LGE2024 JF kama familia moja muhimu na ya maana sana, my friends, ladies and gentlemen, sote tukajiandikishe bila kukosa, kwa mustakabali mwema wa taifa letu

LGE2024 JF kama familia moja muhimu na ya maana sana, my friends, ladies and gentlemen, sote tukajiandikishe bila kukosa, kwa mustakabali mwema wa taifa letu

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Juma pili hii tar 20.10.2025, zoezi la kujiandikisha kwaajili ya uchaguzi muhimu sana na wa kihistoria wa serikali za mitaa na vijiji Tanzania, litahitimishwa rasmi nchi nzima.

Kama mzalendo na kiongozi mwenye heshima wa familia hii pana ya JF, natoa wito na kuwarai wadau wote humu jukwaani, kuchukua hatua za makusudi, kujitolea na kuwajibika kizalendo, kwenda kujiandikisha na hatimae kushiriki katika zoezi la maamuzi la kupiga kura ili kuchagua wale watakaofaa kuongoza na kushughulika na changamoto mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi katika maeneo tunapoishi.

Platform hii maalumu kama oversight team katika mambo mbalimbali nchini, imesaidia pakubwa sana kuchochea mageuzi na mabadiliko katika mambo mengi sana humu nchini. Hivyo basi ni muhimu sana, sote kama wadau wa kuchochea mabadiliko, kua sehemu ya mchakato huu muhimu kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa ili kua na haki, hoja Lakini pia fursa pana zaidi ya kushauri na kukosoa pale inapobidi badala ya kulalamika au kuzira pekee. Tuisaidie nchi yetu kwa vitendo.

Tututumie vizuri sehemu ya muda mfupi wa siku tatu zilizobaki na kua sehemu ya wapiga kura wa kihistoria Tanzania Nov 27, 2024. :pulpTRAVOLTA:

Mungu Ibariki Tanzania
 
Kwa kuwa kura yangu haiheshiwi.nimeamua kwa hiyari yangu kuto kujiandikisha na sitopiga kura.waendelee tu kujimilikisha nchi hii.siwezi poteza muda wangu huku nikijuwa kabisa wataiba kura.
 
Hatuwezi poteza muda juani tuache kutafuta ugali alafu wataoshinda washapangwa na wanajulikana, madhara makubwa sana yanaonekana baada ya kauli zile za kibaradhuri kuonekana za kawaida kawaida haya kiko wapi? Na nahisi mengine yanakuja watu wamesusa haswaaaa
 
Kwa kuwa kura yangu haiheshiwi.nimeamua kwa hiyari yangu kuto kujiandikisha na sitopiga kura.waendelee tu kujimilikisha nchi hii.siwezi poteza muda wangu huku nikijuwa kabisa wataiba kura.
Nani huyo asie heshimu kura yako hali ya kua una haki na fursa ya kuilinda na kuidai kikatiba?

hiyari yako iwe ni haki na uhuru wako pekeyako, na isiwe usumbufu wala bugudha kwa wengine watakao amua mustakabali wa uongozi wa eneo unaloishi kwa niaba yako..

watakao chaguliwa waheshimiwe na wananchi wote 🐒
 
Ili iweje kama watu wana matokeo tayari. Its wastage of time! Afadhali siku hiyo nikalala hata akili itapata afya kuliko kupoteza mda!!

Siku nitajiandikisha nakupiga kura ni siku kutakuwa na tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.. Hizi chaguzi ni viini macho kama siyo mazingaombwe. Kupotezeana muda!
 
Hatuwezi poteza muda juani tuache kutafuta ugali alafu wataoshinda washapangwa na wanajulikana, madhara makubwa sana yanaonekana baada ya kauli zile za kibaradhuri kuonekana za kawaida kawaida haya kiko wapi? Na nahisi mengine yanakuja watu wamesusa haswaaaa
ikiwa ni kupoteza muda ifike mahali basi pasiwepo na hali ya kulalamika kupita kiasi kwa walioshiriki zoezi hilo na kupewa dhamana ya uongozi. Wanachokifanya ndicho wengi wameamua kiwe hivyo kupitia sanduku la kura, waliona ni kupoteza muda kiwewe kisiwepo basi..

akina nani hao waliopangwa na wanajulikana ndugu mdau?

Infact mpaka sasa,
zoezi la kujiandikisha kwajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa limeenda vizuri mno katika maeneo mengi ya nchi. Huu ni mchakato, yawezekana kuna dosari na kasoro ndogo ndogo katika maeneo fulani fulani.

Hata hivyo,
hiyo haizuii hata kidogo zoezi kukamilika na uchaguzi kufanyika Nov27.2024.

Nadhani mpka sasa zaidi ya 70% ya waliotarajiwa kujiandikisha tayari tayari wamejiandikisha 🐒
 
Screenshot_20241016-202019.png
 
Juma pili hii tar 20.10.2025, zoezi la kujiandikisha kwaajili ya uchaguzi muhimu sana na wa kihistoria wa serikali za mitaa na vijiji Tanzania, litahitimishwa rasmi nchi nzima.

Kama mzalendo na kiongozi mwenye heshima wa familia hii pana ya JF, natoa wito na kuwarai wadau wote humu jukwaani, kuchukua hatua za makusudi, kujitolea na kuwajibika kizalendo, kwenda kujiandikisha na hatimae kushiriki katika zoezi la maamuzi la kupiga kura ili kuchagua wale watakaofaa kuongoza na kushughulika na changamoto mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi katika maeneo tunapoishi.

