JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Je, Wajua unyonyeshaji ukifanyika ipasavyo, uwezekano wa Mtoto kupata Magonjwa hatari ya kuambukizwa au kuugua mara kwa mara hupungua na hivyo kupunguza Vifo vya Watoto?
Hata hivyo, tafiti mbalimbali zinaonesha baadhi ya Wanawake wanaonyonyesha wakiwa katika ajira wamekuwa wakishindwa kunyonyesha kila inapohitajika kutokana na kubanwa na Mazingira, ratiba au majukumu yao.
Kufahamu zaidi kuhusu Haki za Akina Mama Wanaonyonyesha wakiwa katika Ajira na Wajibu wa Waajiri, Shiriki katika Mjadala na Wataalamu wa Masuala ya Uzazi na Sheria, Agosti 7, 2024 kuanzia Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2 Usiku kupitia XSpaces ya JamiiForums
Kushiriki Mjadala x.com
=======
Mjadala umeanza ambapo afisa programu wa Jamiiforums, David Magobeko alikaribisha waliojiunga na kuwatambulisha wachangiaji na Dkt. Mariam Nooran anaanza.
Dkt. Mariam Noorani (Daktari wa Watoto/Mtaalamu wa Unyonyeshaji - Aga Khan Hospitali): Tunapoongelea faida za Unyonyeshaji tunaongelea faida kwa jamii, kwa Mama, Mtoto na Kwa Nchi
Lakini nataka kuongelea faida za Unyonyeshaji kwa Mtoto
Unyonyeshaji wa Watoto hasa kwa Miezi 6 ya mwanzo una faida nyingi kwa mtoto
Kubwa zaidi ni kusaidia ukuaji wake na kumlinda dhidi ya Magonjwa kama Pumu na Magonjwa ya Ngozi
Mercy-Grace Seuya: Mwakilishi Chama cha Waajiri Tanzania (ATE): Waajiri wana nafasi kubwa sana katika malezi ya mtoto kabla hata hajazaliwa
Na ni wajibu wao kufuata Sheria zinazowaruhusu Wazazi kupata muda wa kunyonyesha Watoto
Mwajiri ana uwezo wa kutunga sera rafiki zitakazo mwezesha Mama kuweza kunyonyesha Vizuri
Mfano; kuna Ofisi ambazo zimetenga Maeneo maalum ya faragha ili kunyonyesha au kumwezesha Mama kukamua Maziwa kwa ajili ya Mtoto
Mary Yunge (Mwakilishi TUGHE): Lazima tufahamu kuwa kuna Sheria zinatuongoza Kazi
Mfanyakazi anapokosa likizo ya kunyonyesha anaweza kutoa Malalamiko katika Chama cha Wafanyakazi kilichopo katika eneo lake la kazi
Kwasababu moja ya sababu za kuanzishwa kwa Vyama vya Wafanyakazi ni kuhakikisha mazingira bora ya kazi.
Ni vizuri kuwa na Maxingira mazuri ya ushirikishwaji kati ya Waajiri na Wafanyakazi wa namna gani Wafanyakazi wanaonyonyesha waweze kupata nafasi
Kwasababu Mfanyakazi anayeyonyesha asipokutana na changamoto, utendaji kazi wake unakuwa hauathiriki hivyo ni faida kwa Kampuni.
Muhimu zaidi ni Elimu
Elimu iendelee kutolewa kwa Wafanyakazi waweze kuzifahamu haki zao zikiwemo za kunyonyesha
Pia Elimu itolewe ili Waaajiri na Wafanyakazi waweze kukaa pamoja na kupanga namna bora zaidi ya kurahisisha Mchakato wa Unyonyeshaji kwa Waajiriwa Wanaonyonyesha.
Kwa Mtumishi anayekuwa ameshindwa kunyonyesha vizuri kutokana na kazi yake na ana malalamiko anaweza kuwasilisha Malalamiko yake kwa Kamishna wa Kazi pia Kamati ya Usuluhishi (CMA)
Huko Sheria itatumika ambapo Shauri lake litashughulikiwa pasipo kuathiri ajira ya Mlalamikaji.
