Je, unaweza kupona bila dawa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363


MAGONJWA mengi hayahitaji tiba. Miili ina njia mbalimbali za kukinga maradhi. Njia hizi ni bora zaidi kuliko kutumia dawa.

Magonjwa mengi, kama vile mafua na fluu hupona bila ya dawa.

Ili kusaidia kukinga na kishinda maradhi ni lazima kujimudu katika hali hizi;
- kujiweka katika hali ya usafi.
- Kula chakula bora.
- Kupumzika vya kutosha
- Kufanya kazi na mazoezi

Hata kama ugonjwa ni wa kutisha na unahitaji dawa, mwili unaopambana na ugonjwa, dawa huwa zinasaidia tu. Jambo la muhimu ni usafi, kupumzika na kula chakula bora.
Huduma za kiafya hazitegemei dawa.

Hata kama unaishi sehemu ambazo hazina dawa za kigeni, kuna mengi unayoweza kufanya ili ukinge na kutibu magonjwa mengi mradi tu, uelewe namna ya kufanya.

Magonjwa mengi yanaweza kukingwa na kutibiwa bila ya kutumia dawa.
Kama watu wanaelewa namna ya kutumia maji vizuri, itakuwa njia nzuri ya kinga na kuponyesha magonjwa bila ya kutumia dawa.

Kuponya kwa maji
Wengi tunaishi bila ya kutumia dawa lakini, hakuna hata mmoja anayeweza kuishi bila maji. Ukweli ni kwamba, zaidi ya asilimia 57 ya mwili wa mwanadamu, ni maji.

Kama kila aishiye vijijini angeweza kutumia maji vizuri, basi magonjwa na vifo hasa kwa watoto wadogo yangepungua sana.

Kwa mfano, matumizi mazuri ya maji ni msingi wa kuzuia na kutibu ugonjwa wa kuharisha. Kuharisha ni ugonjwa mkubwa na wenye kuleta vifo kwa watoto wadogo katika sehemu nyingi ulimwengu. Maji machafu husababisha ugonjwa huu pia.

Njia mojawapo muhimu ya kuepuka ugonjwa huu wa kuharisha ni kuchemsha maji ya kunywa na kupikia hasa kwa ajili ya watoto wachanga.

Chupa ya maziwa na vyombo vingine vya mtoto mchanga, vinabidi pia vichemshwe kabla na baada ya kutumiwa.

Mikono lazima ioshwe kwa sabuni baada ya kutoka msalani, kabla ya kula chakula.
Ukosefu wa maji mwilini ni sababu kubwa ya vifo kwa watoto wenye ugonjwa wa kuharisha.

Kama mtoto anapewa maji mengi yenye chumvi na sukari na asali kidogo, hii itakinga na hata kutibu upungufu wa maji mwilini.

Kumpa mtoto mwenye kuharisha maji mengi, itamfaa zaidi kuliko dawa. Ukweli ni kuwa umpapo maji ya kutosha hutahitaji kumpa dawa yoyote ya kutibu kuharisha.

Nyakati ambazo matumizi mazuri ya maji yanasaidia zaidi kuliko dawa.

Kuhara, minyoo, ugonjwa wa tumbo namna ya kukinga, tumia maji, chemsha maji ya kunywa, osha mikono.
- Ugonjwa wa ngozi
- Oga kila siku

- Vidonda vyenye usaha, pepopunda; osha vidonda kwa maji na sabuni
Kutibu:

Kuharisha na upungufu wa maji mwilini, tumia maji, kunywa maji mengi.
-Homa; Osha kiwiliwili na maji baridi
-Homa kali
-Ogesha kiwiliwili kwa maji baridi
-Mkojo mchafu (hasa kwa akinamama)
-Kunywa maji mengi

-Kukohoa, pumu, nimonia, kifaduro - kunywa maji mengi na fukiza mvuke wa maji ya moto.
-Vidonda, baka la ngozi au kichwa na chunusi

-Sugua kwa maji ya sabuni.
-Madonda ya vijidudu yanayochonota - kanda kwa maji ya moto.

