Jenerali Ulimwengu: Mlio Madarakani Mjifunze Kuchelea

Jenerali Ulimwengu: Mlio Madarakani Mjifunze Kuchelea

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Jenerali Ulimwengu aandika shairi kuwaasa walioko madarakani

MLIO MADARAKANI, JIFUNZENI KUCHELEA


Nakuletea shairi, lino latoka moyoni
Nakuomba likariri, ulitie maanani,
Usije kulighairi, kuniona majinuni,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Uliye nazo akili, huna budi utambue,
Mwenza wako ni adili, uendako mchukue,
La, utakuwa batili, insi wasikutambue,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Jifunzeni kuchelea, mlio madarakani,
Na sudi twawaombea, awalinde Rahmani,
Na pindi mkikosea, basi radhi tuombeni
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Unapokuwa mkubwa, wako ukubwa ogopa,
Hivyo si ulivyoumbwa, hadi ukafika hapa,
Kwa bahati umekumbwa, wakati wewe ni kapa,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Kikataeni kiburi, na tambo za ufidhuli,
Tutawapeni sufuri, mkijifanya ni nduli,
Yenu ni ndefu safari, ya akili si misuli,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Epukeni kuwatisha, watu walio dhalili,
Ogopa kudhalilisha, mtu aso na misuli,
Ukitaka jaribisha, kwa mwamba alo kamili
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Madaraka nisemayo, si ya mmoja tu wengi,
Kila mmoja anayo, kila mtu yake rangi,
Kama hujui unayo, labda wavuta bangi,
Mlio madarakani, Jifunzeni kuchelea
Jifunzeni lugha tamu, haiba inopendeza,
Wajihi wa tabasamu, kila mkijieleza,
Watu watieni hamu, kuja kuwasikiliza,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Ewe mkuu wa kaya, mwenye wake na uledi,
Kisha umekosa haya, umewaacha stendi,
Wakimbilia malaya, nyumbani katu huendi,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Mkikunja nyuso zenu, hovyo mwajiropokea,
Watawacha mwende zenu, nyumbani watarejea,
Wakumbuka nyuso zenu, mazimwi mlopotea,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Wake zako na watoto, nani atayewalea?
Wafifiza zao ndoto, wakati ukibembea,
Wajikalia kushoto, juha unachekelea,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea ,
Msijeona muhali, kwa niliyojisemea,
Wala hayana ukali, utaowaelemea,
Yangu ni ya Kiswahili, lugha iliyotulea,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Kila siku u mkali, wana wanakuogopa,
Wakiuliza maswali, huna jibu la kuwapa,
Wanapokudai wali, wawatupia makopa,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Ki kitamu Kiswahili, na wageni waafiki,
Yawaje hatukubali, nasi tukakipa tiki,
Tukaionja asali, ya muruwa na mantiki,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Na mtemi wa kijiji, ama wewe mwenyekiti,
Watu wanataka maji, wanazo zao risiti,
Wanapokuita huji, kila siku vizingiti,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Kwa kujisemea hovyo, Kiswahili mwakitusi
Hivyo msemavyo sivyo, mnatutia mikosi,
Vyovote vile iwavyo, mu watu wenye nakisi,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea.
Pesa zao umekwiba, umeenda kuolea,
Hujui wameza mwiba, tumboni utatoboa,
Wajiletea msiba, usioutegemea
Walio madarakani, jifunzeni kuchelea
Tamati natua nanga, kituoni napumua,
Mtajaliona tanga, siku nitolifungua,
Mawazo nitayapanga, mengi na yenye murua
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Ni mkuu wa wilaya, ama wako ni mkoa,
Kubali kuwa na haya, watu wakikukosoa,
Situtungie riwaya, majidai kutuboa,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Nakuombea salama, na maisha ya furaha,
Uepushwe na zahama, na kila lenye karaha,
Uzidishiwe karama, uongezewe staha,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
 
Huo ugeneral aliupata jeshi gani huyu mhutu, tumbaku imemuharibu sana
 
Siwezi kusahau walipo mwambia kuwa mzee Ulimwengu siyo mtanzania bali ni mhamiaji haramu
Jenerali Ulimwengu aandika shairi kuwaasa walioko madarakani

