Jemedari Said: Mpira ni mchezo wa makosa

Jemedari Said: Mpira ni mchezo wa makosa

DullyJr

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
13,983
Reaction score
11,857
Maoni yangu kuhusiana na muda/ dakika zinazoongezwa baada ya dakika 90 za mchezo kumalizika (additional or added minutes), maoni yamejikita kwenye ukweli na uhalisia wa jambo lenyewe kwa wale ambao hawana uelewa kuhusiana na huu muda/dakika za nyongeza.

MPIRA NI MCHEZO WA MAKOSA
Kagere kukosa penati na kudhani kwamba amefanya makusudi ni kumkosea heshima mchezaji. Ukweli kwamba Kagere amewahi kuwa mchezaji wa Simba haina maana yoyote au uhusiano wa Kagere kukosa penati ya jana ambayo iliipa Simba ushindi wa 3-2 baada ya sare ya 1-1 kwa dakika 90.

Ni bahati mbaya (coincidence) kwamba imetokea hivyo ila kwa utamaduni wa mpira wetu kinachoendelea ni kitu cha kawaida na tumekiruhusu, jaribu kufikiria kwamba kama ingekuwa ni mechi ya Simba na Yanga. Simba walibeba ubingwa wa Afrika Mashariki mwaka 1992 pale pale Amaan kwa matuta wakiwafunga Yanga, penati ya mwisho ya Yanga ilipigwa na David Mwakalebela na Mwameja akadaka, mpaka leo watu hawajamsamehe Mwakalebela.

Chibe Hamidu Chibindu akiwa Yanga naye aliwahi kukosa penati katika penati tano tano Mwameja tena akadaka, Simba wakaja kuibuka Mabingwa wa FA Cup kama sijakosea, mpaka leo wapo ambao hawajamsamehe Chibe Chibindu.

Naamini Kagere hakuwa na nia ya kukosa ili kuwapa nafasi Simba, ni sehemu ya makosa kama yale ya Gadiel Michael ambaye alicheza Simba na yale ya Kennedy Juma ambaye aliwahi kucheza Singida, hawakufanya hivyo kulipa fadhila kokote ni makosa tu, soka ni mchezo wa makosa.

NB: Walipofungwa Yanga 3-1 na APR, waliolalamika zaidi ni Simba, jana wamefungwa Singida wanaolalamika zaidi ni Yanga, sijui uhusiano uliopo.

BIN KAZUMARI MTIPA (The voice of the voiceless)
 
Screenshot_20240111-113723.jpg


Soma chronometer hiyo. Dakika za ziada zaidi ya NNE nje ya SITA zilizotolewa, ziliongezwa na matukio gani?
 

Attachments

  • Screenshot_20240111-113723.jpg
    Screenshot_20240111-113723.jpg
    78.4 KB · Views: 3
Bahati mbaya kwa Singida, Mechi nyingi anazocheza na Simba yakitokea makosa ya kibinadamu uwa ni ya kuwa athiri Singida tu na si Simba.

Ninachowashauri Singida, wasikate tamaa waimarishe kikosi Chao awapo mbali Sana kuweza kudhibiti makosa ya kibinadamu.

Waongeze washambuliaji wawili wakali vijana, waongeze mido Moja yenye Kasi, Waige kwa Azam.

Azam kwasasa wameweza kuwadhibiti Simba, ata refa afanye upuuzi Wana mkanda Simba watakavyo.
 
Kikundi cha Malalamiko na Lawama (KIMALA) Mmeamkaje huko, Sisi huku bado tunashangilia kutinga fainali

Mkimaliza kulalamikia jambo lisilowahusu nendeni mkawapokee wenzenu wanarudi leo
Mnashangilia kutinga fainali ya bonanza.
**PUMBA...V
 
SINGINDA KILIO CHENU TUMEKISIKIA....HAO WAPUMBAVU WA KUBEBWABEBWA GOLI 7 ZITAWAHUSU

@Wananchi [emoji617][emoji617][emoji617].
 
Mwenyekiti wa kamati ya waamuzi mapinduzi cup akifafanua katika mahojiano na waandishi wa habari,
Anasema baada ya mchezo wao kama kamati walijaribu kupitia marejeo ya tukio la Kona ya utata iliyo zaa goli na walibaini haikustahili kuwa Kona.
Mwamuzi Alifanya makosa ya kibinadamu.
 
Back
Top Bottom