Jeshi la Korea Kusini limewazuia polisi 3000 kumkamata Rais aliyeondolewa madarakani na bunge

Jeshi la Korea Kusini limewazuia polisi 3000 kumkamata Rais aliyeondolewa madarakani na bunge

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
1735917970313.png

Jaribio la kumkamata Yoon Suk Yeol, Rais wa Korea Kusini aliyeondolewa madarakani na bunge, limegonga mwamba baada ya polisi na wachunguzi wa rushwa takribani 3,000 kuzuiwa na Jeshi la Korea Kusini

Wanasheria wa Yoon wamesema polisi na wachunguzi wanaojaribu kumkamata Yoon wamevunja sheria kwakuwa waranti yao ya ukamataji ipo kinyume cha sheria na kuapa watawachukulia hatua za kisheria kwa kitendo hicho.

Itakumbukwa Bunge la Korea Kusini lilipiga kura ya kumuondoa Yoon madarakani mwezi December mwaka 2024 baada ya Rais huyo kutangaza sheria ya matumizi ya nguvu ya kijeshi akisema ni kwa ajili ya kulinda Nchi yake dhidi ya vitisho vya vikosi vya kikomunisti vya Korea Kaskazini.

PIA SOMA

- Rasmi, Bunge la South Korea lapiga kura kumuondoa Rais Yoon Suk Yeol madarakani baada ya kutangaza utawala wa kijeshi
 

Jaribio la kumkamata Yoon Suk Yeol, Rais wa Korea Kusini aliyeondolewa madarakani na bunge, limegonga mwamba baada ya polisi na wachunguzi wa rushwa takribani 3,000 kuzuiwa na Jeshi la Korea Kusini

Wanasheria wa Yoon wamesema polisi na wachunguzi wanaojaribu kumkamata Yoon wamevunja sheria kwakuwa waranti yao ya ukamataji ipo kinyume cha sheria na kuapa watawachukulia hatua za kisheria kwa kitendo hicho.

Itakumbukwa Bunge la Korea Kusini lilipiga kura ya kumuondoa Yoon madarakani mwezi December mwaka 2024 baada ya Rais huyo kutangaza sheria ya matumizi ya nguvu ya kijeshi akisema ni kwa ajili ya kulinda Nchi yake dhidi ya vitisho vya vikosi vya kikomunisti vya Korea Kaskazini.

PIA SOMA
- Rasmi, Bunge la South Korea lapiga kura kumuondoa Rais Yoon Suk Yeol madarakani baada ya kutangaza utawala wa kijeshi
Aisee
Kumbe ipo serious hivi

Kwa hiyo hapa nchini Jeshi linaweza kutaka kumkamata Mafwele na polisi wakaweza uzio
 
Wanasheria wa Yoon wamesema polisi na wachunguzi wanaojaribu kumkamata Yoon wamevunja sheria kwakuwa waranti yao ya ukamataji ipo kinyume cha sheria na kuapa watawachukulia hatua za kisheria kwa kitendo hicho.
Vita ya kisheria na kikatiba hiyo
 
Wazee wa k drama na k pop kunani tena? Hatujawazoea ivo wenzenu.
 
Back
Top Bottom