Je, tetesi kwamba matokeo ya uchaguzi uliomalizika Simba Sc yanachangia kuathiri uwezo wa timu uwanjani, zina uzito kiasi gani?

Tumuulize msimamizi wa kimataifa Manzoki, atakuwa na majibu.........tulipowaambia mbumbumbu mmedharauliwa sana hamkutuelewa naona saizi akili imewakaa sawa
 
soka letu kivyetuvyetu (azam tv)
simba waliingia kwenye mabadiliko kichwa kichwa wakitafuta furaha ya muda mfupi.
leo mambo yapo dhahiri hawajui waanzie wapi?
zipo wapo 20 bl za MO?
 
Makundi yako mengi msimbazi na wengi hawamtaki mangungu hata yeye pia alipita kimafia kama 2020
 
Timu kufungwa kwako ni jambo geni ?
Sio jambo geni, hapa kinachonifanya nihisi kitu ni sababu ya tabia zetu za kiswahili, hizi tunazo tu, hakuna sababu ya kujitoa akili kwa kujiona sisi wazungu wakati figisu za mpira wetu sote tunazifahamu.

Lets face it, no need to hide anything.
 
Kuna uhusiano gani ya uchaguzi na timu kufanya vibaya?

Kwani viongozi wapya wamefanya badiliko lolote kiasi cha kuathiri performance ya timu?
Nimeshakupa sababu hapo juu, mpira wetu sio kama wa ulaya, unachofanya wewe ni kutumia akili/mawazo ya ulaya kuhukumu mpira wetu, hapo unakosea, mpira wetu na yanayotokea yahukumiwe kivyetu, sijui unanielewa dogo?
 
Tumuulize msimamizi wa kimataifa Manzoki, atakuwa na majibu.........tulipowaambia mbumbumbu mmedharauliwa sana hamkutuelewa naona saizi akili imewakaa sawa
Akili zipo sawa siku zote, ndio maana mnafundishwa masomo ya sheria kila mara[emoji1787][emoji1787]
 
Makundi yako mengi msimbazi na wengi hawamtaki mangungu hata yeye pia alipita kimafia kama 2020
Ndo ukae kwa kutulia, Mangungu ndio chaguo la wanasimba wengi kama hautaki nenda zako huko utopoloni Hatutaki washabiki maandazi kama wewe
 
soka letu kivyetuvyetu (azam tv)
simba waliingia kwenye mabadiliko kichwa kichwa wakitafuta furaha ya muda mfupi.
leo mambo yapo dhahiri hawajui waanzie wapi?
zipo wapo 20 bl za MO?
Hii pointi ya soka letu kivyetu vyetu ndio nataka wengi waione na kuikubali, wasijifiche kwenye kivuli cha soka la uzunguni wakati mpira wetu na yaliyomo.hayafanani hata kidogo na kinachotokea uzunguni.
 
Makundi yako mengi msimbazi na wengi hawamtaki mangungu hata yeye pia alipita kimafia kama 2020
Haya mambo yakijadiliwa wengine wanaogopa, huu ukweli kama upo lazima ufanyiwe kazi ili uishe, hakuna sababu ya kujificha kiuoga.

Kama Mangungu hapendwi lazima wajue huyo ndie alishinda wanachotakiwa kufanya sasa ni kumuunga mkono timu iwe moja, wanachofanya ni kuharibu kwa kudhani wanamkomoa Mangungu kumbe wanatuunganisha na wengine tusiohusika.
 
Suala sio kukomolewa mtu suala ni siasa zimetamalaki sana msimbazi
 
Ndo ukae kwa kutulia, Mangungu ndio chaguo la wanasimba wengi kama hautaki nenda zako huko utopoloni Hatutaki washabiki maandazi kama wewe
Tulia basi punga zeze
Wenye akili tumeiomba takukuru ifuatilie upya uchaguzi mkuu ulikuwa na maseke sana
 
Tulia basi punga zeze
Wenye akili tumeiomba takukuru ifuatilie upya uchaguzi mkuu ulikuwa na maseke sana
Hili la TAKUKURU sikuwahi kulisikia ..

Kwanini ushindi wa Mangungu uonekane kuwaudhi wengi, kwamba inaonekana hakuwa chaguo la mwekezaji, au wagombea wenzake?

Lakini kama wanachama walimpa ushindi kwa kura zilizopigwa na kuhesabiwa wazi, sioni sababu ya kuwa na kinyongo na ushindi wake ..
 
Simba hakuna makundi. Ni kiwango funi cha wachezaji. Just imagine boko anapata nafasi 5 hafungi na Sakho sehem ya kutoa pasi ananyonga kibaiskeli.
 
Fuatilia sana thread za jenta kuna point nyingi anazimwaga kimasihara
Kwa ujinga wetu tunamkejili lakini ndio hali halisi yq simba kwa sasa
 
Fuatilia sana thread za jenta kuna point nyingi anazimwaga kimasihara
Kwa ujinga wetu tunamkejili lakini ndio hali halisi yq simba kwa sasa
Hili la TAKUKURU ndio nimlisikia leo kwenye vyombo vya habari, pale Simba Sc kuna tatizo, watu wasijidanganye kuficha maradhi, kifo kitatuumbua ...
 
Hili la TAKUKURU ndio nimlisikia leo kwenye vyombo vya habari, pale Simba Sc kuna tatizo, watu wasijidanganye kuficha maradhi, kifo kitatuumbua ...
Tatizo lipo sana kwenye uongozi wa mangungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…