Je, Unajua Pesa Yako Inaenda Wapi? Tuangalie Matumizi ya Watanzania kwa Bidhaa za Ndani na Nje

Je, Unajua Pesa Yako Inaenda Wapi? Tuangalie Matumizi ya Watanzania kwa Bidhaa za Ndani na Nje

E-Maestro

Member
Joined
Nov 25, 2013
Posts
29
Reaction score
31
Habari Wana JamiiForums,

Natumaini mko salama na mnaendelea vizuri na shughuli za kila siku. Leo ningependa tujadili jambo muhimu sana linalotuhusu sisi sote kama Watanzania. Tujaribu kuangalia jinsi tunavyotumia pesa zetu baada ya kupata ujira wetu na ni kwa kiasi gani tunachangia uchumi wa ndani au nje ya nchi(Uchumi wa wengine).

Sote tunafahamu kuwa mwisho wa mwezi ni wakati ambao wengi wetu hupokea mishahara au malipo ya kazi tulizofanya. Lakini, je, umewahi kujiuliza pesa yako inaenda wapi baada ya kuipokea? Katika matumizi yetu ya kila siku, kuna bidhaa tunazonunua ambazo zinazalishwa hapa nchini na nyingine zinazoagizwa kutoka nje. Hii ina maana kuwa matumizi yetu yanaweza kuimarisha uchumi wa ndani au kuchangia uchumi wa nchi nyingine. kujikuta kumbe tunawafanyia kazi wachina! Au wajapani. Au hata majirani zetu wakenya!

Mifano ya Bidhaa za Ndani na Nje:
  • Bidhaa za Ndani: Mikate ya viwanda vya ndani, mchele wa Kyela, maziwa ya Tanga Fresh, matunda na mboga kutoka kwa wakulima wa ndani.
  • Bidhaa za Nje: Perfumes, TV, majiko ya gesi, vifaa vya elektroniki, na bidhaa nyingine ambazo hatuzalishi hapa nchini.
Swali la Msingi:Kwa wastani, inakuchukua muda gani kutumia pesa yako kwa bidhaa ambazo hazizalishwi Tanzania baada ya kupata mshahara wako? Je, unadhani tunatumia zaidi kwenye bidhaa za ndani au za nje?

Faida za Kununua Bidhaa za Ndani:

  1. Kuimarisha Uchumi wa Ndani: Kununua bidhaa za ndani husaidia kuongeza ajira na kukuza uchumi wa nchi yetu.
  2. Kuunga Mkono Wazalishaji wa Ndani: Tunaposaidia viwanda na wakulima wa ndani, tunachangia maendeleo yao na kuongeza ubora wa maisha.
  3. Kupunguza Utegemezi: Tunapunguza utegemezi wa bidhaa za nje na kuimarisha uwezo wetu wa kujitegemea.
Ningependa kusikia mawazo na uzoefu wenu kuhusu hili. Mnachukuliaje matumizi yenu ya pesa baada ya kupata ujira? Je, ni rahisi kubaki na pesa ndani ya nchi au tunavutiwa zaidi na bidhaa za nje?

Karibuni tujadili na tushirikiane mawazo kuhusu jinsi tunavyoweza kusaidia uchumi wa Tanzania kwa kutumia pesa zetu kwa bidhaa za ndani. Kwa ajiri ya uchumi wetu!

Asanteni sana!
 
Tuanze kwa kuangalia matumizi ya serikali yetu.

Kutumia Shs 400m kununua V8 moja na yananununiliwa zaidi 200 kwa mwaka ni matumizi mabaya.

Kusafirisha watumishi takriban 100 kwenye msafara wa rais au waziri na kuwalipa posho ambazo ni zaidi ya mishahara yao ni matumizi mabaya
 
Tuanze kwa kuangalia matumizi ya serikali yetu.

......Kutumia Shs 400m kununua V8 moja na yananununiliwa zaidi 200 kwa mwaka ni matumizi mabaya.
....Kusafirisha watumishi takriban 100 kwenye msafara wa rais au waziri na kuwalipa posho ambazo ni zaidi ya mishahara yao ni matumizi mabaya/
Pazito hapo. Lakini pia sio sababu ya sisi kutojitathmini! Kila kitu ni hatua. Huwezi fanya yote kwa wakati mmoja! Atapatikana kiongozi siku moja atasikia kilio cha Watanzania. na Mambo yatakaa sawa! Kwa sasa, TUISHI NAO TU!
 
