Jeshi sasa laanza biashara ya ulinzi

Jeshi sasa laanza biashara ya ulinzi

Kite Munganga

Platinum Member
Joined
Nov 19, 2006
Posts
1,773
Reaction score
952
Katika kupitia gazeti la Nipashe nimekumbana na habari yenye kichwa cha habari kinachosema-Jeshi sasa laanza biashara ya ulinzi, na baada ya hapo ilinikumbusha miaka ya 1979/80 hivi wakati Dar ilikuwa inalindwa na JKT pamoja na Polisi hata hivyo ilikuja gundulika kuwa hao hao walikuwa ama wanashirikiana na majambazi au wanaazimisha bunduki zao kwa majambazi, mwisho wake serikali ilisitisha mradi huo, sasa najaribu kuwaza kuwa vijana hawa watakuwa trained kijeshi na wataiva kisawasawa (kumbuka ghasia zote za JKT) na baada ya hapo umpe ajira akalinde mamilioni au mabillioni ya matajiri wetu, sasa swali kubwa ninalojiuliza ni kwa mshahara upi mali hiyo itakuwa salama? kwani hata kama watapewa mshahara unaolingana na JWTZ bado watakosa marupurupu wanayopata wakiwa kambini ambayo hulainisha ugumu wa maisha uraiani, je serikali haioni kuwa inatayarisha hatari kwa watu wake na yenyewe pia? Mfano kijana huyu umpeleke North Mara Barrick akalinde dhahabu ya wale jamaa na huku unamlipa KCC unategemea nini hapo kwa mtu aliyepitia JKT?

Na Lulu George na Godfrey Mushi, Handeni

Serikali imeridhia Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA- JKT), liongezewe nguvu kiutendaji na kuwa kampuni ya ulinzi itakayotoa ushindani kwa makampuni binafsi ya ulinzi yanayotoa huduma hiyo kwa kiwango kisichoridhisha.

Kwa sasa SUMA, imejikita katika ujenzi wa nyumba za serikali, barabara na kutengeneza samani.

Uamuzi wa JKT kuwa na kampuni ya ulinzi, una lengo la kuajiri vijana wanaohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Kanali Ayoub Mwakang’ata, alitoa taarifa hiyo jana wakati akihutubia katika kilele cha mafunzo ya Operesheni Uadilifu yaliyokuwa yakifanyika katika Kambi ya 835 JKT Mgambo wilayani Handeni.

Katika taarifa yake alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na Jeshi hilo wameridhia kampuni hiyo kuanza kazi rasmi mapema mwakani.

Kampuni hiyo imepanga kuboresha huduma za ulinzi kwa kuajiri askari waliopitia Jeshi hilo pekee na kuwasambaza katika maeneo mbalimbali nchini kote wakichuana na makampuni mengine yaliyoko sasa, lakini bila ya kuathiri utendaji wao.

``Suma JKT itakuwa kampuni ya ulinzi rasmi kuanzia mwakani na itachukua vijana waliohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi na si askari wa akiba wa mgambo, mpango huu ni maalumu kwa ajili ya kuwasaidia vijana kama hawa kupata ajira za uhakika baada ya kuhitimu mafunzo haya… na ukweli ni kwamba hatua hii itakuwa ni changamoto kwa vijana wengi wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne kujiunga JKT,``alisema.

Awali Ofisa Utumishi wa JKT Makao Makuu, Meja Elvis Massawe alipohojiwa kuhusiana na hatua iliyofikiwa hadi sasa na Kitengo hicho cha SUMA alikiri kwamba Ofisi hiyo imeshapokea maombi zaidi ya robo tatu ya vijana waliohitimu katika Jeshi hilo nchi nzima wakisubiri kuajiriwa rasmi.

Kwa mujibu wa Ofisa huyo ni kwamba Kampuni hiyo mbadala ya ulinzi itachukua askari wa rika mbalimbali bila kujali umri wao na kwamba bado jeshi hilo linapokea maombi ya yawanaotaka kujiunga na kampuni hiyo.

