Je, ubaguzi hufanywa na ‘weupe’ pekee?

Je, ubaguzi hufanywa na ‘weupe’ pekee?

nguvu

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2013
Posts
22,976
Reaction score
22,564
Aliyekuwa kocha wa Yanga ametimuliwa kwa kutamka maneno yanayoaminika ni ya kibaguzi kwa mashabiki kwa kuwafananisha washabiki na nyani na mbwa kubweka bweka hovyo.

Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar ndugu Paul Makonda wakati akikabidhi ofisi amesema wakati anafanya kazi kuna mbwa mwitu walikuwa wanabweka lakini sioni watu wakisema maneno ya kibaguzi.

Je, watu wapo kimya kuhusisha na ubaguzi kwakuwa Makonda ni mweusi mwenzetu?
 
Atakaelalamika ndio atakua mbwamwitu sasa. Maana hakuna alieambiwa mbwamwitu ila mbwa mwitu walikua wanabweka sasa ukilalamika basi ndio mbwekaji Unakua wewe.
 
Atakaelalamika ndio atakua mbwamwitu sasa. Maana hakuna alieambiwa mbwamwitu ila mbwa mwitu walikua wanabweka sasa ukilalamika basi ndio mbwekaji Unakua wewe.
Lakini inajulikana wazi alikuwa anawaita binaadam wenzie mbwa mwitu
 
Kocha aliwaita MASHABIKI Mbwa na Nyani,
Makonda kasema wakati anafanyakazi kuna Mbwa Mwitu walikua wanabweka,

Huoni kama ni mambo mawili tofauti?

Mtu akisema kwenye msafara wa Mamba na Kenge wapo, unaweza kureact kua umeitwa Mamba au Kenge? Wapi umetajwa?

Tafakari.
 
Duniani hakuna kitu kinaotwa "ubaguzi wa rangi" Ila ubaguzi upo.Dhana ianayojengeka ya ubaguzi wa rangi ninkutokana na ufinyu wa akili ya binadamu.Kama mambo Kama haya yangeachwa tu Basi hakuna ambako lingeendelea Ila kwa kuwa nao wanaikweza hii dhana Basi hii dhana nayo unajua kwa Kasi.Kwa mfano mtu alisema we mbwa,nyani,sokwe na huku wewe sio nyani wala sokwe inakuuma Nini?Mimi ningechukulia Kama hali ya kawaida.Ila ubaya Ni kubaguliwa katika vitu mfano ulitaka kupanda gari unazuiwa,ulitaka kuingia mgahawani au hotelini wanakutakaa huo ndo ubaguzi mbaya.Ni maoni yangu tu
 
Kocha aliwaita MASHABIKI Mbwa na Nyani,
Makonda kasema wakati anafanyakazi kuna Mbwa Mwitu walikua wanabweka,

Huoni kama ni mambo mawili tofauti?

Mtu akisema kwenye msafara wa Mamba na Kenge wapo, unaweza kureact kua umeitwa Mamba au Kenge? Wapi umetajwa?

Tafakari.
Hata kocha hakusema ni manyani au mbwa alisema mashabiki wa Yanga wanapiga tu makelele kama nyani au mbwa?
 
Duniani hakuna kitu kinaotwa "ubaguzi wa rangi" Ila ubaguzi upo.Dhana ianayojengeka ya ubaguzi wa rangi ninkutokana na ufinyu wa akili ya binadamu.Kama mambo Kama haya yangeachwa tu Basi hakuna ambako lingeendelea Ila kwa kuwa nao wanaikweza hii dhana Basi hii dhana nayo unajua kwa Kasi.Kwa mfano mtu alisema we mbwa,nyani,sokwe na huku wewe sio nyani wala sokwe inakuuma Nini?Mimi ningechukulia Kama hali ya kawaida.Ila ubaya Ni kubaguliwa katika vitu mfano ulitaka kupanda gari unazuiwa,ulitaka kuingia mgahawani au hotelini wanakutakaa huo ndo ubaguzi mbaya.Ni maoni yangu tu
Unasema duniani hakuna kitu kinaitwa ubaguzi wa rangi, hapo hapo umetoa mfano wa mtu kuzuiwa kupanda gari au kuingia mgahawani,
Umeshindwa kujua wapo wanaokatazwa kufanya hayo sababu ya rangi zao, yaani mgahawa unaandikwa "haturuhusu watu weusi" unadhani huo ni ubaguzi wa nini?
 
