Je, tui la nazi ni salama kwa mgonjwa wa presha/ kisukari?

XII Tz

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2020
Posts
4,345
Reaction score
7,076
Habari wakuu,

Je, kwa mgonjwa wa presha/ kisukari ambaye ana jaribu kuondokana na vyakula vyenye mafuta, ni sahihi kula vyakula vilivyo ungwa kwa Tui la nazi ama karanga?

Natanguliza shukrani
 
Habari wakuu,

Je, kwa mgonjwa wa presha/ kisukari ambaye ana jaribu kuondokana na vyakula vyenye mafuta, ni sahihi kula vyakula vilivyo ungwa kwa Tui la nazi ama karanga?

Natanguliza shukrani
Kwa maelezo na tafiti zilizopo, bado wataalamu wanasigana kwenye ubora dhidi ya ubaya wa mafuta yapatikanayo kwenye nazi.

Hili linalenga zaidi kwenye:
1: Nazi kuwa na uwezo wa kuongeza mafuta mabaya(LDL).

2: Nazi kuwa na viinirishe vinavyoukina moyo thidi ya magonjwa/cardio-protective.

3: Nazi kuwa na manufaa ya mafuta mazuri/yanayohitajila mwilini(HDL).

4: Nazi kuweza kusaidia mpangilio mzuri wa mafuta husika.

Ushauri:

1: Kama unaweza kupata mafuta ya alizeti au olive ni bota zaidi.

2: Kama ndio mafuta pekee unaweka kupata ulipo, basi tumia kwa kiasi kidogo (wastani mdogo sana).
 
Shukrani sana mkuu

Sent from my SM-G950U using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…