Jeshi la Polisi kukiri kuwa linamshikilia kada wa CHADEMA, Kombo Mbwana, jeshi hilo sasa linapaswa kufumuliwa

Jeshi la Polisi kukiri kuwa linamshikilia kada wa CHADEMA, Kombo Mbwana, jeshi hilo sasa linapaswa kufumuliwa

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Wajibu namba Moja wa Jeshi letu la Polisi nchini ni kuwalinda raia na Mali zao.

Sasa inapotokea Jeshi hilo ndilo linalohusika Kwa kiasi kikubwa na kupotea Kwa raia nchini, wananchi wa nchi hii watakosa kuliamini Jeshi lao la Polisi, jambo ambalo ni la hatari kubwa sana.

Siku ya Jana tarehe 14 tulipata taarifa toka Kwa kamanda wa Polisi wa mkoa wa Tanga, Zakaria Bernard, akikiri kuwa Jeshi hilo linamshikilia kada wa Chadema, Kombo Mbwana, kada wa Chadema, huko wilayani Handeni, Mkoani Tanga, Kwa siku 29 mfululizo Kwa makosa ambayo Jeshi hilo linadai kuwa ni makosa ya kutumia vibaya mitandao ya kijamii

Nchi hii inaendeshwa Kwa mujibu wa sheria na tunaambiwa Kwa mujibu wa Katiba ya nchi, hakuna mtu aliye juu ya sheria.

Sasa niwaulize Jeshi la Polisi, ni kwanini wao ndiyo wanafanya kazi kama wako juu ya sheria, Kwa kumshikilia mtuhumiwa Kwa siku 29 mfululizo, badala ya kumfikisha katika chombo Cha Mahakama, kama inavyotakiwa Kwa mujibu wa sheria??

Huyo kada wa Chadema, alishatangazwa na ndugu zake kuwa watu wasiojulikana walimteka siku 29 zilizopita, lakini wao Jeshi la Polisi, wamekuwa wakikana kuwa hawahusiki na kutekwa kwake na Jeshi hilo halina taarifa yoyote kuwa kada huyo anashikiliwa na kituo chochote Cha Polisi Mkoani humo!

Ndugu zake Kombo Mbwana, walivyotembelea vituo mbalimbali vya Polisi Mkoani humo na Jeshi hilo limekuwa liikikana kumshiikilia mtu huyo.

Sasa Kwa Jeshi hilo kukiri kuwa wamekuwa wakimshikilia Kombo Mbwana Kwa siku 29 mfululizo, tafsiri yake ni kuwa, wamekuwa wakitoa taarifa za UWONGO kuwa Jeshi hilo halimshikiliii Kombo Mbwana, wakati wao ndiyo wanamshikilia!

Suala lingine ni kuwa Jeshi hilo pia linatambua kuwa wao siyo chombo kinachopaswa kutoa haki hapa nchini, Bali ni chombo Cha Mahakama pelee ambacho ndicho lkilichppewa haki hiyo Kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Niwaulize tena Jeshi la Polisi nchini, ni kwanini waliendelea kumshiikilia Kombo Mbwana, Kwa zaidi ya masaa 48, ambapo ni kinyume Cha sheria, badala ya kumpeleka mahakamani, ambako ndiko pekee, Katiba ya nchi inasema ndiyo chombo kilichopewa haki hiyo kisheria ya kuhukumu kama raia yeyote amevunja sheria??

Nitoe wito Kwa Rais weru, ambaye pia ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vyote vya ulinzi na usalama, kulivunja Jeshi hilo na kuliunda upya, kutokana na Jeshi hilo kutoteleleza wajibu wao namba Moja nchini wa kutulinda sisi raia na Mali zetu na kujigeuza kuwa ndiyo adui namba Moja nchini wao kuwa "majambazi" wanaosuka mipango ya kuwateka raia wema hapa nchini!

Pia soma==>>> Boniface Jacob: Kombo amezungushwa mikoa 10 akihojiwa na kuteswa na Polisi kabla ya kurudishwa Tanga
 
Polisi wana madudu mengi mno
Kwa kuwa Jeshi la Polisi ndilo linawalinda watawala, Kwa hiyo watawala hao wanashindwa kuliwajibisha Jeshi hilo, ingawa wanajua waziwazi kuwa Jeshi hilo halizingatii hata PGO, ambayo ndiyo mwongozo wao wa kufanya kazi!
 
kwa hii ccm inavopenda kujifichia humo ni ngumu
Sasa watawezaje kuamua kulikalia kimya Jeshi hilo, wakati wanaona waziwazi kuwa Jeshi hilo ndilo limejigeuza kuwa ndiyo "majambazi" wa kuwateka raia Kila uchao??
 
