Jf ilinikutanisha na tapeli wa mapenzi

msichana ukishamchoma na kumuacha anakuwa mkali huyo dah!. atakusema hadi ujute kwanini umemchoma. utasikia ooh..umeniharibia maisha, kumbe maisha yaliharibika kabla hata hamjaonana. mapenzi si mchezo aisee. unaweza ukafa au ukawa tahila. mi ndo maana huwa sitongozi.
 
Vipi tena mbn umekuwa mkali kwa binti wa watu.
Au ww ndo tapeli mwenyewe,
unajihami kwa kuanza kumshambulia binti.

Yawezekana ndo mimi nilimtapeli
Jamaa atakuwa kala ze duduz
 

Tupo pamoja mkuu huyu tayari kesha liwa ndo maana anaonekana manyoya
 
Mama kiu ya ndoa mama. unaweza kujikuta unaparamamia gume gume lililoshindikana na mitume yote. umakini unahitajika

Pole dada lakini usikate tamaa. Kuna wakati ina-work kwani namfahamu dada mmoja ameolewa happily USA na kupata watoto. Endelea kuwa mwangalifu saana, kama ulivyokuwa hapa. Kikubwa usiwe mrahisi kutoa tundi...
 
pole sana ila sijui lini mtajifunza kuwa uhusiano wa kufaa huwezi kuupata kwenye mitandao
 
Pole sana mwaya,
Nakupongeza kwa kutomgaia utamu,ungeumia zaidi,
Ila pia nina wasiwasi na huyo mdada pia inawezekana kaamua tu kumharibia jamaa baada ya kupigwa chini,

Ulipaswa kuongea na huko mkaka naye ukamsikiliza kwa upande wake ikiwezekana hata kuwakutananisha kuliko ulivotumia hasira,
Inawezekana alikuwa ni X wake na ni king'ang'anizi tu kwa jamaa!
 
jinenee nafsi yako,wanaume wengine hawako unavyodhania wewe,akitoka toka na mkeo,ndo nyie mnaogongesha wasichana.
Heshimu mkeo.

mkuu mimi sijaoa ila naona nyie mlio oa mnavyo fanya. wanaume wengine ambao sio wa kibongo ndo labda hawapo hivyo. wanaume matapeli wa mapenzi tu. ukubali ukatae. hadi aje kuoa utakuta amemwaga wanawake kama 20 hivi. kwani siri.
 
mkuu mimi sijaoa ila naona nyie mlio oa mnavyo fanya. wanaume wengine ambao sio wa kibongo ndo labda hawapo hivyo. wanaume matapeli wa mapenzi tu. ukubali ukatae. hadi aje kuoa utakuta amemwaga wanawake kama 20 hivi. kwani siri.

Hata wanawake nao hivyo hivyo wengi wao unakuta mwanamke anawanaume zaidi ya mmoja na anawapanga kama foleni ya ATM za NMB na hawajuani
 
Pole sana nakumbuka bandiko lako la kutafuta mchumba. Labda niseme na wewe una makosa nasema hivyo kwasababu gani.

1. Inaonekana you were too desparate kutafuta huyo mchumba ndio maana umekutana na haya ungejitahidi kuchukua muda wa kufahamiana nje ya JF (maisha halisi) nafikiri kuna baadhi ya vitu ungevigundua kuhusu huyo mtu.

2. Mimi nilitegemea baada ya kuwasiliana na kuchat mngeweza kuonana physically badala ya kuanza kupeana emails na facebook account kama mtu yuko serious na wewe hawezi kuanza kukupa facebook account yake there's more than that sasa wewe kama uliacha kuuliza mambo ya msingi ukaenda kuuliza facebook account bila hata ya kuonana na mtu face to face sababu hata bila facebook still angekudanganya tu.

3. Hakuchukua muda wa kutosha kumfahamu nje ya JF na ninaposema kumfahamu nje ya JF nadhani unanielewa i believe kwenye mtandao people start as friends and get to know each other vizuri kama ana nia nzuri na wewe lazima atahitaji kujua maisha yako nje ya JF eg..What do you do, where do you live, what kind of life do you live, your family na mengineyo.

4. Ndoa haisakwi, ndoa inakuja yenyewe tu automatically bila kutumia energy nyingi.
 
Hata nje ya JF au social media nyinginezo wapo waongo, neno KWELI katikati ya jamii yetu ni adimu. Hata wewe inawezekana siyo mkweli ndiyo maana ulikutana na wa kufanana nae. Hivyo basi anza wewe kuwa MKWELI na mara nyingi utakutana na mkweli mwenzako. Unatafuta mwanaume JF, una tatizo wewe katika jamii inayokuzunguka. Jamii yote inayokuzumguka hujaona mwanaume au wanaume hawajakuona, something wrong, somewhere!!!
 
4. Ndoa haisakwi, ndoa inakuja yenyewe tu automatically bila kutumia energy nyingi.

Tatizo ni kuwa amekaa zaidi ya miaka 4 hakupata hata mwanaume aliye mtongoza au kumsifia tu ndo maana akaamua kutumia njia hii. Vp mkuu wewe ulivyo ona tangazo hukutuma maombi nini?
 


TF kwa kweli umenena vyema kwani asilimia kubwa ya mahusiano ya sasa wegi hawafuatilii vitu muhimu ambavyo vinasaidia katika maisha ya kila siku .. mfano kwa sasa mtu anaangalia unawasiliana na wakina nani na unafanya nini kuliko kuangalia wewe ukoje kitabia na mwenendo, maisha yako yakoje , umetoka ktk familia yako, mahusiano yako na watu wengine yakoje nk

pia ndoa haitafutwi wala kushinikizwa bali huridhiana kutoka na na mambo mengi zaidi ya facebook, twiter, jf etc
 
Kudos mkuu umeongeza mambo ya msingi sana..😛oa😛oa
 
pia ndoa haitafutwi wala kushinikizwa bali huridhiana kutoka na na mambo mengi zaidi ya facebook, twiter, jf etc

Hapa mkuu umenena kuna kesi nyingi binti analengesha apate mimba ili umuoe na ni wazi umemwambia mtu mcheze kidalipo pasipo kuja kuishi pamoja sasa mtu analengesha mimba na kushinikiza umuoe
 
hiviii inakuwagaa ni maigizooo au??ilaa sisi wanaume viumbe hatariii sanaaa///ila naona wote 2 wake kwa waume 50/50 awaaminiki.mapenzii ya maprosoooo
 

hapo kwenye red ndio palikupelekea ukadondokea pua.next time don't use 'kuchuja chuja and trial and error'. this time you were just lucky na sio ujanja wako as you said.....pole sana anyway and all the best
 
"Mapenzi siyo kitu kipya, mwanzo wake ni zamani,
Mapenzi si lele mama yataka malezi kama mtoto,
Mapenzi siyo mchezo, kusema weka segere tucheze,
Wala mapenzi siyo pesa, kusema kanunue shati,

HAYA MAPENZI NI KITU GANI........EEEEHHHH,

Wasiwasi wa mapenzi ukianza kwa kweli ni adhabu, umpate akupendaye usipate muongo wa mapenzi.

Mapenzi siyo mchezo, kusema weka segere tucheze,
Wala mapenzi siyo pesa, kusema kanunue shati,

HAYA MAPENZI NI KITU GANI........EEEEHHHH,

PANYA HAWEZI KUMLA NYAU.

Diamond Sound - Tanzania - Congo - Diamond Musica - Mapenzi - YouTube
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…