Je, ulishawahi kuombwa kitu na ndugu, jamaa au rafiki akiwa mgonjwa bahati mbaya akafa haujamtimizia?

Je, ulishawahi kuombwa kitu na ndugu, jamaa au rafiki akiwa mgonjwa bahati mbaya akafa haujamtimizia?

Blueface

Member
Joined
May 2, 2020
Posts
46
Reaction score
47
Nikiwa kwenye mtihani wa taifa kidato cha pili, baba alisafiri kwenda kijijini ambako mama yake ambaye ni bibi yangu alikuwa anaumwa sana.Huyu bibi alikuwa ananipenda sana.

Bahati mbaya wakati anaumwa sana na kuzidiwa alikua anahitaji anione kabla hajafa. Kama ujuavyo mabibi wanavyopenda wajukuu kiukweli alimsihi sana baba anataka anione. Hivyo baba alikuwa anavutavuta mda kwa kumfariji ili nikimaliza pepa tu niende kijijini nikamuone. Maskini, Mungu nae ana mipango yake akamchukua kabla sijamaliza mitihani.

Baada ya kumaliza pepa nilienda msibani tayari akiwa ameshazikwa siku kadhaa zilizopita. Hali ile ilinihuzunisha sana kwani nilikuwa nampenda sana bibi yangu.

Watu wanapokaribia kufa huomba wapendwa wao wafanyiwe vitu flani. Mwingine anaweza taka apikiwe chakula Fulani, mwingine ataomba aletewe juisi, mwingine atataka nguo flani anayoipendaga. Vipi wewe ulishawai kwa bahati mbaya ukashindwa kutimiza ulichoombwa na marehemu awe rafiki, ndugu au jamaa?

Unapomkumbuka unapata hisia gani?
 
Nilikua na mshikaji wanaishi gheto na kaka yake. Alikua anaumwa nilivyopita magetoni kuwatembelea nikamwambia kesho tutaenda hosptal kama saa nne hivi. Kipindi hicho nimemaliza six napiga mishe mishe zangu navihela mbuzi ninavyo. Daaah kesho yake naenda saa nne naona watu kibao nje kwa wale washikaji kufika naambiwa mshikaji ameisha fariki. Mpaka leo nikikumbuka naumia sana sana. Linalo wezekana leo lisingoje kesho ndio nilicho jifunza.
 
Da!Hiyo hali huwa inaumiza sana kila ukikumbuka unaiona picha ya marehemu inakujia kichwani
 
Mama yangu mdogo aliniomba mchango fulani kwa ajili ya mambo ya kanisani kwao. Akaugua na kufariki kabla sijatoa ule mchango...

Ile hali ilinisumbua kwa muda....liwezekanalo leo lisingoje kesho.
 
Nilikuwa na rafiki wa tangu secondary ambaye tulikuwa na kawaida ya kila vicent tunavyovipata vitaishia kwenye nguo za Karume na Mwenge

Baada ya kumaliza secondary mimi nikaenda mkoa mwingine yeye akabaki Dar lakini mawasiliano na ukaribu ulikuwepo kama mwanzo

Kuna kipindi nilikaribia likizo ya kurudi Dar tukapanga nikirudi tukasuke nywele sare sare na picha tukatumiana za mtindo tutakaosuka!!

Ilikuwa kama siku mbili hivi kabla sijarudi akaniambia kichwa kinamuuma sana,mie nikamshauri anywe painkiller na maji mengi apumzike akakubali tukaagana.....ile siku ndio ilikuwa mara ya mwisho kusikia sauti yake
Dada yake alinipigia kuniambia mdogo wake alizidiwa akapelekwa Muhimbili na kufia huko!!

Hadi sasa siamini japo imepita miaka miwili tangu afariki lakini nafeel kama ipo siku nitakutana nae hata njiani
 
[SUB]Mie nilimpromise wife kumnunulia wife smartphone kali , baada ya simu yake ya mwanzo kuharibika. [/SUB]
[SUB]Matokeo yake ikawa kila siku ananikumbushia lakini nilishindwa kutimiza ahadi hio kwani kila siku pesa yangu yote niliimalizia kwenye matibabu yake kwani aliugua kwa mda mrefu mpka alipofariki[/SUB]
 
[SUB]Mie nilimpromise wife kumnunulia wife smartphone kali , baada ya simu yake ya mwanzo kuharibika. [/SUB]
[SUB]Matokeo yake ikawa kila siku ananikumbushia lakini nilishindwa kutimiza ahadi hio kwani kila siku pesa yangu yote niliimalizia kwenye matibabu yake kwani aliugua kwa mda mrefu mpka alipofariki[/SUB]
Daa pole sana
 
Kuna siku kitambo kidogo nilipokea sms toka kwa wifi yangu ambayo niliona tu kakosea kutuma kabla sijamjibu akanitumia tena 'Sorry wii nilikua namtumia kaka yako' me nikamjibu 'naona kuna mtu kanimiss, itabidi nijilete huko weekend hii' akacheka, bas tukachat chat pale badae tukaagana usiku mwema kwa miadi weekend ntaenda kumuona.
Kesho yake usiku mida ya sa 3 nkapigiwa sim kuwa wifi yangu amepata ajali na bahati mbaya amefariki niliumia sana nikakumbuka na ahadi yetu ila Mungu alikua amepanga lingine.
 
Back
Top Bottom