Je, unaweza kuzungumza lugha ya kabila la mzazi/wazazi wako?

Je, unaweza kuzungumza lugha ya kabila la mzazi/wazazi wako?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Yaani hata kile cha kuombea maji au kusalimiana au kujitambulisha tu kwa walugha wenzio.

Haya ni matokeo ya fikra na falsafa chanya ya Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere katika kupiga vita na kutokomeza mipaka na ubaguzi wa kikabila nchini.

Kwa mafanikio na matokeo haya, nadhani nia yake hii njema, iliambatana na maombi kwa Mungu ili ifanikiwe..

Mawazo na maono ya mwalimu, yamefanya umoja, mshikamano, uhuru na amani miongoni mwa waTanzania, kua imara sana na wa uhakika mno licha ya changamoto kidogo za maoni na mitazamo tofauti ya kisiasa, ambayo ukabila hauna athari zozote ndani yake.

Na kadiri tunavyokwenda, katika muda usio kua mrefu wazaliwa wa dar kwa mfano, hawatakua wanajua hata kuongea lugha za makabila yao ispokua lugha ya Taifa na lugha nyingine za kibiashara na kimataifa pekee.

Sura na fikra za kikabila zitatoweka na kutokomea kabisa nchini.

Asanti mwenye heri, Baba wa Taifa Mwl.J.K.Nyerere🐒
 
Mimi ndio nimepotea kabisa sijui chochote kuhusu kabila langu , natamani kujua hata salamu kidogo jamani ila wapi.
 
Yaani hata kile cha kuombea maji au kusalimiana au kujitambulisha tu kwa walugha wenzio.

Haya ni matokeo ya fikra na falsafa chanya ya Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere katika kupiga vita na kutokomeza mipaka na ubaguzi wa kikabila nchini.

Kwa mafanikio na matokeo haya, nadhani nia yake hii njema, iliambatana na maombi kwa Mungu ili ifanikiwe..

Mawazo na maono ya mwalimu, yamefanya umoja, mshikamano, uhuru na amani miongoni mwa waTanzania, kua imara sana na wa uhakika mno licha ya changamoto kidogo za maoni na mitazamo tofauti ya kisiasa, ambayo ukabila hauna athari zozote ndani yake.

Na kadiri tunavyokwenda, katika muda usio kua mrefu wazaliwa wa dar kwa mfano, hawatakua wanajua hata kuongea lugha za makabila yao ispokua lugha ya Taifa na lugha nyingine za kibiashara na kimataifa pekee.

Sura na fikra za kikabila zitatoweka na kutokomea kabisa nchini.

Asanti mwenye heri, Baba wa Taifa Mwl.J.K.Nyerere🐒
ਮੂਰਖ
 
Sio kitu cha kujivunia kutokujua kuongea lugha ya wazazi wako na mila na desturi zao
 
SAITA SAYU LAWO MATLATLE! TIHHOO.KUNG` A SAITA
 
Lugha za kurogana za kazi gani,kwanza huko mbeleni hata majina ya ukoo yatapotea yatabaki ya kiswahili na ya kigeni tu. Nawapongeza wazaramo kwa kuipotezea lugha yao,wao wanabonga lugha ya Taifa tu
 
Back
Top Bottom