Katika hatua nyingine, Jeshi hilo limelaani vikali migomo ya wanafunzi wa elimu ya Juu nchini likidai kwamba vitendo hivyo vinatokana na kukosa mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwakuwa hawajafunzwa nidhamu ya kijeshi.

Mkuu wa Kikosi cha JKT Mgambo, Meja Nyiga Singu alimweleza, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Luteni Winfred Lugubi aliyekuwa mgeni rasmi katika kilele hicho kuwa ni vyema sasa serikali ikaona umuhimu wa kurejesha mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria ili vijana watakaopita jeshini na baadae kujiunga na vyuo vya elimu ya juu wasishiriki hata kidogo katika migomo inayoendelea kama ilivyo hivi sasa.

``Afande (Mkuu wa Wilaya) naomba nikueleze mbele ya bosi wangu ambaye ni Kiongozi wa Brigedi ya 303, Brigedia Jenerali Alex Chitenga, kuwa tunaishauri serikali irudishe haraka mafunzo yale kwa mujibu wa sheria kwa vile hii migomo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu itafikia ukomo.

Hii ni kutokana na nidhamu tutakayowafundisha wakati wa operesheni za kijeshi,``alisema Meja Singu.

Katika kilele hicho cha mafunzo ya operesheni uadilifu jumla ya vijana 835 walihitimu mafunzo hayo na walikula kiapo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba watalitumikia Taifa kwa uaminifu na uadilifu mkubwa.

Source: Nipashe
 
hakuna hatari yoyote kwa jeshi kujiingiza kwenye biashara kinachotakiwa ni kuboresha masirahi yao. mbona escortza mamilioni yafedha inafanywa na polisi wenye mshahara wa kcc?
 
hakuna hatari yoyote kwa jeshi kujiingiza kwenye biashara kinachotakiwa ni kuboresha masirahi yao. mbona escortza mamilioni yafedha inafanywa na polisi wenye mshahara wa kcc?

Escort ya fedha ya Polisi ni tofauti kabisa na ulinzi wa 100% wanaotaka kuufanya hawa na ukumbuke kuwa watakuwa kwenye lindo la vitu vyenye thamani akiwa mmoja au na mwenzie tu, hata hivyo hujasikia kuwa Polisi wengi tu wamefukuzwa kwa kushirikiana na Majambazi?
 
Ni hatari kwa jeshi kujiingiza kwenye biashara

Nakubaliana na wewe kabisa katika hili. Ulinzi wa Watanzania lazima ufanywe na polisi walioajiriwa na serikali siyo vikampuni uchwara vitavyoibuka na kuajiri majambazi ambao watajifanya ni walinzi lakini wakati huo huo wakichora mchoro wa jinsi ya kuvamia na kujipatia mamilioni kama siyo mabilioni ya pesa. Serikali itoe kauli haraka ya kupinga tamko hili la jeshi la polisi.
 
Wakuu mimi naomba mnisaidie manake ni kizazi kisichopitia JKT.
Hoja ya hao wakuu kuwa migomo ya sasa vyuo vikuu ni kwa sababu wanafunzi hawakupitia JKT ambako wangefundishwa nidhamu ya kijeshi hivyo wasingegoma ina ukweli wowote?Je huko nyuma pamoja na kuwapo mafunzo ya JKT hakukuwa na migomo vyuo vikuu?Manake kama sikosei nilishawahi kusikia migomo mlimani katika kipindi cha nyerere na kuna rumour nilisikia kuwa Prof Mwandosya kipindi hicho akiwa kiongozi(wa msosi?)mlimani aliwahi kuramba bakora za Rais Nyerere kwa sababu ya kuchochea mgomo
 
Mtarajiwa said:
Manake kama sikosei nilishawahi kusikia migomo mlimani katika kipindi cha nyerere na kuna rumour nilisikia kuwa Prof Mwandosya kipindi hicho akiwa kiongozi(wa msosi?)mlimani aliwahi kuramba bakora za Rais Nyerere kwa sababu ya kuchochea mgomo

Mtarajiwa,

..Dr.Mark Mwandosya amesoma Birmingham University first degree na PhD. hana masters degree.

..inawezekana vipi asome UK, lakini aongoze migomo UDSM, na zaidi achapwe viboko na Chancellor wa UDSM[Mwalimu Nyerere]??