-Maumivu ya misuli na viungo
-Kanda kwa maji moto

-Kuwashwa na malengelenge ya ngozi
-Kanda kwa maji baridi.
 


Kuungua moto kidogo

- Paweke ndani ya maji baridi.
- Magogore au mafindofindo(sore throat au tonsillitis)
- Sukutua maji moto ya chumvi.
- Esidi au takataka iliyoingia jichoni - osha upesi kwa maji baridi.

Mafua - vuta maji ya chumvi

-Kuvimbiwa na kupata choo kigumu
-Kunywa maji mengi, pia kuinika ni bora kuliko dawa za kulainisha choo. Usitumie mara kwa mara).

Kwa kila mfano uliotolewa awali,(isipokuwa nimonia), inaonesha kwamba kama maji yatatumiwa vizuri mara nyingi, dawa hazitahitajika.

Somo hili litapanua mawazo mbalimbali ya kuweza kuponyesa bila kutumia dawa. Tumia dawa tu, kama zinahitajika kweli.

Matumizi mazuri na mabaya ya madawa ya kisasa

Baadhi ya madawa yanayouzwa na mkemia au maduka ya vijijini, husaidia sana.
Watu wengine wana tabia ya kutumia dawa nzuri vibaya na hii humuumiza mgonjwa ili dawa iweze kufanya kazi yake ni lazima itumiwe vizuri.

Watu wengi wakiwemo madaktari na waganga, hutoa dawa nyingi kuliko inavyotakiwa na kufanya hivyo, huzidisha magonjwa na vifo.
Kuna hatari katika matumizi ya madawa.

Dawa fulani zina hatari zaidi kuliko nyingine. Lakini, watu wengine hutumia dawa zenye hatari kwa magonjwa madogo madogo tu.
Watoto wengi wamekuwa wakipoteza maisha kwa sababu mama yake alimpa dawa ya hatari "Chlorophenical" eti kutibu mafua tu. Usitumie dawa yenye hatari kwa ugonjwa mdogo.

Mwongozo wa kutumia dawa:

- Tumia dawa tu, ikiwa ni lazima.
- Kila dawa uitumiayo, ni lazima ufahamu matumizi yake barabara na namna ya kujihadhari.
- Hakikisha unatumia kipimo kamili.
- Kama dawa haisaidii au inaleta matatizo, usiitumie tena
- Kama huna hakika, muone mganga.
 



Hatari za kutumia dawa vibaya

Hii ni orodha ya makosa ya kawaida tunayofanya tunapotumia madawa ya kisasa. Matumizi mabaya ya madawa yafuatayo yanaleta vifo kila mwaka, kuwa mwangalifu Chloramphenical (chloromycetin) -Kwa bahati mbaya, dawa hii hupendelewa sana kutumiwa kwa magonjwa madogo madogo kama vile kuharisha. Hii, ni hatari sana.

- Dawa hii inatumika kutibu magonjwa kama vile homa ya matumbo. Isitolewe kwa watoto wachanga.
- Oxtocin(pitocin) pituitrin na Ergonovine (Ergotrate) - kwa bahati mbaya wakunga hutumia dawa hizo

kuharakisha kuzaliwa kwa mtoto au kumpa nguvu mzazi wakati akiwa na uchungu wa kujifungua.
Matumizi ya namna hii yana hatari sana. Unaweza kumwua mama au mtoto. Zitumie tu, kwa kuzuia kutoka damu baada ya mtoto kuzaliwa.

- Sindano za dawa: Imani kuwa sindano ni bora kuliko vidonge si ya kweli. Mara nyingi dawa za kunywa zinafanya kazi vizuri zaidi kupita sindano. Pia, dawa nyingi zitolewazo kwa sindano huhatarisha maisha kuliko za kunywa. Matumizi ya sindano lazima yapunguzwe.

- Penisilini: Penisilini hufanya kazi kwa magonjwa fulani ya kuambukiza. Ni makosa kutumia dawa hii kwa shida za kustuka misuli, kujiponda, aina yoyote ya maumivu au homa.

