Je, wakati umefika tuikubali Bodi ya Kitaaluma ya Walimu?

Je, wakati umefika tuikubali Bodi ya Kitaaluma ya Walimu?

balimar

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2015
Posts
7,743
Reaction score
13,657
Wadau habari,

Napenda ifikie wakati tufungua mjadala mpana wa uwepo au kutakuwepo kwa Bodi ya Kitaalamu ya Walimu Tanzania (Tanzania Teachers' Professional Board) TTPB.

Tumekuwa na sintofahamu kadhaa hasa kwa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kuona TTPB itaongeza utitiri wa vyombo vinavyomsimamia mwalimu achilia mbali tozo za ada ya kila mwaka ambayo italipwa moja kwa moja na mwalimu na ada za leseni na kuona kama Teachers' Service Commission (TSC) inatosha kabisa kufanya na kuendelea na majukumu hayo.

Ni ukweli usiopingika kuwa KUTOKUWA na bodi maalumu ya kusimamia Professional ya Ualimu imekuwa ni sababu ya kutoheshimika kwa taaluma hii ukilinganisha na taaluma zingine kama za udaktari, uhasibu, sheria n.k. Ukiangalia kwa umakini nchi zinazoheshimu taaluma ya ualimu wanazo bodi za Kitaalumu za Walimu ambazo kazi yake kubwa ni kuweka Viwango na kusimamia na Kuishauri Serikali au mwajiri yeyote wa taaluma hii kuhusu taaluma na weredi husika.

Huu ushauri wa kitaalamu unaoletwa na bodi ndio unamsaidia muajiri kujua nini afanye na nini asifanye kwa mwajiliwa mwenye taaluma husika.

Mapungufu makubwa kwenye taaluma ya Ualimu kwa sasa ni kukosekana kwa viwango (standards) za taaluma hasa kwenye mishahara, uzoefu na elimu za walimu. Tofauti ni kubwa sana. Walimu tunatofautina hata mkiajiriwa na kwa level ya DEGREE tu, ukija shuleni mshahara ni tofauti na ukienda vyuo vya kati na tofauti ni kubwa zaidi ukienda kama tutorial assistant kwenye Elimu ya Juu. Lakini kibaya zaidi ukijiendeleza ndio kama umejichongea utasikia wewe ni kama umejifurahisha tu yaani Masters degree ya Ualimu na ukipata PhD unaambiwa wewe ni Over-qualified.

Nadhani sasa ni wakati wa kuangalia kama serikali inania ya kuleta bodi basi wadau wa Elimu hasa CWT na TSC walimu na wadau wengine wakae chini kwa muono mpana kuona faida ya sasa na vizazi vijavyo kwenye taaluma ya Ualimu na tunazohisi kuwa ni changamoto basi tuzijadili na kuzitatua kwa katika hatua za mwanzoni kabisa za uanzishwaji wa Bodi hii ya Kitaalamu ya Walimu.

Hata hivyo Bodi itasaidia sana maana kutakuwa na standard ambazo ndicho kilio chetu kikubwa kwa sasa ambacho nimekosea majibu. Mathalani madarasa yamefurika wanafunzi, walimu ni wale wale, walimu wanafanya kazi zilizopitiliza, hakuna usawa hata wa madaraja tu ya mishahara kwenye HALMASHAURI walizoajiriliwa, richa ya kuwa na mshahara usioendana na mahitaji ya kawaida ya kiuchumi (njiwa), kukaa muda mrefu bila ya mwajiri kukupandisha daraja, stahiki, uhamisho, matibabu na mwisho ni madharau wanayopewa na Wakuu ambao baadhi yao hawana hata sifa za kuwa hapo waliopo ila kwakuwa ni watoto wa mjomba na Shangazi.

Naomba kuwasilisha mjadala huu mzuri
 
Bodi ya kitaaluma itawasaidia ndugu zangu walimu muweze kujiajiri ninyi binafsi. Upande wa maslahi kifedha mf. Mishahara sioni sana japo ukweli ni kuwa mtazidi kupungua sababu sio waalimu wote wataweza kujisajili kwenye bodi na kuwa active yaani kuhuisha leseni zao.

Sisi upande wa sheria hili tunalishuhudia huwenda hata wenzetu madaktari na wahandisi wanaliona pia.

Ila ukweli ulio wazi ambao nitaungana na wewe ni kuwa kuwepo kwa Bodi ya kitaaluma kutairudishia taaluma ya ualimu heshima yake.

Tatizo ama changamoto ni je ni nani ata qualify kuwa mwalimu? Je, mtu wa cheti au diploma ni mwalimu? Au ni msaidizi wa mwalimu? Je shule itatakiwa kuwa na waalimu wangapi na wasaidizi wa walimu wangapi? Kazi za waalimu zitakuwa ni zipi na kazi za wasaidizi wa walimu zitakuwa ni zipi? Mishahara je?

Haya nadhani ni baadhi ya mambo yanayowapa kigugumizi serikali kufikia hili lengo la Bodi.

