Je wajua jimbo la Texas lilichukuliwa kimabavu na wakolooni wakimarekani kutoka Mexico??

Je wajua jimbo la Texas lilichukuliwa kimabavu na wakolooni wakimarekani kutoka Mexico??

Madrid boy

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2017
Posts
895
Reaction score
615
Habar zenu wakuu nimatumaini yangu hamjambo.Inavyofahamika sasa jimbo la Texas lipo marekani hili jimbo ni moja ya majimbo yanayopatikana kusini mwa nchi ya Marekani limepakana na nchi ya Mexico.Hili moja ya majimbo yaleyale ya kusini yaliyokua yakitaka kuendelea kwa utumwa hata baada ya Marekani kupata uhuru chini ya Generali wao aliyejulikana kwa jina la Generali Robert E. Lee.

Mnamo October 2 1835 kabla ya vita ya Marekani (American civil war )hawa watu wanaliokua wanaishi Texas walikua wanafahamika kama wakoĺooni wa kimarekani waliokua wanakaa Texas kimabavu waliamua kushirikiana na baadhi ya Wamexico wazaliwa wa Texas waliojulikana kama (Tejanos) kuupinga utawala wa Rais Antonio Lopez de Santa Anna.Serikali ya Mexico wakati huo ilishajua ulikua ni mpango wa Marekani kujitanua kieneo kama ilivyo waasi katika mji wa Donenstky kule Ukraine mashariki ambao wanataka kujitenga kutoka serikali ya Kiev na kuwa ni jamuhuri yenye mafungamano na Urusi.



Basi serikali ya Mexico ya wakati huo ikasema itaingia vitani juu ya Mzozo wa eneo hilo Mnamo October 2 1835 vita vikaanza kati ya Mexico na Texas mpaka mwaka 1836 ambapo Mexico walishindwa katika hii vita baada ya huu ushindi Texas ikawa ni jamuhuri inayojitegemea kama ilivyo jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.Ikumbukwe wakati huu Texas haikuwa sehemu ya Marekani hata kidogo.

Rais wa Marekani wakati huo Martin Van Buren alijizuia kuinganisha Texas mapema iwe ni sehemu ya Marekani. Kwa hiyo Marekani ikawa na uhusiano wa kidiplomasia na Jamuhuri ya Texas kama taifa huru .
0a2cd9fc4f99f7e9a52893457e36d8e6.jpg

Rais Martin Van Buren

Mnamo mwaka 1845 rais wamarekani aliyeitwa John Tyler alianza mazungumzo ya kidiplomasia na Jamuhuri ya Texas kuinganisha iwe ni sehemu ya Marekani.Mnamo mwaka 1844 ndipo mazungumzo ya kuinganisha Texas iwe sehemu ya Marekani yalianza Mnamo mwaka 1845 chini ya Rais James k. Polk mkataba wa kuiongeza Texas iwe sehemu ya Marekani uliwekwa.

I ngawa Rais Tyler alikosa kura kutoka seneti kuhalalisha mkataba huo lakini baada ya kustaafu alijitahidi sana kuhakikisha Jamuhuri ya Texas inakua ni sehemu ya Marekani .Kwa upande Wamexico walikua hawataki kutambua kama Texas inakua tena ni sehemu ya Marekani

0df6c4fb5c612cb455b1c3201a215c46.jpg

Rais John Tyler
NB:Nitaendelea wakuu maana ni ishu ndefu kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ahsante kwa historia hii maridhawa mkuu,nasubiri muendelezo
 
Nakusubiri urudi mapema, hili jimbo maarufu kwa wafugaji wa ng'ombe na kilimo cha mahindi na maharage (cowboy asili ya chuck noris mcheza sinema.
 
Nakusubiri urudi mapema, hili jimbo maarufu kwa wafugaji wa ng'ombe na kilimo cha mahindi na maharage (cowboy asili ya chuck noris mcheza sinema.
 
Baada ya "mapindizi ya marekani" kuisha kwa mkataba wa paris mwaka 1783, ufalme wa uingereza ulikubali kuyaachia makoloni ( majimbo) 13 yaliyo unda taifa jipya(USA). Katika kipindi cha miaka 134 marekani iliendelea kujiongezea eneo lake kwa kununua maeneo, kuingia mikataba ya muungano na maeneo mengine na kushinda vita mbali mbali. Eneo ililonalo leo (achia mbali visiwa) lilifikiwa mwaka 1917.
Baadhi ya maeneo yaliyonunuliwa ni Luisiana kutoka utawala wa ufaransa mwaka 1803 kwa dola 15 milioni za wakati huo na alaska kutoka urusi mwaka 1867 kwa dola 7.2 million za wakati huo.
Majimbo yaliyojiunga na US kwa hiyari ( mikataba ) ni pamoja na Hawaii mwaka 1959.
Sehemu kubwa ilipatikana kwa uvamizi na kushinda vita, mexico na yaliyokua makoloni ya spain ndio waliopoteza maeneo mengi zaidi, baada ya kuyatwaa maeneo hayo marekani ilikua inalipa fedha kiasi na kuhakikisha wana sainiana makubaliano na nchi walizozinyang'anya maeneo ili kujilinda kisheria. Japo kua baadh ya maeneo hayo waliyaachia baadae (mfano cuba na phillipines). Maeneo kama texas, new mexico, sehemu ya arizona na maeneo mengi yaliporwa kutoka mexico.
Kwa kifupi marekani imejengwa kwa damu na jasho la native americans na black slaves, it is a barbaric country.
 
