Wakuu, napenda kujua kama inawezekana kwa hapa Tanzania kuanzisha taasisi/kampuni binafsi ya kufanya upelelezi wa makosa ya jinai na hatimae kuandaa mashtaka na kusimamia kesi hizo mahakamani?
Nakuja na swala hilo kwa kuona kuna kesi za jinai (sina takwimu) hata pale ushahidi unapokuwa dhahiri watuhumiwa wanaachiwa huru na mahakama.
Nashawashika kusema kwamba vyombo vyenye mamlaka hayo (Polisi na Waendesha mashtaka) aidha kwa makusudi; kutokuwa na weledi wa fani; kutumiwa na viongozi au kutokana na kukithiri kwa rushwa haviwajibiki ipasavyo. Aidha utakuta jambo halipelelezwi kabisa au upelelezi utakuwa wa kubabaisha na hata pale upelelezi unapofanyika uandaaji wa mashtaka na uendeshaji wa kesi utafanywa kwa kuacha shaka (loopholes) ambazo hatimae mahakama hazitamtia hatiani mtuhumiwa kwa kigezo cha aidha mashtaka kukosewa kwa kutoendana na matwaka ya kisheria kumtia mtu hatiani, au kuwa na ushahidi wenye kutia shaka kwa vile ushahidi inatakiwa usiwe na shaka (evidence beyond reasonable doubt), na mengi mengineyo.
Kama haiwezekani kuwa na taasisi kama hiyo, WaTz tuna maoni gani?
Nawasilisha kwa mjadala zaidi.
Nakuja na swala hilo kwa kuona kuna kesi za jinai (sina takwimu) hata pale ushahidi unapokuwa dhahiri watuhumiwa wanaachiwa huru na mahakama.
Nashawashika kusema kwamba vyombo vyenye mamlaka hayo (Polisi na Waendesha mashtaka) aidha kwa makusudi; kutokuwa na weledi wa fani; kutumiwa na viongozi au kutokana na kukithiri kwa rushwa haviwajibiki ipasavyo. Aidha utakuta jambo halipelelezwi kabisa au upelelezi utakuwa wa kubabaisha na hata pale upelelezi unapofanyika uandaaji wa mashtaka na uendeshaji wa kesi utafanywa kwa kuacha shaka (loopholes) ambazo hatimae mahakama hazitamtia hatiani mtuhumiwa kwa kigezo cha aidha mashtaka kukosewa kwa kutoendana na matwaka ya kisheria kumtia mtu hatiani, au kuwa na ushahidi wenye kutia shaka kwa vile ushahidi inatakiwa usiwe na shaka (evidence beyond reasonable doubt), na mengi mengineyo.
Kama haiwezekani kuwa na taasisi kama hiyo, WaTz tuna maoni gani?
Nawasilisha kwa mjadala zaidi.