..Afande aliyedai mafunzo ya JKT yataondoa migomo ya wanafunzi hajui analoongea. migomo ilikuwepo tangu miaka ambayo vijana walikuwa wakipitia JKT kabla ya kujiunga na vyuo vikuu.
 
..inawezekana vipi asome UK, lakini aongoze migomo UDSM, na zaidi achapwe viboko na Chancellor wa UDSM[Mwalimu Nyerere]??

- Ni marehemu Mwabulambo, ndiye mtumzima aliyekula mbakora Iklulu.
 
Majambazi karibu wengi ni wanajeshi...Let us wait n see the future of TZ...,

Ni vema wakuu wangeseparate Jeshi na Biashara ya Ulinzi...Kama serikali inataka walinzi wa makampuni wapate basic training za jeshi au la.na SI wanajeshi wakafanye kazi za kulinda Maduka...Yanayotarajiwa kutokea hapa in the near future huenda yakawa sawa na yale ya IRAQ na private security companies!!!

Primary roles za jeshi ni tofauti na hii....nafikiri kila kitengo cha jeshi kina roles zake...next polisi nao watakuwa na private security company... i agree na suala la Ujenzi wa nchi ktk secta zingine..na si Ulinzi...
 
Badala ya kuanzisha kampuni ya ulinzi binafsi, afadhali hiyo JKT ikaungana na polisi kulinda public institutions
 
JKT ni vizuri kufanya biashara kubwa zaidi kama kujiingiza ama kuwekeza ktk viwanda vya silaha, electronics, nguo, marumaru, masanduku na babegi, nk, pia miradi mbali mbali ya ujenzi na uzalishaji zaidi ya wafanyayo sasa kwa kutumia askari wake. Miradi hii itawapa mapato zaidi na kufanya jeshi lijitegemee na kuogeza mapatao ama na bonusi kwa askari wake na kua imara zaidi, lakini lazima kuwepo na sheria za kijeshi kulinda na kuendeleza miradi hiyo ama la sivyo itakufa. Sheria za kijeshi zitasidia sana kuendeleza miradi na kudhibiti ufisadi. Serikali KUU inaweza toa mkopo kwa JKT lakini wakiboronga lazima kuwe na kuwajibika.
Kazi ya ulinzi haitaleta mapato maridhawa kwa Jeshi. Kuajiriwa kulinda mali ya raia, pia kutaongeza mgongano wa moja kwa moja na raia. JKT itaimairika zaidi kwa kuzalisha bidhaa zaidi ambapo wataziuza kwa raia na majeshi mengine ama kuuza nje (kuuza nje lazima serikali isimamie).
Kazi yao ya ULINZI WA TAIFA isiingiliwe na ulinzi wa watu binafsi na mali zao. Hata hivyo wanaweza toa huduma hiyo kwa baadhi ya sehemu muhimu kwa kibali maalum pale serikali inapoona umuhimu kwa mfano miradi mikubwa ya umma ama kibinafsi itoayo mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa.
 
Ikiwa Ikulu watu wanafanya biashara mnashangaa Jeshi? Waacheni nao "wajiongezee" kipato! mnaaambiwa nchi ime switch onto auto Pilot mambo yanajiendesha wenyewe tu tusubiri landing ( kama tutafika )
 
Last edited:
JKT ni vizuri kufanya biashara kubwa zaidi kama kujiingiza ama kuwekeza ktk viwanda vya silaha, electronics, nguo, marumaru, masanduku na babegi, nk, pia miradi mbali mbali ya ujenzi na uzalishaji zaidi ya wafanyayo sasa kwa kutumia askari wake. Miradi hii itawapa mapato zaidi na kufanya jeshi lijitegemee na kuogeza mapatao ama na bonusi kwa askari wake na kua imara zaidi, lakini lazima kuwepo na sheria za kijeshi kulinda na kuendeleza miradi hiyo ama la sivyo itakufa. Sheria za kijeshi zitasidia sana kuendeleza miradi na kudhibiti ufisadi. Serikali KUU inaweza toa mkopo kwa JKT lakini wakiboronga lazima kuwe na kuwajibika.
Kazi ya ulinzi haitaleta mapato maridhawa kwa Jeshi. Kuajiriwa kulinda mali ya raia, pia kutaongeza mgongano wa moja kwa moja na raia. JKT itaimairika zaidi kwa kuzalisha bidhaa zaidi ambapo wataziuza kwa raia na majeshi mengine ama kuuza nje (kuuza nje lazima serikali isimamie).
Kazi yao ya ULINZI WA TAIFA isiingiliwe na ulinzi wa watu binafsi na mali zao. Hata hivyo wanaweza toa huduma hiyo kwa baadhi ya sehemu muhimu kwa kibali maalum pale serikali inapoona umuhimu kwa mfano miradi mikubwa ya umma ama kibinafsi itoayo mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa.