Huu mfumo wa kibodi utagusa na kuathiri sehemu kubwa sana ya taaluma ya ualimu na hii inatokana na kuwa taaluma ya ualimu imekwishajiwekea misingi/ mizizi imara sana kuivunja inahitajika kujitoa mhanga na kukubali lawama pia ambapo ni JPM tu angeweza hili, kwa sasa simuoni wakulifanikisha kwa inavyostahili Bodi kuwa.
 
Naunga mkono hoja.
Kiuhalisia Tz tunazalisha kwa asilimia kubwa walimu ambao wako chini ya viwango. Bodi itasaidia kufanya standardization, kuchuja wale ambao hawafai na kuongeza viwango vya walimu.

Kuna nchi kuwa mwalimu, iwe ni wa shule ya awali, msingi au sekondari, inahitaji uwe na masters, na pia ukafanye mitihani ya bodi. Kwahiyo standard ya walimu iko juu, wanaheshimika kuliko madaktari na wanasheria. Wameifanya ualimu kuwa prestigious field iliyo na high standards.

Tatizo hatuko serious na elimu yetu. Kila kitu kiko hovyo, si miundombinu, mitaala, walimu au sera.

Hakuna nchi iliyoendelea bila kuwekeza kwenye elimu, kwasababu watu ndo rasilimali kuu ya nchi. Unaweza usiwe na rasilimali nyingine, mfano madini, mbuga za wanyama n.k na bado ukapiga hatua. Ndo maana kila siku tunabaki kusema Singapore na South Korea tulikuwa nao sawa miaka ya sitini lakini leo wametuacha mbali. Hawana madini wala rasilimali zingine za maana, lakini waliwekeza mno kwenye elimu, ndo matokeo yake hayo wametupiga 'gepu' kubwa. Leo ni nchi za dunia ya kwanza.
 
Naunga mkono hoja.
Kiuhalisia Tz tunazalisha kwa asilimia kubwa walimu ambao wako chini ya viwango. Bodi itasaidia kufanya standardization, kuchuja wale ambao hawafai na kuongeza viwango vya walimu.

Kuna nchi kuwa mwalimu, iwe ni wa shule ya awali, msingi au sekondari, inahitaji uwe na masters, na pia ukafanye mitihani ya bodi. Kwahiyo standard ya walimu iko juu, wanaheshimika kuliko madaktari na wanasheria. Wameifanya ualimu kuwa prestigious field iliyo na high standards.

Tatizo hatuko serious na elimu yetu.
Umenena vilivyo, mfano wa hizo nchi ni JAPAN, mwalimu analipwa pesa ndefu kuliko field zingine, pia education system yao is too practical

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Umenena vilivyo, mfano wa hizo nchi ni JAPAN, mwalimu analipwa pesa ndefu kuliko field zingine, pia education system yao is too practical

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Kwanza nchi ambazo zinaiheshimu kada ya ualimu. Ili mtu ukasomee ualimu, vyuo vinachukua "cream", wale waliofaulu kweli kweli, bila ya hivyo ualimu usahau. Ina maana kwa Tz ingekuwa wale waliopata division one au labda two zile za mwanzoni. Sisi tumefanya ualimu ni kwaajili ya form four/six failures au wale ambao walikosa option nyingine.
 
Mjadala mzuri. Mimi binafsi nashindwa nichangie namna gani sababu SHERIA yenyewe inayoianzisha TTPB sijaiona.

Naomba kama kuna mdau anayo aitupie hapa tuweze kuimwaga.
 
Hao wafanyakazi wengine wenye bodi za kitaalamu wameongezewa ngap na kupanda madaraja mangapi awamu ya JPM?

Tukumbuke tatizo sio Bodi tatizo ni mfumo wa Usimamizi wa hizo Bodi...
Hata CWT wakiacha ujinga kama Nzi wanaweza kutengeneza asali kama Nyuki
 
Wadau habari,

Napenda ifikie wakati tufungua mjadala mpana wa uwepo au kutakuwepo kwa Bodi ya Kitaalamu ya Walimu Tanzania (Tanzania Teachers' Professional Board) TTPB.

Tumekuwa na sintofahamu kadhaa hasa kwa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kuona TTPB itaongeza utitiri wa vyombo vinavyomsimamia mwalimu achilia mbali tozo za ada ya kila mwaka ambayo italipwa moja kwa moja na mwalimu na ada za leseni na kuona kama Teachers' Service Commission (TSC) inatosha kabisa kufanya na kuendelea na majukumu hayo.

Ni ukweli usiopingika kuwa KUTOKUWA na bodi maalumu ya kusimamia Professional ya Ualimu imekuwa ni sababu ya kutoheshimika kwa taaluma hii ukilinganisha na taaluma zingine kama za udaktari, uhasibu, sheria n.k. Ukiangalia kwa umakini nchi zinazoheshimu taaluma ya ualimu wanazo bodi za Kitaalumu za Walimu ambazo kazi yake kubwa ni kuweka Viwango na kusimamia na Kuishauri Serikali au mwajiri yeyote wa taaluma hii kuhusu taaluma na weredi husika.

