Je, ungeshiriki katika msafara wa kuingia "Capital One Arena"?

Je, ungeshiriki katika msafara wa kuingia "Capital One Arena"?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
5f2d192e-8961-4048-a2c7-ae9d0bb02719-PhotoJan20202592219AM.jpg
abandoned-bags.jpg
e90c7049-2511-4e83-81ea-df695e8bf89c-Ghv4pBLWAAATVGK.jpg



Moja ya masharti waliyowekewa raia wa Marekani Januari 20, 2025, kabla ya kuingia katika ukumbi wa "Capital One Arena" jijini Washington DC, ilikuwa ni kuacha mabegi na mikoba nje ili waweze kushuhudia na kusikiliza hotuba katika uapisho wa Rais Donald Trump, na wengi walikubali kutii sharti hilo.
 
Hapa tu bongo kumuona Rais Samia ni shughuli pevu, mpaka ukaribie karibu na jukwa alipo kuna vizuizi vingi vya ukaguzi mpaka inakuwa kero na udhalilishaji mtu mzima na akili zako unakaguliwa mwili mzima na maaskari/walinzi. Jukwaa lenyewe aliko Rais nalo limetengwa mbali yuko yeye na watu wake wa karibu tu. TV kubwa zimewekwa uwanjani wananchi wamuone huko. Tofauti na zamani Rais tuliweza kumuona kwa karibu na hata kumshika mkono kumsalimia tu, siku hizi hata kumuona kwenye gari lake barabarani kunako msafara wake hatumuoni akipungia mkono wananchi waliojipanga barabarani walau awapungie mkono tu. Kwanza haijulikani yupo gari gani na magari yote matatu yanafanana na yana nembo yake, meusi tii mpaka vioo na vimefungwa
 
Back
Top Bottom