Je, umewahi kuvunjiwa mkataba?

Je, umewahi kuvunjiwa mkataba?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
1609999284723.png

Sheria ya Mikataba inabainisha kuwa wakati ambapo mkataba unakuwa umevunjika, mhusika ambaye ameathirika na uvunjwaji huo anastahili kupata fidia ya hasara iliyojitokeza kutoka kwa aliyesababisha ukiukwaji wa mkataba huo, au fidia iliyosababishwa na kujitokeza kwa mambo fulani ambayo ni ya kawaida katika uvunjaji wa mkataba, au ambayo wahusika walijua walipofanya mkataba kuwa yaweza kutokea iwapo mkataba utavunjwa.

Aidha iwapo mkataba umevunjika, kama kiwango cha fedha kimetajwa kwenye mkataba kuwa ndio malipo
yatakayofanywa kwa kuvunjwa kwa mkataba, au kama mkataba umeelekeza adhabu nyingine yoyote, mhusika anayelalamika kuhusu uvunjaji huo unastahili fidia inayoeleweka isiyozidi kiwango kilichotajwa au kama itakavyokuwa, adhabu iliyowekwa.
 
Upvote 2
Safii sana Jamii Forum kwa elimu mnayoitoa kwa Jamii yetu hakika ina manufaa makubwa sana kwa kuwafanya wananchi kutambua haki zao za msingi pale inapotokea changamoto kama hii
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom