Matojo Cosatta
JF-Expert Member
- Jul 28, 2017
- 234
- 390
JE, VITAMBULISHO VYA MACHINGA NI LAZIMA AU NI HIYARI?
Kwa tafsiri yangu ya sheria ni kuwa Vitambulisho vya Machinga ni lazima na msingi wa tafsiri yangu ni rejea za sheria zifuatazo;
(1) Kifungu cha 22 A cha Sheria ya Utawala wa Kodi, Sura ya 438 kama ambavyo imefanyiwa mabadiriko na Kifungu cha 49 cha Sheria ya Fedha, 2017 (Sheria Na. 4 ya 2017) na Kifungu cha 44 cha Sheria ya Fedha, 2019 (Sheria Na. 8 ya 2019) hususani Kifungu cha 22 A (1) na (2) Sura ya 438 kama kilivyofanyiwa mabadiriko.
(2) Kanuni ya 6 ya Kanuni za Utawala wa Kodi (Usajiri Wafanyabiashara Wadogo na Watoa Huduma Wadogo), 2020 [the Tax Administration (Registration of Small Vendors and Service Providers) Regulations, 2020] ambayo ni Tangazo la Serikali Na. 36 of 2020 hususani Kanuni ya 6 (1) na (2).
Masharti ya Kifungu cha 22 A (1) cha Sura ya 438 pamoja na Kanuni ya 5 na 6 (1) za Tangazo la Serikali Na. 36 of 2020 yanamtaka kwa lazima Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (Commissioner General of TRA) kuwatambua na kuwasajiri Wafanyabiashara Wadogo na Watoa Huduma Wadogo (wachuuzi) ambao wanafanya biashara ndogo ndogo kwenye sekta ambayo sio rasmi wakiwemo wamachinga, mama ntilie, MCs, bodaboda nakadhalika
Mfanyabiashara mdogo na mtoa huduma mdogo akiwemo machinga akisajiriwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato basi ni lazima apatiwe Kitambulisho cha Biashara Ndogo Ndogo na ni lazima alipe Tshs 20, 000/= kabla ya kupatiwa Kitambulisho na haya ni matakwa ya .
Machinga akisajiriwa na Commissioner General of TRA basi ni lazima apatiwe Kitambulisho cha Biashara Ndogo Ndogo na ni lazima alipe Tshs 20, 000/= kabla ya kupatiwa Kitambulisho, na haya ni matakwa ya masharti ya Kifungu cha 22 A (2) na (3) cha Sura ya 438 pamoja na Kanuni ya 6 (2) na (5) za Tangazo la Serikali Na. 36 of 2020.
Imeandikwa na Matojo M. Cosatta.
Kwa tafsiri yangu ya sheria ni kuwa Vitambulisho vya Machinga ni lazima na msingi wa tafsiri yangu ni rejea za sheria zifuatazo;
(1) Kifungu cha 22 A cha Sheria ya Utawala wa Kodi, Sura ya 438 kama ambavyo imefanyiwa mabadiriko na Kifungu cha 49 cha Sheria ya Fedha, 2017 (Sheria Na. 4 ya 2017) na Kifungu cha 44 cha Sheria ya Fedha, 2019 (Sheria Na. 8 ya 2019) hususani Kifungu cha 22 A (1) na (2) Sura ya 438 kama kilivyofanyiwa mabadiriko.
(2) Kanuni ya 6 ya Kanuni za Utawala wa Kodi (Usajiri Wafanyabiashara Wadogo na Watoa Huduma Wadogo), 2020 [the Tax Administration (Registration of Small Vendors and Service Providers) Regulations, 2020] ambayo ni Tangazo la Serikali Na. 36 of 2020 hususani Kanuni ya 6 (1) na (2).
Masharti ya Kifungu cha 22 A (1) cha Sura ya 438 pamoja na Kanuni ya 5 na 6 (1) za Tangazo la Serikali Na. 36 of 2020 yanamtaka kwa lazima Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (Commissioner General of TRA) kuwatambua na kuwasajiri Wafanyabiashara Wadogo na Watoa Huduma Wadogo (wachuuzi) ambao wanafanya biashara ndogo ndogo kwenye sekta ambayo sio rasmi wakiwemo wamachinga, mama ntilie, MCs, bodaboda nakadhalika
Mfanyabiashara mdogo na mtoa huduma mdogo akiwemo machinga akisajiriwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato basi ni lazima apatiwe Kitambulisho cha Biashara Ndogo Ndogo na ni lazima alipe Tshs 20, 000/= kabla ya kupatiwa Kitambulisho na haya ni matakwa ya .
Machinga akisajiriwa na Commissioner General of TRA basi ni lazima apatiwe Kitambulisho cha Biashara Ndogo Ndogo na ni lazima alipe Tshs 20, 000/= kabla ya kupatiwa Kitambulisho, na haya ni matakwa ya masharti ya Kifungu cha 22 A (2) na (3) cha Sura ya 438 pamoja na Kanuni ya 6 (2) na (5) za Tangazo la Serikali Na. 36 of 2020.
Imeandikwa na Matojo M. Cosatta.