Je, wamfahamu golikipa huyu?

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,106
Reaction score
12,916
Rene Huguita.
Alipata kuishi katika sayari tuliomo.
Anatoka katika nchi ya Colombia.Mpira kwake ilikuwa ni furaha vituko na vihoja.
Mara nyingi alitoka golini kwake kwenda mbele kuongeza mashambulizi na kupata mabao.
Alikuwa ni mfungaji mahiri wa free kick.

Pichani anaonekana akitumia miguu kuzuia bao,badala ya mikono,hakuna golikipa aliye wahi kuishi katika sayari hii akathubutu mchezo kama huu,manek huko kwao bao likiingia kwa uzembe kama huu,wanakufuturu mapemaa.

Amefanikiwa kushiriki kombe la dunia mara kadhaa.



Huyu jamaa anadaka si masihara.

Anazuia bao kwa miguu.

ni mchangamfu na hutoa maelekezo.


Anaheshimika na pengine ni mwanachama mwenzetu.
 
Ukiingia YouTube wanasema unatakiwa kuwa chizi ili kuweza kudhubutu kufanya robo ya alichokuwa anakifanya huyu jamaaa
 
Mchanyato wake na kina Carlos verderamma na escobar ulikuwa tishio amerika ya kusini kipindi kile ila mbwembwe zilimtokea puani alipotaka kumlamba chenga Roger Milla mwaka wa 90 na kupata bao ambalo ushangiliaji wake alienda penye kibendera na kukata mauno ya nguvu hiyo cameroon ya kina makanaky alfonce yombi bertin ebwele bonaventura djonkep huku stiven tataw beki wa kulia akiwa kepteni kushoto kunde.
 
Ilkua si yakitoto
 
Rene Higuita alikosa mashindano ya WC 94 kwa kuwa alikuwa anatumikia kifungo gerezani. Alikuwa nguzo imara sana kwa Timu ya Taifa ya Colombia na kukosekana kwake kwa kiasi flani iliwagharimu.
 

Mkuu bila kumsahau Bertin Ebwele na Paul Luis Mfede!
 
Mara ya mwisho kumuona akicheza ilkuwa 2002 world cup ilochezwa japan km sio 1998 pale ufaransa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…