Stephen Ngalya Chelu
JF-Expert Member
- Oct 31, 2017
- 8,252
- 18,335
Hivi majuzi mama alinisimulia tukio ambalo hakuwa amewahi kunisimulia hapo kabla na likanifanya nishikwe na baridi ya huzuni na hofu na nikawaza mengi sana.
Iko hivi....
Nilikuwa nina mwezi mmoja tu tangu nizaliwe ambapo tukio hili likitokea. Siku hiyo ilikuwa siku ya kwanza mimi kutolewa nje (sebuleni) tangu nizaliwe. Mama alinichukua na kunipakata akiwa amekaa sebuleni. Katika hali isiyo tarajiwa, alikuja mwanamke mmoja akiwa anakimbia na kuingia sebuleni alipokuwa amekaa mama. Mwanamke huyo alikuwa anafukuzwa na mumewe ambaye walikuwa wanagombana muda huo.
Mwanaume huyo alikuwa ameshika kafimbo kanene kafupi wakati anamfukuza mwanamke wake. Sasa huyo mwanamke akawa anajizungusha alipokuwa amekaa mama ambaye alikuwa amenipakata mimi wakati huo. Wakawa wanazungushana hapo, mke anajikinga kwa kumzunguka mama, na mumewe anazunguka akiwa ameshika fimbo anataka ampige mkewe. Mama akawa amepanic, anajaribu kunyanyuka anashindwa kwa kuhofi a usalama wa mtoto(mimi) akabaki anapiga kelele tu huku akiwa anajaribu kunikinga nisidhurike.
Sasa kitu cha hatari ni kuwa, mzee alipoona kuwa hatimizi lengo lake la kumbutua mkewe, akaamua kurudha ile fimbo ili ampige mkewe. Kwa mstuko mama alinyanyua mkono kwa hamaki kunikinga maana ilikuwa imenilenga kabisa kichwani. Kwa kitendo cha yeye kunyanyua mkono aliiparaza ikapita sentimita chache sana kutoka usawa wa kichwa changu, na ikamkosa mlengwa pia(mke wa huyo mzee). Kwa maelezo ya mama, anadema laiti kama ile fimbo igemgonga sawasawa mkononi, mkono wake ungweza kuvunjika mara kadhaa, sasa imagine ingekipata kichwa cha mtoto wa mwezi mmoja!!
Baada ya tukio lile, yule mwanamke alikimbia nje na mumewe akamfuata huko na inadaiwa hawakusikia tena kelele za watu wakigombana tena. Ni kama ugomvi ulisha pale tu. Mama alilia sana siku hiyo, imagine first born anapitia katika hatari kubwa kama hiyo katika siku za awali tu za maisha yake!!!!
Kuna mengi sana ya kuhatarisha maisha nimeyapitia kitoka umri wa miaka 0-4, hadi wazazi hawaamini kama nimekua na nikiwa na afya njema kabisa.
Tuwapende na kuwaheshimu wote waliotupigania wakati sisi tukiwa hatujui hili wala lile.
Iko hivi....
Nilikuwa nina mwezi mmoja tu tangu nizaliwe ambapo tukio hili likitokea. Siku hiyo ilikuwa siku ya kwanza mimi kutolewa nje (sebuleni) tangu nizaliwe. Mama alinichukua na kunipakata akiwa amekaa sebuleni. Katika hali isiyo tarajiwa, alikuja mwanamke mmoja akiwa anakimbia na kuingia sebuleni alipokuwa amekaa mama. Mwanamke huyo alikuwa anafukuzwa na mumewe ambaye walikuwa wanagombana muda huo.
Mwanaume huyo alikuwa ameshika kafimbo kanene kafupi wakati anamfukuza mwanamke wake. Sasa huyo mwanamke akawa anajizungusha alipokuwa amekaa mama ambaye alikuwa amenipakata mimi wakati huo. Wakawa wanazungushana hapo, mke anajikinga kwa kumzunguka mama, na mumewe anazunguka akiwa ameshika fimbo anataka ampige mkewe. Mama akawa amepanic, anajaribu kunyanyuka anashindwa kwa kuhofi a usalama wa mtoto(mimi) akabaki anapiga kelele tu huku akiwa anajaribu kunikinga nisidhurike.
Sasa kitu cha hatari ni kuwa, mzee alipoona kuwa hatimizi lengo lake la kumbutua mkewe, akaamua kurudha ile fimbo ili ampige mkewe. Kwa mstuko mama alinyanyua mkono kwa hamaki kunikinga maana ilikuwa imenilenga kabisa kichwani. Kwa kitendo cha yeye kunyanyua mkono aliiparaza ikapita sentimita chache sana kutoka usawa wa kichwa changu, na ikamkosa mlengwa pia(mke wa huyo mzee). Kwa maelezo ya mama, anadema laiti kama ile fimbo igemgonga sawasawa mkononi, mkono wake ungweza kuvunjika mara kadhaa, sasa imagine ingekipata kichwa cha mtoto wa mwezi mmoja!!
Baada ya tukio lile, yule mwanamke alikimbia nje na mumewe akamfuata huko na inadaiwa hawakusikia tena kelele za watu wakigombana tena. Ni kama ugomvi ulisha pale tu. Mama alilia sana siku hiyo, imagine first born anapitia katika hatari kubwa kama hiyo katika siku za awali tu za maisha yake!!!!
Kuna mengi sana ya kuhatarisha maisha nimeyapitia kitoka umri wa miaka 0-4, hadi wazazi hawaamini kama nimekua na nikiwa na afya njema kabisa.
Tuwapende na kuwaheshimu wote waliotupigania wakati sisi tukiwa hatujui hili wala lile.