Kwa kawaida, majeraha yoyote ambayo hayakuchubua ngozi, ijapokuwa kuna uvimbe mkubwa ni vigumu vijidudu kuingia kwa hivyo hakuna haja ya kutumia penisilini au dawa nyingine yoyote ya kuua wadudu.

Penisilini ina hatari kwa watu wengine. Kabla ya kuitumia lazima ufahamu hatari zake na namna ya kuzizuia.
- Sindano za Penisilini na Streptomisini (zina majina mengine mengi)- Dawa hizi hutumika sana na mara

nyingi kwa magonjwa yasiyohusika. Dawa hizi zisitumiwe kwa mtu aliye na mafua kwa sababu haziponyeshi ugonjwa wa mafua au fluu, zinaweza kusababisha matiti makubwa wakati mwingine, kuzimia au kifo, zikizidi

kutumiwa ovyo ovyo, zitafanya magonjwa kama kifua kikuu na magonjwa mengine ya hatari yasiyoweza kuponyeka.

Vitamini B12;
Dawa hii haisaidii kutibu ukosefu wa damu au udhaifu isipokuwa kwa wagonjwa wachache tu. Inaweza kutumika tu, kama mganga ndiye karuhusu baada ya vipimo vya damu. Karibu magonjwa mengi ya damu yanatibiwa kwa kutumia vidonge vya madini ya chuma (Ferrous Sulphate).

Vitamini Nyinginezo:
Kwa kawaida, usidunge sindano za vitamini. Sindano hizo zina hatari, ni ghali na hazifanyi kazi yake vizuri kama vidonge.

Bahati mbaya, watu wengi hupoteza fedha zao kwa kununua dawa za maji ambazo zinasemekana zina vitamini. Ukweli ni kwamba nyingi kati ya dawa hizo hazina vitamini. Hata kama zingekuwa navyo ni afadhali kununua chakula kingi na kilicho bora.

Kujenga na kuhifadhi mwili kunahitaji vyakula kama mayai, nyama, matunda, mboga za majani na nafaka; ambavyo vyote vina vitamini na nguvu za kukuza mwili. Mtu mwembamba na aliyedhoofika akipewa chakula

bora mara kwa mara, kitamsaidia sana kuliko kumpa vitamini na chumvi chumvi.
Mtu anayekula vizuri hahitaji nyongeza ya vitamini.
Njia bora ya kupata vitamini.
 


Kumbuka:

Waganga na madaktari wengine, hutoa dawa wakati hazihitajiki mara kwa mara ni kwa sababu wanafikiri kuwa, wagonjwa wanatazamia kupata dawa na hawataridhika kama hawatapewa.
Ni vizuri kuwaomba daktari au mganga wako dawa wakati unapohitaji tu, la sivyo, unaweza kuharibu afya yako.

Tumia dawa ukiwa na hakika kuwa inahitajika na ukiwa na huku ikiwa na uhakika namna ya kuitumia.


Kalsium

Kuna hatari kubwa sana kumpiga mgonjwa sindano ya Kalsium kwa kutumia mshipa wa damu. Kama njia hii inatumika, ni lazima dawa inyunyizwe taratibu sana. La sivyo, itaua mara moja. Ukipiga matakoni, inaweza kusababisha jipu.
Usipige sindano ya kalsium kabla hujapata ushauri kutoka kwa mganga.

Kumbuka:

Huko Mexico na katika nchi nyingine ambako watu hutumia sana mahindi au vyakula vilivyotayarishwa na kuchanganywa na chokaa, haifai kutumia sindano, au vidonge vya kalsium (kwani mara nyingi hutolewa ili kurejesha nguvu ya mwili au kusaidia kukua kwa mtoto).
Mwili hupata kalsium inayohitajika kutokana na chokaa.

Kulisha kwa kutumia mishipa ya damu

Katika sehemu nyingine, watu walio na ukosefu wa damu au wadhaifu sana, hutumia fedha zao hadi senti ya mwisho kwa ajili ya kuwekewa dawa za maji katika mishipa yao ya damu.
Wanaamini kuwa kufanyiwa hivyo, kutawafanya wawe na nguvu za kuwa na damu safi. Lakini, wanajidanganya.

