Je, watu wa mikoani na vijijini wakianza vitimbwi wanavyofanyiwa wakienda kwa ndugu zao wa Dar patatosha?

Je, watu wa mikoani na vijijini wakianza vitimbwi wanavyofanyiwa wakienda kwa ndugu zao wa Dar patatosha?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
ila watu wa mijini na kwenye majiji kuna haja ya kujitafakari.

Mwana DSM ukienda mikoani huko au vijijini ukifika ni kawaida sana kukuta ndugu zako walikuwa wanakusubiri stendi zaidi ya saa ufike, umefika utachinjiwa kuku siku ya kwanza, utaishi hata mwezi na hakuna mtu atakupa maswali ya unaondoka lini, misosi utakula utasaza, ukiondoka utapewa hata debe la unga au maharage na hapo ukunbuke wewe ulipeleka tu mkate, unavyoondoka unasindikizwa kabisa wengine wanakubebea begi, kiufupi watu wa huko wengi ni wakarimu.

Ishu inakuja kwa watu wa Dar sasa, yani hata ndugu kaja kumpokea tu ni mtihani, mwenyeji anatoa maelekezo mgeni ampe simu bodaboda na malipo atalipa mgeni ambae hata hio hela haikuwa kwenye bajeti, akifika msosi ulioandaliwa ni ugali tembele yani ugeni wake ni kama hauthaminiki kama sio kumkomoa, baada ya salamu mwenyeji atakua bize na simu au mke wake kitu kinachoanza kukaribisha upweke kwa mgeni, mgeni akikaa siku 2 tu anaanza kuulizwa anaondoka lini, siku ya kuondoka pekee labda ndio mgeni husindikizwa maana ndio anasepa ni kama mzigo umetoka.

Sasa nauliza hivi watu wa huko mikoani nao wakiamua kwenda kwa style hizo kama zenu, je patatosha?
 
Watu wa mjini hawana muda, elewa hilo......na kila kitu ni pesa, hivyo wanaishi kwa bajeti, sasa wewe ukitoka kijijini kwenu na yeboyebo ukifikiri kuna mtu wa mjini ataku entertain itakula kwako, ndo maana mnaishia kukodolea TV masaa 24.......
 
ila watu wa mijini na kwenye majiji kuna haja ya kujitafakari.

Mwana DSM ukienda mikoani huko au vijijini ukifika ni kawaida sana kukuta ndugu zako walikuwa wanakusubiri stendi zaidi ya saa ufike, umefika utachinjiwa kuku siku ya kwanza, utaishi hata mwezi na hakuna mtu atakupa maswali ya unaondoka lini, misosi utakula utasaza, ukiondoka utapewa hata debe la unga au maharage na hapo ukunbuke wewe ulipeleka tu mkate, unavyoondoka unasindikizwa kabisa wengine wanakubebea begi, kiufupi watu wa huko wengi ni wakarimu.

Ishu inakuja kwa watu wa Dar sasa, yani hata ndugu kaja kumpokea tu ni mtihani, mwenyeji anatoa maelekezo mgeni ampe simu bodaboda na malipo atalipa mgeni ambae hata hio hela haikuwa kwenye bajeti, akifika msosi ulioandaliwa ni ugali tembele yani ugeni wake ni kama hauthaminiki kama sio kumkomoa, baada ya salamu mwenyeji atakua bize na simu au mke wake kitu kinachoanza kukaribisha upweke kwa mgeni, mgeni akikaa siku 2 tu anaanza kuulizwa anaondoka lini, siku ya kuondoka pekee labda ndio mgeni husindikizwa maana ndio anasepa ni kama mzigo umetoka.

