Je unafahamu ni kwa muda gani vyakula vinatakiwa kukaa ndani ya friji?

Je unafahamu ni kwa muda gani vyakula vinatakiwa kukaa ndani ya friji?

Gudboy

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2009
Posts
867
Reaction score
82
Inapokuja katika swala la utayarishaji msosi majumbani kwetu hatuwezi kutoikubali kazi ya friji katika mpango mzima wa kuhifadhi chakula. Kwa kuhifadhi vyakula katika jokofu kunaokoa mda pale unapotaka kupika msosi wa haraka.


Swali la kujiuliza ni vyakula hivi tunavyoviweka katika majokofu yetu vinaweza kuwa salama kwa mahitaji ya mwanadamu ndani ya mda gani? wataalamu wanasema chakula chochote kitakacho hifadhiwa ndani ya nyuzi 0 za Fahrenheit kitakuwa salama kwa kuliwa kwa mda wote lakini ubora wa chakula hautakuwa uleule.

Tumekuorodeshea baadhi ya vyakula na mda wake unaoruhusu kuhifadhiwa kwenye jokofu.


Mkate: Miezi 2 mpaka 3

Nyama iliyopikwa: Miezi 2 mpaka 3

Matunda: Miezi 8 mpaka 12

Sausage: Mwezi 1 mpaka 2

Soupu: Miezi 2 mpaka 3

Vipande vya nyama ya kuku ambayo haija pikwa: Miezi 9

Kuku mzima ambae hajapikwa: Mwaka 1

Mboga za majan : Miezi 8 mpaka 12

Ni muhimu ukazingatia haya:

Kama chakula ni chamoto subiri kipoe kwanza ndio ukiweke kwenye jokofu,hiyo inasaidia kukifanya kipate ubaridi mapema ambapo ubora wake hautapotea kwa haraka. Usigandishe vyakula ambavyo vipo katika makopo au mayai hiyo itavifanya kupata nyufa na bacteria kuingia. Ni muhimu ukafuata maelezo kwa vyakula vilivyotengenezwa viwandani.

 
Du! sup ndani ya friji mwezi mzima! Acha niendelee kubaki bongo-asbuhi unaingia kwa mangi unapiga supu inayotokota jikoni na ng'ombe kachinjwa usiku huo huo!
 
Bwana mkubwa unatupa matata kwa kutumia kipimo cha Fahrenheit (Nani anaituma duniani isipokuwa Marekani???) .

Sawa unamaanisha vyakula vilivyogandishwa kwa -17.8 °C. Kwa hiyo si friji ya kawaida.

Hatari inatokea hasa katika mazigira ambako umeme unaweza kukatwakatwa. Maana kama vyakula vilivyoganda vinaanza kupoa bakteria kama salmonela zinaweza kuingia, hapa hatari inaanza hata kama baadaye umeme unaudi.
 
we umejaribu kuweka kuku mwezi mmoja ukamla au vipi hapo hayo huko huko kwao sie hatuna friji na kiporo tunakula
Conquest-ujanja wao maisha yetu yale yale:hand:
 
Back
Top Bottom