Mkuu, yaani ndio unawaongezea ufisadi. Kama hiyo Meremeta waliyoingia kinmyemela wamekula namna hiyo, sembuse hiyo miradi ambayo itakuwa rasmi!!! Kumbuka kuwa kutakuwa na uwezo mdogo sana wa kuingiza uchunguzi huko kisingizio kikiwa ni kilekile kuwa masuala nyeti ya kijeshi
 
Mimi siona kosa hapa kama nimeelewa vizuri lengo ni kuwapa ajira vijana waliomaliza mafunzo ya ulinzi JKT. Kinachozungumziwa hapa ni ulinzi wa security iwe ktk malls, viwanda ama mashirika yanayohitaji mlinzi..Tumeona pia JKT wakijikita ktk sehemu nyingne za Ujenzi na ndivyo ilivyotakiwa JKT kuwa chombo cha Kujenga Taifa.

Sasa badala ya kutumia Mgambo, JKT imejikita kama employment agency ambaye unaweza kuwaamini zaidi kwa sababu huyo kijana atakuwa amepitishwa na chombo hiki, kuna certain guarantee ya mafunzo na agent wake. Kama kutatokea tatizo la ulinzi JKT wanakuwa answerable badala ya mgambo ambaye atakimbia na hujui wapi pa kuanzia kufuatilia wizi huo.
It sound good, hata Ulaya kuna security guards ambao wamepitia mafunzo ya awali ya Ulinzi na kupewa ajira na vyombo vinavyolinda.
 
Mkandara,

Tatizo hapo hayo ma SMG na SAR yatakapoanza kusambaa ovyo kwenye malindo utakuta "zinakodishwa" na kuwekewa "hesabu" kila usiku ilhali mlinzi kabaki na rungu na asubuhi anarudisha silaha armourer
 
Masatu,
Kweli maneno yako lakini sii JKT watakuwa na utaratibu wa kufuatilia hayo maanake nakumbuka enzi zetu JKT ktk Ulinzi mtu mmoja tu ndiye alikuwa na risas za kweli wengine tuna baruti tu. Kama agency nadhani watakuwa na uatatibu mzuri kuliko Mgambo ambao bado kiutendaji kazi hawakuwa na nafuu..
Ni kweli ukitazama watu na mazingira yetu inahitaji sana askari Polisi lakini sioni tofauti kubwa kati ya Polisi na JKT ikiwa JKT wataweza kujenga upya kitivo hicho kwa malengo ya Ulinzi wa security.
 
Masatu,
Kweli maneno yako lakini sii JKT watakuwa na utaratibu wa kufuatilia hayo maanake nakumbuka enzi zetu JKT ktk Ulinzi mtu mmoja tu ndiye alikuwa na risas za kweli wengine tuna baruti tu. Kama agency nadhani watakuwa na uatatibu mzuri kuliko Mgambo ambao bado kiutendaji kazi hawakuwa na nafuu..
Ni kweli ukitazama watu na mazingira yetu inahitaji sana askari Polisi lakini sioni tofauti kubwa kati ya Polisi na JKT ikiwa JKT wataweza kujenga upya kitivo hicho kwa malengo ya Ulinzi wa security.

Mkandara ndio maana hatuendelei.
 
JKU wameanza kitambo mambo ya Ulinzi...Naona JKT watafanya vizuri zaidi
 
Back
Top Bottom