Je, wahindi ama kihindi ni hoja ya makabila Tanzania?

Je, wahindi ama kihindi ni hoja ya makabila Tanzania?

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Wakuu nimevutiwa na mijadala mikubwa huko Duniani inayohusu ukabila, uraia, u bara na urangi hasa iliyoanza huko Afrika kusini ambapo watu wanavutana je wazungu ama watu weupe wa Afrika kusini ni waafrika ama sio waafrika.

Na je uafrika ni rangi ama ni ubara bila kujali rangi yako. Je kama ni ubara, kwa nini weusi wa Marekani waitwe African American na sio American tu, kwa nini wazungu wa Marekani wasiitwe European American kama vile Watu weusi kwani wote ni wazamiaji Amerika.

Je, kama ni ubara, mbona Waarabu wa kaskazini ya Afrika hua hawataki kuitwa Waafrika na wanatamani kabisa wasiitwe waafrika, je uafrika ni rangi ama ni bara?

Je, wachina wanaozaliwa Afrika wanaweza kuitwa Chinese Afrikan ama African tu? Je weusi wanaozaliwa china ama Japan ama Asia wanaweza kuitwa African Chinese ama Chinese pekee, African Japanese ama Japanese pekee, Korean nk?

Mwaka 2017 Wahindi walitambuliwa na serikali ya Kenya kama kabila rasmi la Kenya, Je kwa Tanzania wahindi wanajitambulisha kama wahindi ama Watanzania ama Wahindi?

Soma huu mjadala.


View: https://x.com/elonmusk/status/1892155910182629383?s=19
 
Back
Top Bottom