MLIO MADARAKANI, JIFUNZENI KUCHELEA


Nakuletea shairi, lino latoka moyoni
Nakuomba likariri, ulitie maanani,
Usije kulighairi, kuniona majinuni,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Uliye nazo akili, huna budi utambue,
Mwenza wako ni adili, uendako mchukue,
La, utakuwa batili, insi wasikutambue,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Jifunzeni kuchelea, mlio madarakani,
Na sudi twawaombea, awalinde Rahmani,
Na pindi mkikosea, basi radhi tuombeni
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Unapokuwa mkubwa, wako ukubwa ogopa,
Hivyo si ulivyoumbwa, hadi ukafika hapa,
Kwa bahati umekumbwa, wakati wewe ni kapa,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Kikataeni kiburi, na tambo za ufidhuli,
Tutawapeni sufuri, mkijifanya ni nduli,
Yenu ni ndefu safari, ya akili si misuli,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Epukeni kuwatisha, watu walio dhalili,
Ogopa kudhalilisha, mtu aso na misuli,
Ukitaka jaribisha, kwa mwamba alo kamili
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Madaraka nisemayo, si ya mmoja tu wengi,
Kila mmoja anayo, kila mtu yake rangi,
Kama hujui unayo, labda wavuta bangi,
Mlio madarakani, Jifunzeni kuchelea
Jifunzeni lugha tamu, haiba inopendeza,
Wajihi wa tabasamu, kila mkijieleza,
Watu watieni hamu, kuja kuwasikiliza,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Ewe mkuu wa kaya, mwenye wake na uledi,
Kisha umekosa haya, umewaacha stendi,
Wakimbilia malaya, nyumbani katu huendi,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Mkikunja nyuso zenu, hovyo mwajiropokea,
Watawacha mwende zenu, nyumbani watarejea,
Wakumbuka nyuso zenu, mazimwi mlopotea,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Wake zako na watoto, nani atayewalea?
Wafifiza zao ndoto, wakati ukibembea,
Wajikalia kushoto, juha unachekelea,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea ,
Msijeona muhali, kwa niliyojisemea,
Wala hayana ukali, utaowaelemea,
Yangu ni ya Kiswahili, lugha iliyotulea,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Kila siku u mkali, wana wanakuogopa,
Wakiuliza maswali, huna jibu la kuwapa,
Wanapokudai wali, wawatupia makopa,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Ki kitamu Kiswahili, na wageni waafiki,
Yawaje hatukubali, nasi tukakipa tiki,
Tukaionja asali, ya muruwa na mantiki,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Na mtemi wa kijiji, ama wewe mwenyekiti,
Watu wanataka maji, wanazo zao risiti,
Wanapokuita huji, kila siku vizingiti,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Kwa kujisemea hovyo, Kiswahili mwakitusi
Hivyo msemavyo sivyo, mnatutia mikosi,
Vyovote vile iwavyo, mu watu wenye nakisi,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea.
Pesa zao umekwiba, umeenda kuolea,
Hujui wameza mwiba, tumboni utatoboa,
Wajiletea msiba, usioutegemea
Walio madarakani, jifunzeni kuchelea
Tamati natua nanga, kituoni napumua,
Mtajaliona tanga, siku nitolifungua,
Mawazo nitayapanga, mengi na yenye murua
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Ni mkuu wa wilaya, ama wako ni mkoa,
Kubali kuwa na haya, watu wakikukosoa,
Situtungie riwaya, majidai kutuboa,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
Nakuombea salama, na maisha ya furaha,
Uepushwe na zahama, na kila lenye karaha,
Uzidishiwe karama, uongezewe staha,
Mlio madarakani, jifunzeni kuchelea
 
TULIKUWA WAMOJA
Kweli corona imekita, kudanganya haifai.
Dunia yote walia, hata wenye utajiri.
Wenzetu wanapambana, siye bado hatujali.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Mlioshika madaraka, hivi mwatupelekapi?
Misingi tumeitoka, twayahama maadili.
Mema tulioachiwa, yanarithiwa na chuki.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Kwa kuringia umwamba, tumesha poteza vingi.
Umoja ulotulea, umekwisha tupwa mbali.
Sasa wapima corona, nao eti wahaini.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Fikra zilizowajaa, kutishana kwa visasi.
Wengine kuwakataa, na kuwazushia uchawi.
Mwanzo wa kushindwa vita, ni dhahiri uko nanyi.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
 
Jiwe na shotii andunje ndugali wakistaafu lazima wakaozee jela hata Kama wakifanikiwa kuuvusha salama muswaada wa kuzuia kushtakiwa.
 
Back
Top Bottom