Angefia mikononi mwao wasingesema. Wangemtupa porini aliwe Na Fisi au baharini. Ni Jeshi katili sana lakini hakuna cha kuwafanya mana mfumo unawaruhusu kufanya watakavyo. Na viongozi wao Wa chama wanasema wazi kuwa ukiwa upinzani Polisi watakushugulikia tofauti na ukiwa CCM. Tukubali tu unyonge huu labda ipo siku Mungu atamaliza ugomvi kama alivyomaliza ugomvi Kati ya kina Nape na Marehemu Magufuli. Sisi, km raia Wa Nchi hii, hatuwezi na hatuna nguvu wala Umoja wa kukataa uonevu wowote. Tusubiri tu ipo siku Mungu atatukumbuka.
 
Angefia mikononi mwao wasingesema. Wangemtupa porini aliwe Na Fisi au baharini. Ni Jeshi katili sana lakini hakuna cha kuwafanya mana mfumo unawaruhusu kufanya watakavyo. Na viongozi wao Wa chama wanasema wazi kuwa ukiwa upinzani Polisi watakushugulikia tofauti na ukiwa CCM. Tukubali tu unyonge huu labda ipo siku Mungu atamaliza ugomvi kama alivyomaliza ugomvi Kati ya kina Nape na Marehemu Magufuli. Sisi, km raia Wa Nchi hii, hatuwezi na hatuna nguvu wala Umoja wa kukataa uonevu wowote. Tusubiri tu ipo siku Mungu atatukumbuka.

Haya maneno ya kinyonge sana...hivi ni mkakati au ni nini? Mimi naamini bado kidogo tu... hata paka mpoole akiwa cornered, mwisho wa siku hugeuka chui.. Ni swala la muda tu.. Kataa Unyonge.
 
Haya maneno ya kinyonge sana...hivi ni mkakati au ni nini? Mimi naamini bado kidogo tu... hata paka mpoole akiwa cornered mwish wa siku, hugeuka chui.. Ni swala la muda tu.. Kataa Unyonge.
Hv kazi ya Polisi ni hiyo ya kumficha mtu? Na walikuwa wanamfanya nn Kwa muda wote huo? Kama kakosea si wampeleke mahakamani? Chakula chake huko Mahabusu ni kodi ya nani maana ndugu hawajui! WaTanganyika wa 2024 siyo wa 1947. Polisi msiandae bomu ndg zangu ili iwe nchi ya amani hekima itawale. Siasa zitaharibu future ya nchi hii. Hao mnaowatii kumbukeni ni wanasiasa wajanja wajanja Kwa faida yao. Sawa ndio waliowaweka hapo, lakini angalieni Katiba na Sheria. Matumbo yao na yenu yatatupeleka pabaya. Huu ni ushauri tu.
 
Hv kazi ya Polisi ni hiyo ya kumficha mtu? Na walikuwa wanamfanya nn Kwa muda wote huo? Kama kakosea si wampeleke mahakamani? Chakula chake huko Mahabusu ni kodi ya nani maana ndugu hawajui! WaTanganyika wa 2024 siyo wa 1947. Polisi msiandae bomu ndg zangu ili iwe nchi ya amani hekima itawale. Siasa zitaharibu future ya nchi hii. Hao mnaowatii kumbukeni ni wanasiasa wajanja wajanja Kwa faida yao. Sawa ndio waliowaweka hapo, lakini angalieni Katiba na Sheria. Matumbo yao na yenu yatatupeleka pabaya. Huu ni ushauri tu.
Ndiyo hiyo hoja ambayo hata Mimi nimewahoji Polisi, hivi kama sheria ndani ya PGO yao wenyewe Polisi inavyosema, kuwa Jeshi la Polisi linapaswa kumshikilia mtuhumiwa yeyote si zaidi ya masaa 48, ni sababu zipi zilizowafanya wao Polisi, wamshikilie Kombo Mbwana, Kwa siku 29 mfululizo, bila kumfikisha Mahakamani??
 
Hii nchi iko vurugu mechi sana, sheria hazifatwi. Wao wanafata amri tu, mkubwa wake, mwanasiasa akisema kamata yule, wanakamata hata kwa kuvunja sheria.

Polisi wamejiwekea adui yao ni mwananchi! Wakati walitakiwa wawe watu wa karibu sana. Ccm wameharibu Mahakama, polisi nasasa Bunge. Kinachotakiwa ni kuwaondosha. Tuanze moja..

Hii nchi ina watu makini sana wa kuweza kuongoza vizuri, bahati mbaya wananchi wengi hawajielewi. Ccm inachukua upenyo hapo, kuifanya kama wanaimiliki hii nchi na kufanya watakavyo. Kutumia polisi na Taasisi zingine, kukandamiza wananchi.
 
Hii nchi iko vurugu mechi sana, sheria hazifatwi. Wao wanafata amri tu, mkubwa wake, mwanasiasa akisema kamata yule, wanakamata hata kwa kuvunja sheria.