Hakuna kitu chochote katika dawa hii inayotolewa kupitia katika mshipa wa damu isipokuwa, ni maji matupu pamoja na chumvi chumvi au sukari. Haiongezi nguvu kuliko kipande kikubwa cha pipi na inafanya damu iwe nyepesi na sio nzito kama vile wanavyofikiria.

Haiponyeshi upungufu wa damu wala kumfanya mnyonge kuwa mwenye nguvu.
Na kama inatolewa na mtu asiye na ujuzi, kuna hatari ya kuingia vijidudu vibaya katika damu, na hii inaweza kumwua mgonjwa.

Dawa hii itumike tu, kwa mtu ambaye hawezi au haruhusiwi kula au ana ukosefu mkubwa wa maji mwilini.
Kama mgonjwa anaweza kumeza, mpe maji yaliyochanganywa na sukari pamoja na chumvi kiasi kipatacho painti mbili(tazama vinywaji vya kurudisha maji) - Dehydration drink, itamsaidia sana kuliko ukimpa kwa kupitisha katika mshipa wa damu.

Kwa wale ambao wanaweza kula, wanaweza kupata nguvu za kutosha kwa kula chakula bora kuliko kutumia aina yoyote ya dawa za maji zinazolishiwa kwa njia ya mishipa ya damu.
Kama mgonjwa anaweza kumeza na kuyahifadhi maji tumboni
 
Mkuu MziziMkavu unaposema,MAFUA-Vuta maji ya chumvi unamaanisha nini?sijakupata hapo,naomba unidadavulie.
 
Last edited by a moderator:
Issue ni moja, usitumie dawa bila kuonwa na daktari. Kwa sababu ya usimamizi mbovu wa nchi yetu pendwa, mtu asie stahili anjiingiza kwenye biashara ya dawa anaanzisha duka. Anapromote hgelo wake kuwa mfamasia. Na wewe unaenda kujipanga akupe prescription ya dawa ambazo kwa kuanzia haziruhusiwi kuwekwa dukani kwake.antibiotic an sindano zote ni lazma kuandikiwa na dr.
 
dawa ya kikohozi na koo kuwasha - kunywa maji ya moto kikombe kimoja au zaidi utakavyo weza asubuhi na jioni.
source mimi mwenyewe natumiaga ndani ya siku tatu kwisha habari.
 
Na ndiyo maana nakuambia kila mara wewe unafaa kuwa waziri wa afya hapa Tanzania. Si unaona sasa, wewe unaona umuhimu wa maji katika maisha ya mwanadamu ila serikali yetu mpaka na mawaziri wa afya waliopita na hawa wa sasa bado hawajajuwa umuhimu wa maji kwetu na ndio maana hawatilii mkazo wa maji huko vijijini na hata mijini pia. Utashangaa wengi wao wanakwenda Dodoma kila mara kwenye vikao vya bunge, najiuliza hivi wanakuwa hawawaoni watoto na kina mama wanaotembea kilomita na kilomita kutafuta maji safi huko njiani? Yaani hiii nchi, sijuwi maslahi ya wananchi wetu yamewekwa wapi? Yaani miaka 52 sasa, suala la maji miaka yote hii ni kitendawili, hivi ni haki kweli jamani? Karibu 2015, Mh. MziziMkavu yuko tayari kuvunja ujinga na kuleta mapinduzi ya uhakika hapa nchini. Nawahakikishia wananchi wote kuwa huyu mtu yuko tayari kufanya kazi na kutoa mfano kwa mawaziri wengine. Atakayechagua CCM ataturudisha nyuma miaka 50 mingine tena ya bila maendeleo.
 
Last edited by a moderator:
Kula vyakula ujitibie pasipo na kutumia dawa Mkuu.@King'asti Madawa ya kizungu sumu tupu yana madhara sana jihadhari nayo kuyatumia kwa wingi utadhurika.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…