Jezi mpya za timu mbalimbali kwa msimu ujao 2021/2022

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Tupo ukingoni mwa msimu huu 2020/2021 ambapo ligi mbalimbali zinaenda kufikia tamati. Kufika tamati kwa msimu huu, ni maandalizi ya kuingia msimu ujao.

Tayari baadhi ya timu zimeshaanza kutoa jezi mpya kwaajili ya msimu ujao.

Nitakuwa nikileta jezi mpya kadiri zitakavyokuwa zikinifikia, kwahyo uzi huu ni endelevu, unataka kujua jezi mpya ya timu yako msimu ujao, kaa nasi hapa kwenye uzi huu!

Karibuni...
 
Jezi ya Man City ya nyumbani ukiitazama vizuri hapo nyuma ya jezi kwa juu, imeandikwa 93:20

Hizo ni dakika ambazo Sergio Agureo alifunga goli la ushindi dhidi ya QPR mwaka 2012 katika siku ya mwisho ya msimu.

Goli hilo ndilo lililowapa ubingwa wao wa kwanza wa EPL huku wenyewe wakijisifu wameshinda ubingwa katika dakika za majeruhi za kocha Alex Ferguson yaani "The Fergie time"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…