Je, Wayahudi (Waebrania) ndiyo walijenga mapiramidi ya Misri?

Je, Wayahudi (Waebrania) ndiyo walijenga mapiramidi ya Misri?

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Himaya ya Misri ilianza miaka mingi sana. Ilianzishwa mwaka 3000 kabla ya kuzaliwa Yesu. Huo ulikuwa utawala wa mwanzo wa kujenga dola. Utawala wa mwanzo ukaisha mwaka 2700 hivi kabla ya Yesu.

Kuanzia mwaka 2700--2200 kabla ya Yesu kukawa na utawala unaoitwa wa kale(old kingdom). Huu ndiyo wakati mapiramidi Mengi na makubwa ya Misri yalijengwa. Piramidi kubwa la Giza lilijengwa wakati huu na pharaoh Khufu.

Kuanzia mwaka 2180--2055 BC kulitokea kipindi cha machafuko, vita nk.

Kuanzia 2040--1782 BC kukawa na utawala wa nyakati za kati(Middle kingdom). Kumbuka kuwa toka hapo mwanzo hadi sasa watawala wote walikuwa ni waafrika weusi. Lakini mwishoni mwa kipindi hiki watu kutoka mashariki ya kati wakaanza kuingia Misri. Na Misri ilipata pharaoh wake wa kwanza kutoka mashariki ya kati katika wakati huu. Mwishoni mwa Kipindi hiki ndipo waebrania waliingia nchini Misri.

Kuanzia mwaka 1650--1550BC kulitokea kipindi cha vurugu sana na watu kutoka mashariki ya kati(levant) wakavamia Misri na kuweka utawala wao. Walitawala upande wa kaskazini lakini bado upande wa kusini ilitawaliwa na wamisri wazawa. Wavamizi hao wanaitwa Hyskos.

Kuanzia mwaka 1550--1077BC kinaitwa kipindi cha utawala mpya. Hapa watawala kutoka mashariki ya kati walitimuliwa na kilikuwa kipindi cha mapharaoh mchanganyiko, weupe, weusi na machotara. Ni katika kipindi hiki ndipo waebrania walitoka Misri.

Kuanzia mwaka 1000--300BC kilikuwa kipindi cha mambo mengi, wanubi walivamia na kuanzisha utawala unaoitwa black pharaohs. Wakafukuzwa, nchi ikagawanyika hadi mwishowe kuja kuanzishwa kwa utawala wa wagiriki. Mmoja wa watawala hao wa kigiriki alikuwa ni Cleopatra.

So hapa inaonyesha kuwa.

1. Japo Misri ilikuwa na miradi mikubwa ya ujenzi wa mapiramidi na majengo mengine karibu katika kipindi chake chote. Lakini ujenzi wa mapiramidi na piramidi kubwa kuliko yote lilijengwa miaka 700 kabla ya waebrania kuingia Misri.

2. Mapharaoh wa mwanzo, waliojenga mapiramidi makubwa na kwa miaka kama 1200 walikuwa ni weusi.

3. Ni kweli Misri ilikuwa na mapharaoh weupe lakini walikuja baadaye kama wavamizi.
 
Kuanzia mwaka 1550--1077BC kinaitwa kipindi cha utawala mpya. Hapa watawala kutoka mashariki ya kati walitimuliwa na kilikuwa kipindi cha mapharaoh mchanganyiko, weupe, weusi na machotara. Ni katika kipindi hiki ndipo waebrania walitoka Misri.
Ikiwa Waebrania waliingia misri mwaka 1077BC, na waliishi miaka 430 misri Na wakasafiri JANGWANI miaka 40. manake walifika kanaani mwaka wa 607BC. Je muda miaka 607 ingetosha kujenga nchi, na kutawala kwa watawala wote katika historia tangu Waamuzi Wote, mfalme Sauli Hadi Sulemani, Kisha uhamisho wa babeli ambapo waebrania walitekwa huko kwa miaka 70 na Kisha kurudi na kujenga hekalu lililobomolewa, pia uvamizi wa Waroma then kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Miaka hiyo hapo juu ingetosha ?!
 
Himaya ya Misri ilianza miaka mingi sana. Ilianzishwa mwaka 3000 kabla ya kuzaliwa Yesu. Huo ulikuwa utawala wa mwanzo wa kujenga dola. Utawala wa mwanzo ukaisha mwaka 2700 hivi kabla ya Yesu.

Kuanzia mwaka 2700--2200 kabla ya Yesu kukawa na utawala unaoitwa wa kale(old kingdom). Huu ndiyo wakati mapiramidi Mengi na makubwa ya Misri yalijengwa. Piramidi kubwa la Giza lilijengwa wakati huu na pharaoh Khufu.

Kuanzia mwaka 2180--2055 BC kulitokea kipindi cha machafuko, vita nk.

