MeinKempf
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 11,093
- 7,229
Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la viongozi mbali mbali wa matifa duniani kuja Tz kusaini mikataba ya uwekezajia katika rasilimali zetu, na Katika kufatilia kwangu mambo ya kiuchumi hasa uwekezaji nimekuja kubaini kuwa sijawahi kuona hata siku moja Tz inasema kuwa imeenda nchi yoyote hasa zile kubwa na zilizoendelea na kwenda kusaini mikataba mikubwa na minono ya kiuchumi na uwekezaji kama wafanyavyo wageni wanokuja hapa kwetu, je kuna mwenye kunisaidia uwekezaji na mikataba ambayo Tz imeenda huko nje na kusaini, kwa mfano:Mkulu wa kaya kwenda USA au china , Thailand, au Ujerumani na kusaini kuwa tz itaanza kuchimba dhahabu yao kwa mkataba fulani, au itaanza kuwinda wanyama wao au kujenga vitega uchumi vya maana (tofauti na balozi uchwara zetu) , naomba kuwasilisha nafasi ya tz katika kuwekeza nje ya nchi kwani yasije kuwa yale yale ya kina chief mangungo wa msovel.