Cambridge ni nzuri ila uwe vizuri mfukoni kwa sasa na kwa kipindi cha miaka 20 ijayo. Itakulazimu aende vyuo vya ulaya, marekani, canada na australia. Omba Mungu afaulu sana apate scholarship. Pia omba Mungu apate kazi ya kueleweka huko ulaya (sio kubeba mabox).
Mimi ninawazo tofauti, kama wewe ni mzazi na una mihela yako imejaa. Bora asome necta pesa inayobaki umtunzie dogo akimaliza chuo unampa pesa kama mtaji (ajira hazipo). Au mpandie miti dogo kwa sasa mpaka akija kuwa mkubwa atavuna apate pesa. Miti kama ya mbao, nguzo za umeme, maparachichi, maembe na mikorosho imsaidie mbeleni huko. Sisi wengine wazazi wanatukazania tusome ila ndo hivyo maisha yanakuwa tatizo na ajira hazipo.
Au wewe kama mzazi anzisha kampuni ndogo uiendeshe mdogomdogo ili mpaka dogo anamaliza shule anaikuta kampuni ishakuwa kubwa na anaingia moja kwa moja kwenye kampuni yako. Wewe mzazi ukifa dogo ataendeleza kampuni.
(Ni mtazamo wangu binafsi)