Leo ndio taifa kubwa linalojinasibisha na demokrasia,uhuru na haki za binadamu. Kweli hata majambazi sadaka zao hupokelewa na Mola. Historia nzuri sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habar zenu wakuu nimatumaini yangu hamjambo.Inavyofahamika sasa jimbo la Texas lipo marekani hili jimbo ni moja ya majimbo yanayopatikana kusini mwa nchi ya Marekani limepakana na nchi ya Mexico.Hili moja ya majimbo yaleyale ya kusini yaliyokua yakitaka kuendelea kwa utumwa hata baada ya Marekani kupata uhuru chini ya Generali wao aliyejulikana kwa jina la Generali Robert E. Lee.

Mnamo October 2 1835 kabla ya vita ya Marekani (American civil war )hawa watu wanaliokua wanaishi Texas walikua wanafahamika kama wakoĺooni wa kimarekani waliokua wanakaa Texas kimabavu waliamua kushirikiana na baadhi ya Wamexico wazaliwa wa Texas waliojulikana kama (Tejanos) kuupinga utawala wa Rais Antonio Lopez de Santa Anna....

Historia yako ina mapengo kidogo, hasa ni Meksiko yenyewe iliyokaribisha walowezi kutoka Marekani waje kwao kwa sababu wenyeji hawakuwa Wameksiko (yaani wasemaji wa kihispania) bali Maindio wazalendo ambao hawakutaka hao pia. Basi ona hitimisho hii:

Koloni ya Hispania
Kabla ya kufika ya Wahispania maeneo ya Texas yalikaliwa na makabila mbalimbali ya Waindio. Tangu uvamizi wa Mexiko kulikuwa na misafara kadhaa ya Wahispania kwenye pwani la Texas lakini hawakukaa. Baada ya Ufaransa kuanzisha koloni ya Lousiana katika eneo la New Orleans Hispania iliogopa uenezaji wa Wafaransa wakapeleka mapadre Mexiko waliojenga misioni kadhaa huko na mwaka 1718 mji wa San Antonio ilianzishwa. Lakini idadi ya walowezi Wahispania ilikuwa ndogo kutokana na upinzani mkali wa Waindio wenyeji.

Jimbo la Mexiko na uhuru
Baada ya uhuru wa Mexiko kutoka Hispania mwaka 1821 Texas ilikuwa jimbo la nchi mpya ya Mexiko. Ilhali serikali ya Mexiko ilikosa uwezo wa kuwashinda Waindio ilikaribisha walowezi kutoka maeneo ya Marekani kuja Texas. Kuingia kwa walowezi wengi wenye lugha na utamaduni wa Kiingereza kutoka Marekani kulisababisha kutokea kwa tofauti ya kiutamaduni na na sehemu ya wakazi wapya hawakukubali mamlaka ya serikali ya Mexiko. Hatimaye mwaka 1836 walowezi Wamarekani katika jimbo walitangaza Jamhuri ya Texas kuwa nchi huru ya kujitegemea ilivumiliwa na Mexiko baada ya vita fupi lakini Mexiko iliendelea kudai mamlaka juu yake.

Utekaji na Marekani
Nchi hii mpya ilikuwa dhaifu na wakazi wengi waliogopa kuvamiwa upya na Mexiko. Kwa hiyo viongozi waliomba kuwa sehemu ya Marekani. Ilhali Texas ilikuwa na sheria ya utumwa, na ndani ya Marekani majimbo ya kukubali na kukataa utumwa yalivutana kwa miaka kadhaa hapakuwa na azimio kuhusu ombi la Texas. Maana majimbo yaliyopinga utumwa hayakutaka kukubali maeneo mapya penye utumwa ndani ya Marekani. Lakini mwaka 1846 raisi mpya James K. Polk alitangaza utekaji wa Texas na Marekani na Texas ilikuwa jimbo la 28 katika Maungano ya Madola ya Amerika. Hatua hii ilisababisha vita ya Marekani na Mexiko iliyokwisha baada ya miaka miwili kwa ushindi wa Marekani mwaka 1848.

Sasa walowezi wapya walihamia Texas. Mashamba makubwa yalianzishwa yaliyolimwa na watumwa weusi walioongezeka hadi theluthi moja ya wakazi wote walikuwa watumwa mnamo 1860.

Chanzo: Texas - Wikipedia, kamusi elezo huru
 
Back
Top Bottom