Kwa habari za kuaminika zilizonifikia hata dakika tatu ( 3 ) kutoka sasa hazijaisha ambazo zimetoka katika chanzo cha kuaminika ndani ya Klabu ya Yanga na Familia nzima ya Jerry Muro iliyopo Dar na Machame kijijini kwao imesema kwamba baada ya tambo zote zile, majigambo yote yale na kujishaua kwake kote kule huku " akipovuka " kwa kupiga " mikwara " yake Mbuzi na " kuidindia " Kamati ya MAADILI ya TFF ni kwamba MKUU WA IDARA YA HABARI NA MAWASILIANO wa Klabu ya Yanga ( wanaosubiri kipigo kingine kikali Jumamosi hii ya Keshokutwa tu ) JERRY CORNELIUS MURO amekubali bila hiyana KUTUMIKIA ADHABU YAKE YA KUTOJIHUSISHA NA MASUALA YA MICHEZO AKIWA KAMA MTENDAJI WA YANGA KWA MUDA WA MWAKA MMOJA ( 1 ).
Inasemekana kuwa Jerry Muro ameamua kukubali yaishe ili aweze kutumia muda huo wa mwaka mmoja kujikita katika KILIMO cha MWENDOKASI huko kwao Machame na kuuza MBEGE kwa wingi ili aweze kupata HELA anazotakiwa kulipa TFF Shilingi Milioni tatu ( 3,000,000/ ) kwani alijaribu kuuomba UONGOZI wa Yanga kuwa umsaidie kulipa hilo DENI lakini akajibiwa jibu moja tu kuwa nanukuu " KILA MTU ATABEBA MZIGO WAKE MWENYEWE ".
Hata hivyo kuna uwezekano mkubwa Jerry Muro asiende kulima na kuuza mbege huko Kwao UMACHAMENI na badala yake akauza ama Gari yake au akakimbia tena kwa TB Joshua kuomba msaada wa KIROHO ili TFF walisahau hilo DENI lao.
Ni hayo tu Wapendwa wana Sports wenzangu. MNYAMA MNYAMANI yupo sasa ULUGURUNI na akitoka huko mtaisoma namba msimu ujao kwa ladha za Kikameruni na Kiganda.