Guus
JF-Expert Member
- Jul 16, 2013
- 1,139
- 842
Habari wana forum?
Juzi nilikuwa nasafiri kutoka Dodoma kuelekea Singida wakati wa usiku. Nikiwa eneo la Sukamahela, kwa mbali upande wa kushoto nilikuwa naona mwanga mkubwa sana. Mwanzoni nilihisi kuna moto mkubwa, lakini kadri nilivyojitahidi kutazama sikuona "ukimove" kwa staili yeyote kuashiria ni moto. Kwa kweli nilikosa jibu, nikamuuliza mmoja wa "team members" niliyekuwa naye safarini ambaye ni mwenyeji wa mkoa huo, akaniambia kuwa hiyo ni mbuga ya maajabu. Usiku huwa inaonekana kama moto, na inatoa mwanga vivyo hivyo uonavyo.
Siku iliyofuata tulikuwa tukirudi Dodoma (bahati nzuri safari hii ilikuwa mchana). Nilijitahidi nisikopeze hata kope nikiwa maeneo yale ya inayosemwa ni mbuga. Safari hii ikiwa ni upande wa kulia, nilijitahidi sana kulitazama lile eneo. Kwa umbali uliopo toka barabarani, ilikuwa vigumu kutambua kama niliyoona ni nyasi ndefu au miti (lakini hakukuwa na majengo eneo lile).
Hapa nilipo najiuliza, hivi hii inayoitwa mbuga ya maajabu ipo, au ni macho yangu hayakufanikiwa kung'amua vizuri kitu kilichopo umbali ule??? (Msaada mwenye kulijua hili)
Juzi nilikuwa nasafiri kutoka Dodoma kuelekea Singida wakati wa usiku. Nikiwa eneo la Sukamahela, kwa mbali upande wa kushoto nilikuwa naona mwanga mkubwa sana. Mwanzoni nilihisi kuna moto mkubwa, lakini kadri nilivyojitahidi kutazama sikuona "ukimove" kwa staili yeyote kuashiria ni moto. Kwa kweli nilikosa jibu, nikamuuliza mmoja wa "team members" niliyekuwa naye safarini ambaye ni mwenyeji wa mkoa huo, akaniambia kuwa hiyo ni mbuga ya maajabu. Usiku huwa inaonekana kama moto, na inatoa mwanga vivyo hivyo uonavyo.
Siku iliyofuata tulikuwa tukirudi Dodoma (bahati nzuri safari hii ilikuwa mchana). Nilijitahidi nisikopeze hata kope nikiwa maeneo yale ya inayosemwa ni mbuga. Safari hii ikiwa ni upande wa kulia, nilijitahidi sana kulitazama lile eneo. Kwa umbali uliopo toka barabarani, ilikuwa vigumu kutambua kama niliyoona ni nyasi ndefu au miti (lakini hakukuwa na majengo eneo lile).
Hapa nilipo najiuliza, hivi hii inayoitwa mbuga ya maajabu ipo, au ni macho yangu hayakufanikiwa kung'amua vizuri kitu kilichopo umbali ule??? (Msaada mwenye kulijua hili)