#COVID19 Je, Virusi vya Corona vinaweza kusambaa kupitia simu na vitasa vya milango?

#COVID19 Je, Virusi vya Corona vinaweza kusambaa kupitia simu na vitasa vya milango?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
20210305_090923_0000.png


Kwa mujibu wa taasisi ya FOPH (Kituo cha Afya cha Taifa) ya nchini Uswisi, uwezekano wa vitu hivyo kubeba maambukizi ni mkubwa endapo mtu aliyeathirika atashika kitasa cha mlango au simu huku akiwa na majimaji yaliyomtoka baada kukohoa au kupiga chafya

Endapo mtu asiye muathirika atashika vitu hivyo (vilivyoguswa na mwathirika) kisha akagusa mdomo, macho au pua yake basi atapata maambukizi ya #COVID19 kirahisi

Jambo la muhimu ambalo linasisitizwa ni kunawa mikono yako kwa sabuni na maji tiririka au utumie kitakasa mikono ili kuua #CoronaVirus

Epuka kugusa pua, mdomo na macho endapo mikono yako si misafi na salama. Na pia jitenge na wengine unapohudhuria kwenye mikusanyiko ya lazima
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom