Jezi Feki za Simba na Yanga, chanzo ni nini?

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,385
Reaction score
10,659
Last weekend niliingia sokoni kwa chinga mmoja nikaona katundika uzi wenye Chata ya vunja bei red, white na kijivu, pia Alikua na matambala yale yenye picha za Misukule kibao ya watani zangu Vyura aka Utopolo au Yanga. Nikauliza bei, full ilikua 15, ila ya juu wa 10-120,000.

Nikajiuliza, Hawa GSM na Vunja bei wamemua kushusha bei ya mzigo wao? Ila baada ya kuchunguza vzr nikakuta ni fekelo! Nimepita pita ndani ya soko nikakuta zipo kibao yani, mitaani Tena full mzigo.

Sasa je, wasambazaji wetu wanadhibitije huu u-fake? Wanaingia hasara kiasi gani?

Kweli biashara ngumu!

Ila poa tu, acha na mtani wangu Mzee Chopeko nae avae uzi wa usukuleni kwa buku 10 Bana, salasini angeitoa wapi...
 
Ununue tisheti ya thelathini wakati za buku teni zipo kisa nini? Hizo jezi si noti kusema hazitumiki, ni nguo za kuvaa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…