Huu ushauri wa kitaalamu unaoletwa na bodi ndio unamsaidia muajiri kujua nini afanye na nini asifanye kwa mwajiliwa mwenye taaluma husika.

Mapungufu makubwa kwenye taaluma ya Ualimu kwa sasa ni kukosekana kwa viwango (standards) za taaluma hasa kwenye mishahara, uzoefu na elimu za walimu. Tofauti ni kubwa sana. Walimu tunatofautina hata mkiajiriwa na kwa level ya DEGREE tu, ukija shuleni mshahara ni tofauti na ukienda vyuo vya kati na tofauti ni kubwa zaidi ukienda kama tutorial assistant kwenye Elimu ya Juu. Lakini kibaya zaidi ukijiendeleza ndio kama umejichongea utasikia wewe ni kama umejifurahisha tu yaani Masters degree ya Ualimu na ukipata PhD unaambiwa wewe ni Over-qualified.

Nadhani sasa ni wakati wa kuangalia kama serikali inania ya kuleta bodi basi wadau wa Elimu hasa CWT na TSC walimu na wadau wengine wakae chini kwa muono mpana kuona faida ya sasa na vizazi vijavyo kwenye taaluma ya Ualimu na tunazohisi kuwa ni changamoto basi tuzijadili na kuzitatua kwa katika hatua za mwanzoni kabisa za uanzishwaji wa Bodi hii ya Kitaalamu ya Walimu.

Hata hivyo Bodi itasaidia sana maana kutakuwa na standard ambazo ndicho kilio chetu kikubwa kwa sasa ambacho nimekosea majibu. Mathalani madarasa yamefurika wanafunzi, walimu ni wale wale, walimu wanafanya kazi zilizopitiliza, hakuna usawa hata wa madaraja tu ya mishahara kwenye HALMASHAURI walizoajiriliwa, richa ya kuwa na mshahara usioendana na mahitaji ya kawaida ya kiuchumi (njiwa), kukaa muda mrefu bila ya mwajiri kukupandisha daraja, stahiki, uhamisho, matibabu na mwisho ni madharau wanayopewa na Wakuu ambao baadhi yao hawana hata sifa za kuwa hapo waliopo ila kwakuwa ni watoto wa mjomba na Shangazi.

Naomba kuwasilisha mjadala huu mzuri
@balimar nakushukuru sana. Huu naamini utakuwa mjadala mzuri sana. Nimependa wazo lako ni nimelichukua na kulitupia katika group moja la walimu ili niweze kusikia mawazo yao pia.
 
Hata hivyo Bodi itasaidia sana maana kutakuwa na standard ambazo ndicho kilio chetu kikubwa kwa sasa ambacho nimekosea majibu. Mathalani madarasa yamefurika wanafunzi, walimu ni wale wale, walimu wanafanya kazi zilizopitiliza, hakuna usawa hata wa madaraja tu ya mishahara kwenye HALMASHAURI walizoajiriliwa, richa ya kuwa na mshahara usioendana na mahitaji ya kawaida ya kiuchumi (njiwa), kukaa muda mrefu bila ya mwajiri kukupandisha daraja, stahiki, uhamisho, matibabu na mwisho ni madharau wanayopewa na Wakuu ambao baadhi yao hawana hata sifa za kuwa hapo waliopo ila kwakuwa ni watoto wa mjomba na Shangazi.
Hoja ya kuwa na bodi ya kitaaluma ya kusimamia kada ya ualimu na ukufunzi ni mrua sana.
Hapa mwisho umekubali kuongozwa na hisia zaidi kuliko mjadala mzuri ulioanza nao. Umelalamika/kulaumu.
TSC na CWT ni miundo hafifu sana katika kushughulikia usitawi wa kada ya ualimu. TSC wanawaza kufungua kesi (charge) tu kwa walimu pale wanapokuwa na changamoto za kinidhamu. Lakini likija suala la kusimama na mwalimu kutatua kero yake, wanamwacha apambane mwenyewe.
Ni matumaini yangu jambo hili litafanyiwa kazi muda siyo mrefu sana ili wataalam hawa waweze kudhibitiwa vilivyo na hatimaye kupata kizazi cha werevu barabara.
 
@balimar nakushukuru sana. Huu naamini utakuwa mjadala mzuri sana. Nimependa wazo lako ni nimelichukua na kulitupia katika group moja la walimu ili niweze kusikia mawazo yao pia.
Walimu wenyewe inatakiwa waujue huu mjadala

Natamani sana kuona memorandum ya uanzishwaji wa bodi

Ni ukweli usiopingika walimu wanapaswa wajipambanue

Nadhani kuna haja ya kuona namna ya kuendelea taaluma ya ualimu nchini na sio itikadi ya ualimu
 
Back
Top Bottom