Kuanzia 2040--1782 BC kukawa na utawala wa nyakati za kati(Middle kingdom). Kumbuka kuwa toka hapo mwanzo hadi sasa watawala wote walikuwa ni waafrika weusi. Lakini mwishoni mwa kipindi hiki watu kutoka mashariki ya kati wakaanza kuingia Misri. Na Misri ilipata pharaoh wake wa kwanza kutoka mashariki ya kati katika wakati huu. Mwishoni mwa Kipindi hiki ndipo waebrania waliingia nchini Misri.

Kuanzia mwaka 1650--1550BC kulitokea kipindi cha vurugu sana na watu kutoka mashariki ya kati(levant) wakavamia Misri na kuweka utawala wao. Walitawala upande wa kaskazini lakini bado upande wa kusini ilitawaliwa na wamisri wazawa. Wavamizi hao wanaitwa Hyskos.

Kuanzia mwaka 1550--1077BC kinaitwa kipindi cha utawala mpya. Hapa watawala kutoka mashariki ya kati walitimuliwa na kilikuwa kipindi cha mapharaoh mchanganyiko, weupe, weusi na machotara. Ni katika kipindi hiki ndipo waebrania walitoka Misri.

Kuanzia mwaka 1000--300BC kilikuwa kipindi cha mambo mengi, wanubi walivamia na kuanzisha utawala unaoitwa black pharaohs. Wakafukuzwa, nchi ikagawanyika hadi mwishowe kuja kuanzishwa kwa utawala wa wagiriki. Mmoja wa watawala hao wa kigiriki alikuwa ni Cleopatra.

So hapa inaonyesha kuwa.

1. Japo Misri ilikuwa na miradi mikubwa ya ujenzi wa mapiramidi na majengo mengine karibu katika kipindi chake chote. Lakini ujenzi wa mapiramidi na piramidi kubwa kuliko yote lilijengwa miaka 700 kabla ya waebrania kuingia Misri.

2. Mapharaoh wa mwanzo, waliojenga mapiramidi makubwa na kwa miaka kama 1200 walikuwa ni weusi.

3. Ni kweli Misri ilikuwa na mapharaoh weupe lakini walikuja baadaye kama wavamizi.

Misri Haijawahi Kuwa Na Pharaoh Mweupe
 
Ikiwa Waebrania waliingia misri mwaka 1077BC, na waliishi miaka 430 misri Na wakasafiri JANGWANI miaka 40. manake walifika kanaani mwaka wa 607BC. Je muda miaka 607 ingetosha kujenga nchi, na kutawala kwa watawala wote katika historia tangu Waamuzi Wote, mfalme Sauli Hadi Sulemani, Kisha uhamisho wa babeli ambapo waebrania walitekwa huko kwa miaka 70 na Kisha kurudi na kujenga hekalu lililobomolewa, pia uvamizi wa Waroma then kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Miaka hiyo hapo juu ingetosha ?!
Soma vizuri. Waliingia Misri ya 1800BC na kutoka mika ya 1500BC, Kipindi Hyksos wanatoka Misri.
 
Historia ni muhimu sana, kama huelewi umuhimu wa historia ya mtu basi uelewa wako una shida.
Sioni umuhimu wowote wa historia
Binadamu anachotakiwa ni kujaribu kuichungulia kesho,Kama hutaweza kuichungulia kesho basi jiandae kisaikolojia kuwa mtumwa wa wanaoitafta kesho yao
 
Sioni umuhimu wowote wa historia
Binadamu anachotakiwa ni kujaribu kuichungulia kesho,Kama hutaweza kuichungulia kesho basi jiandae kisaikolojia kuwa mtumwa wa wanaoitafta kesho yao
Utaichunguliaje kesho kama hujui ulikotoka? Utajua hata kesho iko upande gani?
 
Mkuu Cleopatra hakuwa mweupe ni kutokana na uzuri wake mabeberu wakaamua ku edit story ni kama walivyo edit nyingine nyingi;
Alikuwa ni mgiriki. Uzao wa jenerali Ptolemy aliyekuwa moja ya majenerali wa Alexander the great. Na utafiti zaidi unaonyesha kuwa alikuwa mbaya wa sura sema alikuwa vizuri upstairs na mwenye hila
 
Alikuwa ni mgiriki. Uzao wa jenerali Ptolemy aliyekuwa moja ya majenerali wa Alexander the great. Na utafiti zaidi unaonyesha kuwa alikuwa mbaya wa sura sema alikuwa vizuri upstairs na mwenye hila

Unaamini Ngano Za Wagiriki Mkuu;
 
Unaamini Ngano Za Wagiriki Mkuu;
Siyo ngano, hiyo ndiyo historia ya Misri. Ilianza kuingiliana na wageni miaka ya 1800BC. Kuanzia hapo watawala wakawa mchanganyiko. Lakini kuanzia miaka ya 3000 BC hadi hapo mafarao walikuwa waafrica weusi tu.
 
Siyo ngano, hiyo ndiyo historia ya Misri. Ilianza kuingiliana na wageni miaka ya 1800BC. Kuanzia hapo watawala wakawa mchanganyiko. Lakini kuanzia miaka ya 3000 BC hadi hapo mafarao walikuwa waafrica weusi tu.

Shukrani Mkuu
 
Back
Top Bottom