Jeshi la Madagascar lavamia hoteli wanayokaa Taifa Stars kwa madai ya kutaka kuwaondoa wachezaji wenye maambukizi ya Corona

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
TFF imethibitisha kuwa wanajeshi wa Madagascar, wamevamia hoteli iliyofikia Taifa Stars huko Antananarivo na kukaa kwenye korido ya vyumba vya wachezaji wakiwa na bunduki kabla ya mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Madagascar. Askari walidai wanataka kuwatoa wachezaji wa Taifa Stars ambao wao wanadai wana maambukizi ya Covid-19.

Your browser is not able to display this video.
 
Mbona sisi wote tushatolewa
 
Mlitaka mkaambukize korona? Tupo kwenye korona na tahadhari ni muhimu sana naungana na jeshi hilo.
 
Wajifunze kwa uto tu,wakomae wapewe certificate za kuthibitisha kukutwa na huo ugonjwa,wasipopewa wasiingize timu uwanjani
 
Tanzagiza ni nchi hatari maana kuna ugaidi mwingi ukute wanajeshi wamepenyezewa za ndani.
 
Hawa Madagascar si ndo walituuzia ile dawa yao ya kolonya?...kwanini sasa wanatufanyia uhuni tena.
 
Kwani Karia hayupo huko?!
 
Kwani lile deni la zile dawa za corona mlilipa?

Na mkicheza mechi ikiisha wanajeshi waingie uwanjani na kuwakamata wote na kuwekwa ndani mpk deni la dawa la Corona mlimalize
 
Wanajeshi wanaingiaje hapo sasa, nchi zingine ni za ajabu sana na hata hivyo wote wameshatolewa mashindanoni.
 
Kwani lile deni la zile dawa za corona mlilipa?

Na mkicheza mechi ikiisha wanajeshi waingie uwanjani na kuwakamata wote na kuwekwa ndani mpk deni la dawa la Corona mlimalize
Zile zililetwa ili kufanya majaribio tu...ile mitishamba hata bongo ipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…