JE,WAMACHINGA WA MBAGALA WAMESHINDIKANA?

JE,WAMACHINGA WA MBAGALA WAMESHINDIKANA?

Doctor Ngariba

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2020
Posts
588
Reaction score
951
Nawasalimia wapendwa kwa salamu ya kikombati.
Moja kwa moja kwenye mada kama ilivyo kwenye kichwa cha habari

Juzi nilipita Mbagala na usafiri wangu wa asili (sina gari,boda wala baiskeli) nilichokiona kilinifanya nifikiri labda gen z ya Tanganyika ina jambo lake kupitia wamachinga.Jamaa wamepanga bidhaa zao kuanzia njia ya watembea kwa miguu hadi robo ya barabara ya magari.

Najiuliza maswali haya:-
1. Wamachnga wameshindikana au serikali imeamua kuwahurumia wananchi wake ili wajipatie riziki zao halali?

2. Hawa viranja wa maeneo yale hawajui kuwa miongoni mwa sababu za foleni kuanzia Zakhem hadi Kanisani ni hao wamachinga waliojinyakulia hiyo road?

3. Vipi kuhusu usalama wa watembea kwa miguu ambao wanalazimika mara nyingine kutembea barabarani ili kupisha biashara za wamachinga?

4. Je, wamachinga wenyewe wamejishukuru kwamba wanaona poa tu kupanga biashara zao barabarani?

Maswali ni mengi lakini nadhani niishie hapa maana nisije onekana nina roho mbaya kwa wapiga kura.

Picha wakuu sijapata nilihofia kunajisi biashara za watu au kumbulia kipigo bure.

UHURU BILA MIPAKA NI UTUMWA.
 
Hicho kitu kinafkirisha sana ila Mwisho wa siku ukiona watu wenyewe wanaofanya biashara unaona ni Bora wapate tu riziki .....awapendi ila lyf is really hard
Ni kweli mkuu life is hard lakini inashangazaa kiasi flani maana sometimes nafikiria vipi wateja wao tarajiwa wanapitaje ili kununua bidhaa zao.
 
Wamachinga wameshindikana Tanzania nzima. Kama ilivyo kwa bodaboda. Ni matunda ya kuingiza siasa kwenye Kila kitu.

Mwanzo wa wamachinga kuweka vibanda ilikuwa ni disabled kiosks. Jambo likakuwa mpaka hapa tulipofikia.

Bodaboda walipewa uhuru wa kuvunja sheria kwa kuwa ndio wapiga kura wetu.
 
Wamachinga wameshindikana Tanzania nzima. Kama ilivyo kwa bodaboda. Ni matunda ya kuingiza siasa kwenye Kila kitu.

Mwanzo wa wamachinga kuweka vibanda ilikuwa ni disabled kiosks. Jambo likakuwa mpaka hapa tulipofikia.

Bodaboda walipewa uhuru wa kuvunja sheria kwa kuwa ndio wapiga kura wetu.
Nilitaka kuongea mengi Ila Kwa comment yako umemaliza kilakitu...Jambo lolote duniani la maendeleo ukitanguliza siasa utafeli pakubwa Sana
 
Ingawa hao wamachinga wapo barabarani kabisa Sasa mtoto wa masaki jichanganye ukanyage nyanya za watu hapo mbagala uone mtiti.


Umaskini ni laana
 
Ingawa hao wamachinga wapo barabarani kabisa Sasa mtoto wa masaki jichanganye ukanyage nyanya za watu hapo mbagala uone mtiti.


Umaskini ni laana
LAana kweli kweli.
 
Back
Top Bottom