Jerry Muro amtusi tena Haji Manara

Hapo kwa soka la bongo ndipo unapowakuna mashabiki!...ukishangaa ya Muro ungrtaajabu kauli za Mwinakaduguda, kupigwa mshituko na kai za Masu Bwire na ungezimia kwa kauli za Manara na mbwiga wa Mbwiguke


Kauli za Masau Bwire zina mvuto mkubwa japo propaganda ni kubwa kuliko uhalisia. Sikumbuki kuwahi kusikia matusi kabisa au kuponda kabila la mtu. Hata Mbwiga ni burudani tupu. Kaduguda ni ubabe na kiburi. Huyu mwingine sijui tuweke kundi gani....
 
Kipindi kile Muro ana kesi na Police hakuwekwa ndani kidogo? kuna haja ya kufatilia huko ndani alitendewa nini. mnaweza kuwa mna mlaumu kumbe aliathirika kisaikolojia kutokana na vitendo alivyo fanyiwa akiwa huko. hata kama alikaa kwa masaa matatu tu. aangaliwe vizuri. maana wengi huwa wakifanyiwa vitendo hivyo wakitoka wanakuwa hawajiamini so wanatokwa na maneno kama hayo ili kujipa moyo kuwa bado ni wanaume na hamna tatizo.
 
Mzee wakati mwingine kitanda hakizai haramu! Ukiona hiyo ujue wazee walikaa ili kuistiri ndoa yao.
 
maneno ya Muro wakati mwingine ananikosha.... eti simba wana nyota ya paka kupendwa na wachawi...
 
Muanzisha mada una mawili, aidha MNAFIKI au unaionea aibu timu yako ya Simba Koko. Mtu usiye shabiki wala mfuatiliaji wa soka huwezi kubaini mapenzi ya redio fulani kwa timu fulani....acha kujibaraguza.

Mbili, siungi mkono kauli tata kwenye nyanja yeyote. Yanga inapaswa kuwa na AFISA HABARI mwenye nidhamu na adabu ya hadhi ya klabu.

Tatu, Simba ifikie sehemu ithamini ELIMU. Haji Manara na timu ya uongozi wa Simba iachane na zama za mijungu na uswahili kiasi cha kuwa na MSEMAJI kama Haji Manara. Kila kukicha huyu jamaa ni YANGAAA, YANGAAA, mara leo Azam wamebebwa kesho Yanga wafungiwe sijui wamemshika nani makalio...kesho sipeleki timu uwanjani sijui nani ana VIPORO kesho ana hili.

Sina hakika kama Simba Koko ina uongozi wa kimichezo na sio waganga wa kienyeji tena wale matapeli wa Dubai. Kwani Simba Koko haiwezi kucheza mpira uwanjani bila kutajataja Yanga? Simba Koko si walipata nafasi mbili za kukutana na Yanga ana kwa ana, kwa nini wasioneshe huo umahiri uwanjani badala yake ibakie kulialia na kuomba huruma kwenye media kila uchao?

Soka la midomoni limepitwa na wakati

 
mm naomba audio ya hicho kipande nipeleke tff,km huna itakuwa mikia on work......
 
Hao wanajuana nyinyi mnahangaika bure,hamna kesi walanini endeleeni na shughuli zenu,Azam naYanga ruksa na nyinyi subiri zamu yenu ikifika mambo yatakuwa HV hv
 
Acha Uongo mkuu! Mimi pia nilisikiliza kipindi, Jeri hakuongea Kama unavyojaribu kuwaaminisha watu hapo! Unaongeza maneno Ili iweje! Au kwa vile kuanzisha thread hapa Ni bure basi ukikosa cha kuandika unaongeza uongo?
 
Hawa wana beef zaidi na wote wana mdomo mchafu sioni kwa nini une na mfano mmoja.
MAJUZI WAMETUKANANA HADI GROUP MOJA LA WHATSSAP LA MMOJA WA MADC LIKAVUNJWA RASMI ....ilikuwa mbaya mno
 
Mtoa mada ndio wewe mtu mzima anayemzungumzia Jerry au? Mbona imekuuma sana.?
 
Napenda saana malumbano ya Yanga na Simba...lakini SIPENDI wakiingiza matusi kwenye hayo malumbano.Tuitane kanda mbili...Simba koko nk..nk..lakini tusitukanane.
 
Halafu,hivi timu za ulaya zina wasemaji? Au na sisi tumejiongeza kuweka hiki kitengo?
 
Mi naona ni vituko na vijimambo tu ivyo vya Muro na Manana na vinafanya mpira unakuwa na ladha yake nje ya uwanja. ...

Kingine lakini si kwa umuhimu, naona radio EFM imekuja kunoga hapa town balaa...
 
hao wote wanajuana mbona muro alimuambia manara kwamba ualbino wake usiwe kigezo cha kujitetea, lakini baadae jioni wanakula bata wote...hapo hamna tatizo maana wote ni maafisa habari wa vilabu vyao....manara natishia kumshtaki jerry muro kisa kamdhalilisha lakini cha ajabu haendi mahakamani wala TFF sababu hao wote ni mswaiba afu wanataniana..

tena ukiwafuma meza moja wanavyotaniana kama sio hao
 
Post yako umeipost kishabiki sana.Eti kituo cha radio ambacho 90% kina MAHABA ya wazi kwa klabu ya Yanga.
Kumbe hata wewe unawashwa.
 
manara kwa hayo maneno waachen nao wanaligi yao ya maneno katika top 3 wapo
muro
manara
masau bwire sasa sisi tuwaache mbona muro na manara ni marafiko na hata alipomtukana kipnd kile walikuwa poa sana na manara na wakawa wanaenda uwanjan kuangalia mpira wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…