Sasa nauliza hivi watu wa huko mikoani nao wakiamua kwenda kwa style hizo kama zenu, je patatosha?
Mimi nilifika dar.usiku saa tano kuangaza mwenyeji hayupo ubungo.kupiga sim hapatikani hee.baada ya masaa mawili ndio napigiwa na dada wa kazi umefika wapi dada kalala, chukua bodaboda ikupeleke fery uvuke kuja kigamboni saa saba na nusu hiyo usiku.nafika kigamboni sim haipatikani nikakaa hapo na walinzi baadae anapiga chukua boda tena ikulete dege.hata dege sipajui jamani huyo boda boda alikua ana pepeza pikipiki kila nikitaka kuongea midomo haiwezi sababu ya supidi, Tukawa tunatokomea tu nauliza bado anasema bado saa tisa usiku hiyo, mpaka nafika saa kumi.kufika hamna maji ya kuoga hamna chakula.nikalala nashtuka saa kumi ba mbili dada ananiambia amka tufanye usafi nikasema bado napumzika.Akasema Lazima tutoe magodoro.Nikahamia sebuleni ile usingizi unaanza naambiwa hata hapo nakuja kakae nje.Dah sitasahau nimeacha mkoani mjengo wangu wa maana kitanda nateseka wallah nilitoa chozi.Nilipata homa kali sikununua hata biashara nikarudi nyumbani baada ya siku tatu.mpaka leo nikija Dar nina ndugu lakini nafikia Hotel.Bora lawama kuliko fedheha
 
Ilibidi wanisingizie nimembaka mtoto wa jirani Ili niondoke pale kwao
Nikasema Kama kweli pelekeni kesi Polisi wakawa hawataki
Ndo nikajua watu wa daslamu wanakufukuza kistyle!

Niliondoka mwaka Jana tukakutana kule kijijini wakaanza kujikosha aaah nasikia upo palepale mjini halafu huji kutembelea

Ungekua ule wimbo wa harmonize umetoka ningewaimbia

Wanajikooooo
Wanajikoshaaaaaa🎵🎶
Wanajikooooo 🎶🎵🎼
Wanajikosha🎵🎶
💃🕺🎤🎸🎻🎷🥁🎧📻
 
Hali duni ya maisha inachangia, mtu ana room moja kwa siku akitumia 3000 kafuja pesa, Hana ajira ya maana huyo kuku unaesema anachinjiwa akipenda mkoa huku anaishiaga kula miguu tena mabroiler, Sometimes mkoani inatakiwa ijulikane ni sehemu ambayo tukienda tunaenda kurefresh mind, Huku Dar ni vitani, Sasa ndugu kaja kukutembelea vitani anategemea nini? Hatukatai kutembelewa ila wanatakiwa kujua huku ukisimama nchale ukiinuka nchale.
 
Hali duni ya maisha inachangia, mtu ana room moja kwa siku akitumia 3000 kafuja pesa, Hana ajira ya maana huyo kuku unaesema anachinjiwa akipenda mkoa huku anaishiaga kula miguu tena mabroiler, Sometimes mkoani inatakiwa ijulikane ni sehemu ambayo tukienda tunaenda kurefresh mind, Huku Dar ni vitani, Sasa ndugu kaja kukutembelea vitani anategemea nini? Hatukatai kutembelewa ila wanatakiwa kujua huku ukisimama nchale ukiinuka nchale.
😀😀😀
 
Hio ilikuwa zamani...
Siku hizi utamtishia nani kwamba unaishi Dar?
 
Sehemu ambayo niko comfortable kuitembelea ni nilipotokea kwa wazazi huko mpaka huwa natamani nibakie,lakini huko kwingine siendi hata kwa risasi kwanza wala simuambii mtu kama nimekuja mkoa alipo
 
Wa DSM wanakiwaga wajanja sana mikoani... ukiibuka kwao wamechoka sana. huwa nashangaa eti familia ya watoto 6, mke na Mme wana kula mchele kilo moja... wao wanaujazo gani Wa matumbo?


watoto wangu watatu Range, Median na Mode wanaikamua kilo na hawabakizi hata punje.


DSM mnakwama wapi?...
 
Back
Top Bottom