Dkt. Haika Malik (Mwakilishi Chama cha Madaktari wa Watoto Tanzania): Waajiri wanasema bado hawajaona Waraka wa Mabadiliko ya Sheria mfano; Likizo ya Mama aliyejifungua Mtoto Njiti
Kwa hiyo ni jukumu letu Wadau kutoa elimu ili kuhakikisha Mama anapata na anatumia haki yake ya kunyonyesha.
Mary Yunge: Chama chetu cha Wafanyakazi (TUGHE) huwa tunapokea Maoni na Ushauri kutoka kwa Wafanyakazi kuhusu unyinyeshaji
Kwa mfano suala la likizo ya Mama aliyejifungua Mtoto njiti, ni suala ambalo tumelipokea kwa muda mrefu
Sasa Mama akijifungua Mtoto njiti analazimika kukaa Hospitali muda mrefu, na hadi akitoka unakuta zile siku 84 zimeisha
Lakini Mei Mosi hili suala lilipata Ufumbuzi
Elimu itolewe kwa Waajiri kuhusu haki na Umuhimu wa Waajiriwa Kunyonyesha
Lakini pia Waajiriwa wapewe elimu ya haki zao za Kunyonyesha
Wakizijua haki zao ni rahisi kutambua zikivunjwa
Mercy-Grace Seuya: Sisi kama Chama cha Waajiri tunafanya kazi kubwa katika Kutoa Elimu kwa Waajiri na Waajiriwa
Pia katika Kila Ofisi ni muhimu kuwa na Sera ya Rasilimali watu. Na ni takwa la kisheria
Sera hii inatoa Mwongozo wa haki na wajibu wa Mwajiri na mwajiriwa. Inaeleza huyu asipofanya nini afanye nini.
Mwakilishi Chama cha Waajiri Tanzania (ATE): Tamko kutoka kwa Makamu wa Rais kuhusu likizo ya Mama anayejifungua Mtoto njiti bado ni tamko, bado halijawa sheria
Ni kweli ni tamko kubwa lakini linatoa gurudumu la utunzi wa Sheria kuhusiana na hilo.
Dkt. Haika Malik: Mama na Mtoto njiti huwa wanakuwa wanakaa Hospitali kwa muda mrefu zaidi kwa sababu wanahitaji uangalizi na ufuatiliaji wa karibu zaidi
Na wakiweza kunyonyeshwa vizuri tafiti zimeonesha inaweza kupunguza muda wa kukaa hospitali
Changamoto kubwa katika Hospitali za Umma hazina nafasi ya kumruhusu Mama kulala na Mwanae aliye njiti
Mama analazimika kutembea kutoka Wodi moja kwenda kwenye wodi ya Mtoto ili kumyonyesha
Hiyo inasababisha mama anakuwa hapumziki. Unakuta usiku kucha anaamka kutembea kwenda kunyonyesha.
Katika Hospitali nyingine wamewasaidia Wakina Mama kwa kuweka Friji Wodini
Yaani Mama anakuwa anakamua Maziwa yanahifadhiwa kwenye friji na mtoto akihitaji anapelekewa , japokuwa hii inategemea na ukubwa wa Mtoto
Njia hii inamsaidia Mama kupumzika kidogo, kutembea tembea kuna pungua.
Idda Katigula (Mtaalam wa Lishe na Mwanzilishi wa Shirika la Unyonyeshaji la JJ): Wakina mama wengi ambao wamejiajiri au wameajiriwa wamekutana na changamoto mbalimbali
Moja ni ukosefu wa elimu ya Ukamuaji wa Maziwa, hii inaenda hadi kwa Wenza na watu wanaomzunguka.
Unakuta Mama amekamua Maziwa kwa mujibu wa Maelekezo ya Wataalamu wa Afya lakini watu wanaomzunguka hawayaamini
Yaani unakuta Wifi, au Mama Mkwe haamini Maziwa yalikamuliwa na wanaona hayana umuhimu au virutubisho. Jambo ambalo sio la kweli.
