Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!

Tena Kuna uwezekano Dr.Tulia akwa Spika wa hovyo zaidi ya Maspika wa wote kuwahi kuongoza Bunge la jamuhuri ya Muungano wa Tanzania..hamfikii hata Job licha ya kufanya Maamuzi ya hovyo kulinda chama chake [emoji848]
 
Msikilizeni hapa Spika wetu Dr. Tulia
I was dam right about this lady!.
Nilisema Dr. Tulia akitulia she can make the best Spika!. That video clip is the proof, she is the best!.

Tena nadhani huyu mwanamke aliyezungumzwa hapa for 2030, could be Dr. Tulia!. Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke
Hongera sana Spika Dr. Tulia, umeonyesha uwezo to be the best,
God bless you.
God bless Tanzania.

P
 
Mayalla umezeekaaa sana MUNGU atakulaani
 

Attachments

  • tweeload_0920e46b.mp4
    3.5 MB
Tena Kuna uwezekano Dr.Tulia akwa Spika wa hovyo zaidi ya Maspika wa wote kuwahi kuongoza Bunge la jamuhuri ya Muungano wa Tanzania..hamfikii hata Job licha ya kufanya Maamuzi ya hovyo kulinda chama chake [emoji848]
Yaani wa hovyoooo
 

Attachments

  • 20221002_220507.jpg
    50.1 KB · Views: 4
Spika Tulia kaiva sana kwenye suala kutafiri Sheria, naangalia hapa Bunge live wanapitisha muswada wa tume ya uchaguzi naona anamtoa knout mpaka AG huyu dada ni balaa wabunge wote wanampigia makofi.

Mbeya tunasema Tulia mitano tena.
Naunga mkono hoja Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria?

Tena sio Tulia mitano tena bali 2025 could be ni Dr. Tulia!.
Angalia tulikotoka nae
1. Hivyo japo ni mimi niliyemtabiria Dr. Tulia uspika, Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...

2. Fursa ya Spika mpya ilipojitokeza, niliwaomba CCM Kujiuzulu kwa Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili tupate Spika Bora. CCM itateua Spika Bora au Bora Spika kama kawa?

3. Hivyo Dr Tulia aliposhinda nikamshauri Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!

4. Kwa vile Rais Samia amesisitiza 2025 twende na Mwanamke Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! wengi wanadhani Mwanamke wa 2025 ni lazima awe Rais Samia, anaweza kuwa ni Dr. Tulia!.
5. Sababu ya kwanini 2025 anaweza kuwa ni Dr. Tulia ni HII

P
 
Unaonaje Paul Makonda??
 
Unaonaje Paul Makonda??
Huyu ni jembe Pongezi Paul Makonda kuifufua CCM kwa amsha amsha. Twende mdogomdogo ngoma ikivuma sana inakaribia kupasuka!
Na Nikimwangalia Makonda, mambo anayoyafanya namuona kama Magufuli na Bado kuna ubishi kuwa hiki ni chuma? Je, chuma hiki ni chuma kingine ila ni kama kile au chuma hiki ni kile kile kimerejea kivingine?

kwasababu hakuna mkamilifu, ila human beings are not static, they are dynamics and hence, they change with time. Kwa mapito aliyoyapitia amejifunza humility, he will be the best of the best!.

Ili kumjua vizuri, anzia hapa Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Kisha Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam

Akawa RC wa DSM na akafanya makubwa ikiwa ni pamoja na kupitishwa kwenye tanuri la moto kupikwa akaiva kisawasawa

Kwa wale mnaopenda kujua mapito aliyo yapita karibuni pande hizi
Najua kuna watu bado hawaamini hili linawezekana, naomba kuwathibitishia, lisilo wezekana kwa binadamu, kwa Mungu linawezekana!.
P
 
Mkuu, analysis kama hii ndiyo inawafanya watu wakuweke kundi moja na machawa mazagazaga. Tulia kwa taaluma yake siyo mtu wa kushindwa kutofautisha wajibu na kazi ya mihimili mikuu mitatu ya dola. Wote tunajuwa kauli yake tata mbele ya Rais, sitaingia kwa undani.

Ni mtu mbinafsi ambae anatafuta na kutumia frusa kwa ajili ya maslahi yake binafsi. Ameamua kuwasaliti wananchi na kujiegemeza kwa watawala kwa jinsi anavyoliendeasha bunge na maamuzi yake kipindi chote kuanzia alipokuwa naibu spika. Hapana shaka kabisa ktk elimu wala uelewa wake.

Watu wa nature ya Tulia ubadilika kutokana na frusa. Usitegemee hata siku moja atakuja kusimama kwa maslahi ya taifa zaidi ya maslahi binafsi. Mifano ni mingi, lakini chukulia mmoja tu, mkataba wa bandari na DPW. Yeye kama mwanasheria msomi ni kipi alichokuwa hakijui hadi kufikia yale maamzi?
 
Sasa Pascal unaenda mbali. Unataka kutuaminisha kurudishwa kwa Makonda na kateuliwa kuwa Mwenezi, Mungu kahusika? Kwa maana nyingine Samia ni Mungu. Hachana na siasa za kiwango hicho. Hitler aliyeuwa makumi elfu ya watu kule Ujerumani chama chake cha NAZI kilichaguliwa na wananchi. Je, Mungu pia alihusika?
 
Yes ni Mungu ndiye huziweka serikali za mataifa, hata Firauni aliwekwa na Mungu, hata Iddi Amini aliwekwa na Mungu!. JPM aliwekwa na Mungu, akatwaliwa na Mungu, Samia pia kaletwa na Mungu!. Samia ni mpango wa Mungu kwa Tanzania: Kwa hili atabarikiwa, Taifa litabarikiwa. Asante Mungu kwa Samia, Mungu mbariki Samia, Mungu ibariki Tanzania!
P
 
Mayala,Tulia alinifurahisha alipouliza maana za trat na trap na jibu alilopewa,ndiyo ujue uozo uliopo mbele
 
Humjui MUNGU wewe,Daud alipowahesabu waIsrael MUNGU alishusha tauni maelfu wakafa,endelea kujifunza.
 
Hili la kuwakemea Mabeberu huku unawaangalia usoni hata Mwanasiasa Maarufu mh Tundu Lisu haliwezi...
Naunga mkono hoja, niliwahi kusema humu, Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana! Kisha nikasema Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria?

Kwa vile tumepania Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! kuna uwezekano huyo mwanamke wa 2025 sio Sa100 ni Tulia.

Ila mimi kwenye hesabu zangu, Dr. Tulia nilimpangia 2030-2040 kama ninavyoeleza hapa kwenye HII kitu.

Sauti inasema sasa ni Dr. Tulia!. Ameonyesha uwezo

P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…