGI NI SAWA NA KUUZA FIMBO YA MUSSA ILIKUWA NI YA MTI GANI MPINGO AU MSONOBARI AU KUULIZA TUNDA ALILOKUWA ADAM NI PEAS AU CHUNGWA ILA KIFUPI IBILISI ALIZALIWA KATIKA MAJINI NA MAJINI ASILI YAO NI MOTO....MAJINI YANAZALIANA NA KUFA ILA IBILISI ATAISHI MPAKA KIAMA,IBILISI YEYE HAZALIANI BALI ANA WAFUASI WANAOMTII NA KUMFUATA.....
MKUU ULIZA MWASWALI YA MSINGI MANA SITAKUSHANGAA KUJA KUULIZA NA BIRTHDAY YA IBILISI ILIKUWA LINI.....MAJINI YALIYOANGAMIZWA NI YALE MAASI WEMA WALIISHI NA KIZAZI CHAO NDIO ICHIKAMA KIZAZI CHA ADAM KILIVYO ANGAMIZWA ZAMA ZA NUHU.....NARUHUSU KUKOSOLEWA
NA ALLAH ANAJUA ZAIDI
 
UHUSIANO BAINA YA JINNI NA Shaytwaan
Shaytwaan na Jinni asili yao ni moja, hapana hitilafu baina ya maulamaa kuhusu jambo hili, isipokuwa wamekhitalafiana katika suala; “Je Ibilisi ndiye baba wa Majinni (asili yao) mfano wa Adam ambaye ni baba yetu na asili yetu ?)”

Majibu;

Iblisi si asili yao, bali yeye ni miongoni mwao.

Allaah Anasema:

"Basi wakamsujudia isipokuwa Iblisi; yeye alikuwa miongoni mwa majini."

Al Kahf -50



Kwa vile Allaah Amemtaja Iblisi kuwa ni MIONGONI mwa majini, kwa hivyo yeye ni mmoja wao na si asili yao kama mfano wa Adam ('Alayhis Salaam) alivyokuwa asili ya wanadamu.



Tulisema kuwa wameitwa 'Majinni ' kwa sababu ya kutokuonekana kwao na sisi tumeitwa 'Insaan' kwa sababu ya kusahau kwetu, kwani neno 'Insan', asili yake linatokana na neno 'Nisiyaan', na maana yake ni Kusahau.

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:

"Adam alisahau na vizazi vyake vikasahau."

Ama neno 'Shaytwaan', katika lugha ya kiarabu maana yake ni 'Kila anayeasi na kupinga au kuzuwia au kushawishi viumbe wasiifuate njia ya Allaah', awe Jinni au Mwanadamu.

Allaah Anasema:

"Na nama hii tumemfanyia kila Nabii maadui (nao ni) Mashaytwaan katika watu na (Mashaytwaan katika) majini. Baadhi yao wanawafunulia wenziwao maneno ya kupambapamba ili kuwadanganya."

Al An am 112
 
Kwa hiyo kupanua uwezo wa maarifa juu yake na sisi waja wake ni vibaya?
Si vibaya ni vizuri sanaa.
ila ukimuwaza Sana mungu unaweza ukawa chizi.kuna siku nilishawahi kujiuliza hivi mungu ametokea wapi? kabla yake yeye kulikuwa na nani?mjombaa.nilianza kuogopa.
 
Kwa nini umesema Ibilisi hazaliani bali anawafuasi tu wanaomtii?

Kama ikiwa Ibilisi ni jini kama majini wengine kwa nini yeye asizaliane? Je hana kizazi wala jinsia?

Sisi binadamu asili yetu ni baba yetu Adamu ndio maana alipolaaniwa yeye basi vizazi vyake vyote (binadamu) tumelaaniwa mpaka tutubu ndipo Mungu ataturudisha tena peponi ,kama ingekuwa ni dhambi ya Adamu pekee basi binadamu wengine waliofuatia baada ya Adamu tukiweml mimi na wewe na sisi tungeishi peponi moja kwa moja kabla ya kuletwa duniani kama ingetokea tumeasi , lakini kitendo cha kuletwa huku duniani moja kwa moja inaonesha Mungu anataka tutubu ndipo aturudishe kule alipokusudia kutuweka hapo awali.


Sasa mantiki ya kukuuliza asili ya Ibilisi ni ipi ni kwamba nilitaka kujua kama majini wote wenye asili kama yake wamelaaniwa kama yeye au laah kuna wengine kutoka katika asili yake wametubu na kuwa waja wema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…