Kumekuwa na kawaida ya watanzania kuumia kisa uwepo wa madalali hasa kwenye kutafuta nyumba za kupanga,frame za biashara,ofisi,stoo au maeneo ya biashara ,ambapo madalali huhitaji viwango vikubwa vya malipo kama mwezi mmoja wa kodi ili kumpangisha mteja jambo amabalo huwaumiza sana wapangaji na hulipa kwakuwa hawana namna.
Pia , kutumia muda mwingi kutembea kutafuta nyumba na kuishia kukosa na kutupa pesa kiasi cha kuwafanya watu wawe na stress wanapofikiria kuhama.
Mimi nimekuja na suluhisho la kuandaa Application maaalumu itakayotambulika kwa sheria na taratibu zoote za nchi ambapo hiyo itakuwa na kazi kuu ya kuwakutanisha wenye makazi,ofisi n.k za kupangisha na wapangaji ambapo nyumba na ofisi zitakuwa zikipatikana kwanjia ya App kisha mpangaji akiipenda nyumba atabook moja kw amoja kwawenye nyumba ili aweze kupata huduma hiyo.
Lakini najiuliza je watanzania wako tayari kupokea mabadiriko haya ya kiteknolojia? Wadau naomba tujadiriane hili.