Jerry Muro, kwa Kiingereza chako hiki, hakika umejidhalilisha na kuwatia aibu mno walimu wako wote

Hiyo Already yako ni kama unamchukia sana huyu na kiaina Tanzania ya enzi zile amejitahidi as angeeleweka anasema nini. Nilizani nitakuta kaongea visivyo endana kumbe mwalimu angempa tiki fulani.

ALL READY
kwa nini hukuandika hii ambayo ndio inaelekea ndicho alichosema?
 
Nilifikiri unamshauri atumie kiswahili kumbe na wewe mtumwa tu!!
 
GENTAMYCINE

Mbona wewe hata Kiswahili ni shida! Jirekebishe wewe mwenyewe kwanza unamanisha nn kuanza kila neno kwa herufi kibwa?

Ngoja nikuongezee stress. .."Simba mwenda pole ndio mla nyama" Slow slow of lion Yes, is that eat meat!
 
Last edited by a moderator:
Mbona hata Kiswahili watu tunakosea sana
Licha ya kuwa ndo lugha yetu ya Kwanza.....

Sio watanzania wote Kiswahili ndo lugha yao ya kwanza
wengi kiswahili lugha ya pili...kingereza ya tatu
unaweza kuona hapo matokeo yake
 
Bora Jerry Muro, maana ile si lugha mama. Je we mleta mada huoni uandishi wako ni wa hovyo?. Tangu lini kila neno likaanza na herufi kubwa. Nani alikufundisha uandishi wa namna hii. Hata mtoto wa darasa la pili hawezi kosea kama wewe. Sasa kama umeshindwa kuandika kiswahili kwa ufasaha, tutaaminije maneno ya kiingereza unayodai yametamkwa na Jerry Muro?. Pengine wewe ndiyo umeshindwa kumsikiliza na kumuelewa Jerry vizuri.
 
he is in the 3rd stage of second language acquisition, shida iko wapi hapo? mleta uzi nlijua kakosea kiswahili lugha yake kumbe hyo ya kujifunza !! ok tu assume kakosea then what? what is the relationship between skills alo nazo na kiingereza? the main function of language is to communicate,

as long as mmemuelewa yupo kwa right track
 
kiwe kiingereza kibovu au kizuri sio issue ya kujadili,cha msingi anapiga hela maisha yanaendelea.kuna watu wanajua kiingereza vizuri sana na hawana kazi hiyo lugha inawasaidia nn?
 
Na Spika naye jana kasema Mnyika iam taken reaction

Si Mchezo! Kumbe Ni Ugonjwa Wa Watanzania Wengi? Poleni Sana Na Walaumuni Watawala Wenu Kwa Kuwafukuza Wazungu Mapema Na " Kubaka " Mfumo Mzima Wa Elimu Yenu. Narudia Tena Poleni Sana Watanzania Kwa Kuwa Na Tatizo Kubwa La " Language Barrier ". Kumbe Hata Ras Simba Hatofanikiwa Na Anapoteza Tu Muda Wake Kuwafundisheni Na Kuwafundishieni Watoto Wenu. Poleni Sana Jamani!
 
Mi nimeshakua zamani nilikua napenda Sana hizi ligi. Jerry anatafuta umaarufu.
 
Sio watanzania wote Kiswahili ndo lugha yao ya kwanza
wengi kiswahili lugha ya pili...kingereza ya tatu
unaweza kuona hapo matokeo yake

Hiyo ni kweli.

Lakini kwa mfano mimi, kwangu Kiswahili naweza kusema ndo lugha yangu ya kwanza, Kisukuma ni lugha yangu ya pili, na Kiingereza ya tatu.

Ila pia, hata wale watu ambao Kiingereza ni lugha yao ya kwanza nao hukosea sana tu mbona.

Mfano Barack Obama na G.W. Bush washawahi kukosea Kiingereza mara kadhaa tena hadharani kabisa.

Sasa hao kweli unaweza kusema Kiingereza si lugha yao ya kwanza?
 


Sisi kukosea kingereza ni kama 'kuonekana hujasoma'
naona shida inaanzia hapo...
mtu atakukosoa kama anataka ku prove kwa watu hujaenda shule
au mtu anakukosoa kwa nia nzuri but mtu anaona 'kadhalilishwa'..
 
Sisi kukosea kingereza ni kama 'kuonekana hujasoma'
naona shida inaanzia hapo...
mtu atakukosoa kama anataka ku prove kwa watu hujaenda shule
au mtu anakukosoa kwa nia nzuri but mtu anaona 'kadhalilishwa'..

Naamini hili ndilo ufanya waTZ wengi kuwa waoga kuzungumza kiingereza, kwa hofu ya kukosea na 'kuchekwa' na wengine.

Hii imeanzia kwenye mfumo wa elimu yetu; ambapo kwa mfano katika elimu ya msingi, mtoto anapokosea, basi mwalimu uwaambia wengine wamzomee!! Pia katika ngazi za sekondari na hata chuo, mtu akikosea kuzungumza kiingereza, wengine umcheka!

Haya ni mambo ya ajabu kabisa! Na ni tabia mbaya sana pale mtoto anapojifunza lugha ama jambo lolote lile kuchekwa ama kuzomewa baada ya kukosea. Ni jambo ambalo limejenga mizizi hata pale maprofesa wanapokuwa na harsh criticisms kwa wanafunzi, badala ya kutoa constructive criticisms. Matokeo yake wanafunzi wanajengewa mazingira ya kutojiamini.

Mifano ipo pale waTZ (baadhi) wanapokuwa hawajiamini kuchangia ama kuzungumza mbele ya hadhara kubwa katika mikutano ya kimataifa, madarasa katika vyuo vya nje n.k.
 
Thread ndeeeefu, kumbe tatizo lipo kwenye sentensi moja tu,Ýanga, we are ok'? Kwa mtazamo wangu, kama unaongea swanglish kutamka hivyo ni kawaida tu. Mtoa mada punguza munkari usije kuchinja watu humu manaake naona unatukanana kumbe tatizo lenyewe dogo tu.
 
Baada ya Yanga kupoteza mbele ya Azam Jerry muro amesema The best team has lose ,ameshindwa hata past tense ya lose ambayo ni lost ,alaf et ana masters ,ambayo yanga wanamtumia kuwawakilisha kimataifa ,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…