Hata kocha hakusema ni manyani au mbwa alisema mashabiki wa Yanga wanapiga tu makelele kama nyani au mbwa?
Lakini aliwazungumzia walengwa ambao ni Mashabiki wa Yanga, kwa kesi ya Makonda hajaweka ulinganisho, ila amesema mbwa mwitu, sasa binaadam akipanic kwa kauli hiyo lazima tumshangae.
 
Aliyekuwa kocha wa yanga ametimuliwa kwa kutamka maneno yanayoaminika ni ya kibaguzi kwa mashabiki kwa kuwafananisha washabiki na nyani na mbwa kubweka bweka hovyo, aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar ndugu Paul Makonda wakati anakabidhi ofisi amesema wakati anafanya kazi kuna mbwa mwitu walikuwa wanabweka lakini sioni watu wakisema maneno ya kibaguzi, je watu wapo kimya kuhusisha na ubaguzi kwakuwa Makonda ni mweusi mwenzetu?
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO

Sisi kwa sisi hizo ni kesi za kifamilia.......tutajuana wenyewe......
 
Eymael alisema "Mashabiki wa Yanga Wanapiga makelele tu kama Manyani na Wanabweka kama Mambwa."

Makonda kasema "Kuna Mbwa Mwitu walikuwa Wanabweka."

Eymael kataja Mashabiki wa Yanga, Mashabiki wa Yanga Wapo na Wanajijua na kujuilikana.

Makonda kataja Mbwa Mwitu tu lakini hakutaja Mtu wala kundi Fulani.

Sasa nani hapo mlalamikani wa kuwa kabaguliwa na Makonda?
Au wewe ndiye uliyeitwa Mbwa Mwitu tukusaidie kupiga kelele?
 
Duniani hakuna kitu kinaotwa "ubaguzi wa rangi" Ila ubaguzi upo.Dhana ianayojengeka ya ubaguzi wa rangi ninkutokana na ufinyu wa akili ya binadamu.Kama mambo Kama haya yangeachwa tu Basi hakuna ambako lingeendelea Ila kwa kuwa nao wanaikweza hii dhana Basi hii dhana nayo unajua kwa Kasi.Kwa mfano mtu alisema we mbwa,nyani,sokwe na huku wewe sio nyani wala sokwe inakuuma Nini?Mimi ningechukulia Kama hali ya kawaida.Ila ubaya Ni kubaguliwa katika vitu mfano ulitaka kupanda gari unazuiwa,ulitaka kuingia mgahawani au hotelini wanakutakaa huo ndo ubaguzi mbaya.Ni maoni yangu tu

Ingawa Mimi mtu akiniita mweusi sikereki lakini Ubaguzi wa Rangi upo wala usibishe! South Afrika mpaka leo kuna maeneo hukanyagi kama wewe ni mweusi.
China wakati wa Korona watu wesi walichokutana nacho usiombe wakuhadithie.
 
Ingawa Mimi mtu akiniita mweusi sikereki lakini Ubaguzi wa Rangi upo wala usibishe! South Afrika mpaka leo kuna maeneo hukanyagi kama wewe ni mweusi.
China wakati wa Korona watu wesi walichokutana nacho usiombe wakuhadithie.
Ni kweli Hilo hata Mimi Ndio sipendi,Yani kuzuiwa kufanya shughuli fulani kwa sababu ya rangi ya ngozi,mfano baadhi ya migahawa unakuta Ni ya wahindi tu ukiingia mweusi unakatazwa hapo sio sawa.Ila eti unalalamika kuwa nimeitww nyani na wakati wewe sio mtu huo Ni utoto.Ubaguzi wa rangi wa kumzuia mchezaji mweusi au wa Dino fulani kujifunga na timu yenu huo ndo mbaya
 
Back
Top Bottom