Jee ushawahi fikiria njee ya Boksi??

TOHATO

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2016
Posts
1,336
Reaction score
4,653
Neno umefungwa haimanishi upo gerezani ila Ni jinsi gani fikra zako hazitoki njee ya (unayoyaamini) kutokana na sababu flani. Sababu hizo hueza pelekea kuwa mshabiki pekee bila kuhoji au kuhitaji kudadisi zaidi ya hapo.

Kuwa ndani ya Boksi kunaeza kukawa ni DINI SIASA, au hata SAYANSI.

Ni vipi MTU huwa ndani ya boksi?
Je waelewa upo ndani ya boksi?

MFANO
Ukitaka jua umo ndani ya Boksi angalia inapotolewa mada ya DINI wewe unatetea wapi? Je ushajiuliza kwanini watetea hapo tuu? Unaeza jipa moyo kwa kusema kwa vile ndo sehem sahihi,jee huo usahihi umeufikiria ukiwa njee ya boksi?
Karibia wote Dini tumezikuta toka kwa wazazi hali ilotupelekea kuwa ndani ya Boksi. Na Siku zote DINI hukufanya kuiamini bila kuhoji huku ikiiponda dini nyingine( hapa boksi ndo linapoanzia)
. Ni ngumu kusema ipi ndo Dini sahihi huku ukiwa ndani ya Boksi.

Hata kwenye siasa ,wapo ambao hupenda upande flani(Vyama). Hata kama ataona ubovu mkubwa ndani ya chama chake atatumia njia ya kutetea ili kuufrahisha moyo wake. Ni ngumu kujua mengi kama utasoma gazeti LA (Uhuru,Tanzanite) au kuiskiza TBc kama wewe ni ccm Au kusoma gazeti la Tanzania Daima kama wewe ni mpinzani.

Njia pekee ya kutoka njee ya Boksi ni kwa kusoma vitabu bila upendeleo na ushabiki
 
Hoja naiunga mkono.

Binafsi kwasababu ya kua mdadisi nakujiuliza maswali mengi ambayo yananipelekea kutafuta maarifa , i can assure you mbali na my carrier, ninajua mambo mengiiiiii nabado naendelea kuyatafuta .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…