Pazito hapo. Lakini pia sio sababu ya sisi kutojitathmini! Kila kitu ni hatua. Huwezi fanya yote kwa wakati mmoja! Atapatikana kiongozi siku moja atasikia kilio cha Watanzania. na Mambo yatakaa sawa! Kwa sasa, TUISHI NAO TU!
Pesa zinazofujwa na serikali ni zetu.
 
Okay... nizetu. Tunafanye sasa????
TATIZO LETU NI CCM TU. Mambo mengine yangewezekana kama CCM wangeondoka, kuendelea kuwa nao hatuwezi kupata suluhu ya tatizo hata moja kwa sababu, watunga sera, kanuni na sheria ni wao. Na WAHALIFU, na wabadhilifu wa mali za umma ni wao.
 
MImi natumia laki 1.5 kwa siku kama sehemu ya matumizi binafsi bado familia kwa UJUMLA sijui nifafanue hiyo laki natumiaje...? 😃😃😃🙌🙌🙌
 
Habari Wana JamiiForums,

Natumaini mko salama na mnaendelea vizuri na shughuli za kila siku. Leo ningependa tujadili jambo muhimu sana linalotuhusu sisi sote kama Watanzania. Tujaribu kuangalia jinsi tunavyotumia pesa zetu baada ya kupata ujira wetu na ni kwa kiasi gani tunachangia uchumi wa ndani au nje ya nchi(Uchumi wa wengine).

Sote tunafahamu kuwa mwisho wa mwezi ni wakati ambao wengi wetu hupokea mishahara au malipo ya kazi tulizofanya. Lakini, je, umewahi kujiuliza pesa yako inaenda wapi baada ya kuipokea? Katika matumizi yetu ya kila siku, kuna bidhaa tunazonunua ambazo zinazalishwa hapa nchini na nyingine zinazoagizwa kutoka nje. Hii ina maana kuwa matumizi yetu yanaweza kuimarisha uchumi wa ndani au kuchangia uchumi wa nchi nyingine. kujikuta kumbe tunawafanyia kazi wachina! Au wajapani. Au hata majirani zetu wakenya!

Mifano ya Bidhaa za Ndani na Nje:

  • Bidhaa za Ndani: Mikate ya viwanda vya ndani, mchele wa Kyela, maziwa ya Tanga Fresh, matunda na mboga kutoka kwa wakulima wa ndani.
  • Bidhaa za Nje: Perfumes, TV, majiko ya gesi, vifaa vya elektroniki, na bidhaa nyingine ambazo hatuzalishi hapa nchini.
Swali la Msingi:Kwa wastani, inakuchukua muda gani kutumia pesa yako kwa bidhaa ambazo hazizalishwi Tanzania baada ya kupata mshahara wako? Je, unadhani tunatumia zaidi kwenye bidhaa za ndani au za nje?

Faida za Kununua Bidhaa za Ndani:

  1. Kuimarisha Uchumi wa Ndani: Kununua bidhaa za ndani husaidia kuongeza ajira na kukuza uchumi wa nchi yetu.
  2. Kuunga Mkono Wazalishaji wa Ndani: Tunaposaidia viwanda na wakulima wa ndani, tunachangia maendeleo yao na kuongeza ubora wa maisha.
  3. Kupunguza Utegemezi: Tunapunguza utegemezi wa bidhaa za nje na kuimarisha uwezo wetu wa kujitegemea.
Ningependa kusikia mawazo na uzoefu wenu kuhusu hili. Mnachukuliaje matumizi yenu ya pesa baada ya kupata ujira? Je, ni rahisi kubaki na pesa ndani ya nchi au tunavutiwa zaidi na bidhaa za nje?

Karibuni tujadili na tushirikiane mawazo kuhusu jinsi tunavyoweza kusaidia uchumi wa Tanzania kwa kutumia pesa zetu kwa bidhaa za ndani. Kwa ajiri ya uchumi wetu!

Asanteni sana!
hata viongoz wanatumia mashangingi cm computer vyte vnatoka nje so we usjal ht iv vya nje km ulivosema pafyum sijui saa vinanunuliw na wa tanzania wanauza wapat faida na wanalip kodi pia ukumbuke ht sie tunauza sato sangara korosho mchele alizet maharage parachich ngozi mahind kwenda nje...dunia inaznguka na hela inaznguka pia acha ubinafs
 
Back
Top Bottom