Polisi wamejiwekea adui yao ni mwananchi! Wakati walitakiwa wawe watu wa karibu sana. Ccm wameharibu Mahakama, polisi nasasa Bunge. Kinachotakiwa ni kuwaondosha. Tuanze moja..

Hii nchi ina watu makini sana wa kuweza kuongoza vizuri, bahati mbaya wananchi wengi hawajielewi. Ccm inachukua upenyo hapo, kuifanya kama wanaimiliki hii nchi na kufanya watakavyo. Kutumia polisi na Taasisi zingine, kukandamiza wananchi.
Hakika hii nchi, mambo yako shaghala bahaghala
 
Wajibu namba Moja wa Jeshi letu la Polisi nchini ni kuwalinda raia na Mali zao.

Sasa inapotokea Jeshi hilo ndilo linalohusika Kwa kiasi kikubwa na kupotea Kwa raia nchini, wananchi wa nchi hii watakosa kuliamini Jeshi lao la Polisi, jambo ambalo ni la hatari kubwa sana.

Siku ya Jana tarehe 14 tulipata taarifa toka Kwa kamanda wa Polisi wa mkoa wa Tanga, Zakaria Bernard, akikiri kuwa Jeshi hilo linamshikilia kada wa Chadema, Kombo Mbwana, kada wa Chadema, huko wilayani Handeni, Mkoani Tanga, Kwa siku 29 mfululizo Kwa makosa ambayo Jeshi hilo linadai kuwa ni makosa ya kutumia vibaya mitandao ya kijamii

Nchi hii inaendeshwa Kwa mujibu wa sheria na tunaambiwa Kwa mujibu wa Katiba ya nchi, hakuna mtu aliye juu ya sheria.

Sasa niwaulize Jeshi la Polisi, ni kwanini wao ndiyo wanafanya kazi kama wako juu ya sheria, Kwa kumshikilia mtuhumiwa Kwa siku 29 mfululizo, badala ya kumfikisha katika chombo Cha Mahakama, kama inavyotakiwa Kwa mujibu wa sheria??

Huyo kada wa Chadema, alishatangazwa na ndugu zake kuwa watu wasiojulikana walimteka siku 29 zilizopita, lakini wao Jeshi la Polisi, wamekuwa wakikana kuwa hawahusiki na kutekwa kwake na Jeshi hilo halina taarifa yoyote kuwa kada huyo anashikiliwa na kituo chochote Cha Polisi Mkoani humo!

Ndugu zake Kombo Mbwana, walivyotembelea vituo mbalimbali vya Polisi Mkoani humo na Jeshi hilo limekuwa liikikana kumshiikilia mtu huyo.

Sasa Kwa Jeshi hilo kukiri kuwa wamekuwa wakimshikilia Kombo Mbwana Kwa siku 29 mfululizo, tafsiri yake ni kuwa, wamekuwa wakitoa taarifa za UWONGO kuwa Jeshi hilo halimshikiliii Kombo Mbwana, wakati wao ndiyo wanamshikilia!

Suala lingine ni kuwa Jeshi hilo pia linatambua kuwa wao siyo chombo kinachopaswa kutoa haki hapa nchini, Bali ni chombo Cha Mahakama pelee ambacho ndicho lkilichppewa haki hiyo Kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Niwaulize tena Jeshi la Polisi nchini, ni kwanini waliendelea kumshiikilia Kombo Mbwana, Kwa zaidi ya masaa 48, ambapo ni kinyume Cha sheria, badala ya kumpeleka mahakamani, ambako ndiko pekee, Katiba ya nchi inasema ndiyo chombo kilichopewa haki hiyo kisheria ya kuhukumu kama raia yeyote amevunja sheria??

Nitoe wito Kwa Rais weru, ambaye pia ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vyote vya ulinzi na usalama, kulivunja Jeshi hilo na kuliunda upya, kutokana na Jeshi hilo kutoteleleza wajibu wao namba Moja nchini wa kutulinda sisi raia na Mali zetu na kujigeuza kuwa ndiyo adui namba Moja nchini wao kuwa "majambazi" wanaosuka mipango ya kuwateka raia wema hapa nchini!

Pia soma==>>> Boniface Jacob: Kombo amezungushwa mikoa 10 akihojiwa na kuteswa na Polisi kabla ya kurudishwa Tanga
Kesi yake mbona ipo mahakamani, kama kakosa dhamana mahakamani, polisi inahusika vipi?

"Tarehe 16/07/2024 Kombo Mbwana Twaha alisomewa mashitaka matatu ikiwemo (1).kutotoa taarifa kuhusu laini ya simu,(2) kutumia laini isiyo na jina lake pamoja na (3) kutotoa taarifa ya mabadiliko ya laini ya simu."
 
Back
Top Bottom