Hata hivyo, tafiti mbalimbali zinaonesha baadhi ya Wanawake wanaonyonyesha wakiwa katika ajira wamekuwa wakishindwa kunyonyesha kila inapohitajika kutokana na kubanwa na Mazingira, ratiba au majukumu yao.
Kufahamu zaidi kuhusu Haki za Akina Mama Wanaonyonyesha wakiwa katika Ajira na Wajibu wa Waajiri, Shiriki katika Mjadala na Wataalamu wa Masuala ya Uzazi na Sheria, Agosti 7, 2024 kuanzia Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2 Usiku kupitia XSpaces ya JamiiForums
Kushiriki Mjadala x.com
=======
Mjadala umeanza ambapo afisa programu wa Jamiiforums, David Magobeko alikaribisha waliojiunga na kuwatambulisha wachangiaji na Dkt. Mariam Nooran anaanza.
Dkt. Mariam Noorani (Daktari wa Watoto/Mtaalamu wa Unyonyeshaji - Aga Khan Hospitali): Tunapoongelea faida za Unyonyeshaji tunaongelea faida kwa jamii, kwa Mama, Mtoto na Kwa Nchi
Lakini nataka kuongelea faida za Unyonyeshaji kwa Mtoto
Unyonyeshaji wa Watoto hasa kwa Miezi 6 ya mwanzo una faida nyingi kwa mtoto
Kubwa zaidi ni kusaidia ukuaji wake na kumlinda dhidi ya Magonjwa kama Pumu na Magonjwa ya Ngozi
Mercy-Grace Seuya: Mwakilishi Chama cha Waajiri Tanzania (ATE): Waajiri wana nafasi kubwa sana katika malezi ya mtoto kabla hata hajazaliwa
Na ni wajibu wao kufuata Sheria zinazowaruhusu Wazazi kupata muda wa kunyonyesha Watoto
Mwajiri ana uwezo wa kutunga sera rafiki zitakazo mwezesha Mama kuweza kunyonyesha Vizuri
Mfano; kuna Ofisi ambazo zimetenga Maeneo maalum ya faragha ili kunyonyesha au kumwezesha Mama kukamua Maziwa kwa ajili ya Mtoto
Mary Yunge (Mwakilishi TUGHE): Lazima tufahamu kuwa kuna Sheria zinatuongoza Kazi
Mfanyakazi anapokosa likizo ya kunyonyesha anaweza kutoa Malalamiko katika Chama cha Wafanyakazi kilichopo katika eneo lake la kazi
Kwasababu moja ya sababu za kuanzishwa kwa Vyama vya Wafanyakazi ni kuhakikisha mazingira bora ya kazi.
Ni vizuri kuwa na Maxingira mazuri ya ushirikishwaji kati ya Waajiri na Wafanyakazi wa namna gani Wafanyakazi wanaonyonyesha waweze kupata nafasi
Kwasababu Mfanyakazi anayeyonyesha asipokutana na changamoto, utendaji kazi wake unakuwa hauathiriki hivyo ni faida kwa Kampuni.
Muhimu zaidi ni Elimu
Elimu iendelee kutolewa kwa Wafanyakazi waweze kuzifahamu haki zao zikiwemo za kunyonyesha
Pia Elimu itolewe ili Waaajiri na Wafanyakazi waweze kukaa pamoja na kupanga namna bora zaidi ya kurahisisha Mchakato wa Unyonyeshaji kwa Waajiriwa Wanaonyonyesha.
Kwa Mtumishi anayekuwa ameshindwa kunyonyesha vizuri kutokana na kazi yake na ana malalamiko anaweza kuwasilisha Malalamiko yake kwa Kamishna wa Kazi pia Kamati ya Usuluhishi (CMA)
Huko Sheria itatumika ambapo Shauri lake litashughulikiwa pasipo kuathiri ajira ya Mlalamikaji.
Dkt. Haika Malik (Mwakilishi Chama cha Madaktari wa Watoto Tanzania): Waajiri wanasema bado hawajaona Waraka wa Mabadiliko ya Sheria mfano; Likizo ya Mama aliyejifungua Mtoto Njiti
Kwa hiyo ni jukumu letu Wadau kutoa elimu ili kuhakikisha Mama anapata na anatumia haki yake ya kunyonyesha.
Mary Yunge: Chama chetu cha Wafanyakazi (TUGHE) huwa tunapokea Maoni na Ushauri kutoka kwa Wafanyakazi kuhusu unyinyeshaji
Kwa mfano suala la likizo ya Mama aliyejifungua Mtoto njiti, ni suala ambalo tumelipokea kwa muda mrefu
Sasa Mama akijifungua Mtoto njiti analazimika kukaa Hospitali muda mrefu, na hadi akitoka unakuta zile siku 84 zimeisha
Lakini Mei Mosi hili suala lilipata Ufumbuzi
Elimu itolewe kwa Waajiri kuhusu haki na Umuhimu wa Waajiriwa Kunyonyesha
Lakini pia Waajiriwa wapewe elimu ya haki zao za Kunyonyesha
Wakizijua haki zao ni rahisi kutambua zikivunjwa
Mercy-Grace Seuya: Sisi kama Chama cha Waajiri tunafanya kazi kubwa katika Kutoa Elimu kwa Waajiri na Waajiriwa
Pia katika Kila Ofisi ni muhimu kuwa na Sera ya Rasilimali watu. Na ni takwa la kisheria
Sera hii inatoa Mwongozo wa haki na wajibu wa Mwajiri na mwajiriwa. Inaeleza huyu asipofanya nini afanye nini.
Mwakilishi Chama cha Waajiri Tanzania (ATE): Tamko kutoka kwa Makamu wa Rais kuhusu likizo ya Mama anayejifungua Mtoto njiti bado ni tamko, bado halijawa sheria
Ni kweli ni tamko kubwa lakini linatoa gurudumu la utunzi wa Sheria kuhusiana na hilo.
Dkt. Haika Malik: Mama na Mtoto njiti huwa wanakuwa wanakaa Hospitali kwa muda mrefu zaidi kwa sababu wanahitaji uangalizi na ufuatiliaji wa karibu zaidi
Na wakiweza kunyonyeshwa vizuri tafiti zimeonesha inaweza kupunguza muda wa kukaa hospitali
Changamoto kubwa katika Hospitali za Umma hazina nafasi ya kumruhusu Mama kulala na Mwanae aliye njiti
Mama analazimika kutembea kutoka Wodi moja kwenda kwenye wodi ya Mtoto ili kumyonyesha
Hiyo inasababisha mama anakuwa hapumziki. Unakuta usiku kucha anaamka kutembea kwenda kunyonyesha.
Katika Hospitali nyingine wamewasaidia Wakina Mama kwa kuweka Friji Wodini
Yaani Mama anakuwa anakamua Maziwa yanahifadhiwa kwenye friji na mtoto akihitaji anapelekewa , japokuwa hii inategemea na ukubwa wa Mtoto
Njia hii inamsaidia Mama kupumzika kidogo, kutembea tembea kuna pungua.
Idda Katigula (Mtaalam wa Lishe na Mwanzilishi wa Shirika la Unyonyeshaji la JJ): Wakina mama wengi ambao wamejiajiri au wameajiriwa wamekutana na changamoto mbalimbali
Moja ni ukosefu wa elimu ya Ukamuaji wa Maziwa, hii inaenda hadi kwa Wenza na watu wanaomzunguka.
Unakuta Mama amekamua Maziwa kwa mujibu wa Maelekezo ya Wataalamu wa Afya lakini watu wanaomzunguka hawayaamini
Yaani unakuta Wifi, au Mama Mkwe haamini Maziwa yalikamuliwa na wanaona hayana umuhimu au virutubisho. Jambo ambalo sio la kweli.