Platform hii maalumu kama oversight team katika mambo mbalimbali nchini, imesaidia pakubwa sana kuchochea mageuzi na mabadiliko katika mambo mengi sana humu nchini. Hivyo basi ni muhimu sana, sote kama wadau wa kuchochea mabadiliko, kua sehemu ya mchakato huu muhimu kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa ili kua na haki, hoja Lakini pia fursa pana zaidi ya kushauri na kukosoa pale inapobidi badala ya kulalamika au kuzira pekee. Tuisaidie nchi yetu kwa vitendo.

Tututumie vizuri sehemu ya muda mfupi wa siku tatu zilizobaki na kua sehemu ya wapiga kura wa kihistoria Tanzania Nov 27, 2024. :pulpTRAVOLTA:

Mungu Ibariki Tanzania
Nimejiandikisha tayari. Mlio bado twawahimiza mjiandikishe.
 
UKIONA UNALAZIMISHWA KUFANYA JAMBO BASI TAMBUA UNAENDA KUTUMIKA KUNUFAISHA WATU WACHACHE WASIOFAA KTK JAMII...
Ukiona unalazimishwa kwenye fursa basi tambua wewe ndiyo fursa/mtaji...

Mkienda mtapigwa msipoenda mtapigwa... Sasa ya nini kujichosha
 
Kituo ambacho nimejiandikisha nitaomba kuwa wakara ,alafu nimuone mtoto chin ya miaka 18 anakanyaga pale, hana cheti cha kuzaliwa hapigi kura na viboko vitamhusu au mtu anakuja na kura alizopiga yeye na mke wake nyumbani , kitaeleweka , ccm mwisho wa kuchukuliana poa umekwisha ,
 
kama inaleta hela sawa nje na hapo kimeumana!
Jukumu la kutafuta hela linabaki kua ni la mtu binafsi,

lakini jukumu la kutengeneza mazingira mazuri ya kupata pesa linahusu kuwajibika kwako moja kwa moja, hususan kwenye uamuzi wa kumchagua kiongozi wa kujenga, kulinda amani na kusimamia mazingira mazuri na bora zaidi hususan ya kiusalama kwa wewe na wengine kupata hela. Full stop 🐒
 
Jukumu la kutafuta hela linabaki kua ni la mtu binafsi,

lakini jukumu la kutengeneza mazingira mazuri ya kupata pesa linahusu kuwajibika kwako moja kwa moja, hususan kwenye uamuzi wa kumchagua kiongozi wa kujenga, kulinda amani na kusimamia mazingira mazuri na bora zaidi hususan ya kiusalama kwa wewe na wengine kupata hela. Full stop 🐒
Ni jukumu la viongozi pia kutafuta njia nzuri,bora na za uhakika za raia wao kujipatia kipato! kama haina hela haina tija na mipango bila pesa ni kelele!
 
Juma pili hii tar 20.10.2025, zoezi la kujiandikisha kwaajili ya uchaguzi muhimu sana na wa kihistoria wa serikali za mitaa na vijiji Tanzania, litahitimishwa rasmi nchi nzima.

Kama mzalendo na kiongozi mwenye heshima wa familia hii pana ya JF, natoa wito na kuwarai wadau wote humu jukwaani, kuchukua hatua za makusudi, kujitolea na kuwajibika kizalendo, kwenda kujiandikisha na hatimae kushiriki katika zoezi la maamuzi la kupiga kura ili kuchagua wale watakaofaa kuongoza na kushughulika na changamoto mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi katika maeneo tunapoishi.

Platform hii maalumu kama oversight team katika mambo mbalimbali nchini, imesaidia pakubwa sana kuchochea mageuzi na mabadiliko katika mambo mengi sana humu nchini. Hivyo basi ni muhimu sana, sote kama wadau wa kuchochea mabadiliko, kua sehemu ya mchakato huu muhimu kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa ili kua na haki, hoja Lakini pia fursa pana zaidi ya kushauri na kukosoa pale inapobidi badala ya kulalamika au kuzira pekee. Tuisaidie nchi yetu kwa vitendo.

Tututumie vizuri sehemu ya muda mfupi wa siku tatu zilizobaki na kua sehemu ya wapiga kura wa kihistoria Tanzania Nov 27, 2024. :pulpTRAVOLTA:

Mungu Ibariki Tanzania

Comments za watu zinaonesha kabisa watu wanaandamana vichwani mwao na kihisia
 
Ili iweje kama watu wana matokeo tayari. Its wastage of time! Afadhali siku hiyo nikalala hata akili itapata afya kuliko kupoteza mda!!

Siku nitajiandikisha nakupiga kura ni siku kutakuwa na tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.. Hizi chaguzi ni viini macho kama siyo mazingaombwe. Kupotezeana muda!
Yako wapi hayo matokeo gentleman kwa faida ya wadau?

au umeenda kwa mganga na hayo ndiyo majibu ya ramli?

na ikiwa ni kupoteza muda, usije kupoteza muda pia kubweka bweka wakati mambo yatakavyokua yanaamuliwa na yakiendeshwa na ambao unasema ni kupoteza muda right?🐒
 
ikiwa ni kupoteza muda ifike mahali basi pasiwepo na hali ya kulalamika kupita kiasi kwa walioshiriki zoezi hilo na kupewa dhamana ya uongozi. Wanachokifanya ndicho wengi wameamua kiwe hivyo kupitia sanduku la kura, waliona ni kupoteza muda kiwewe kisiwepo basi..

akina nani hao waliopangwa na wanajulikana ndugu mdau?

Infact mpaka sasa,
zoezi la kujiandikisha kwajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa limeenda vizuri mno katika maeneo mengi ya nchi. Huu ni mchakato, yawezekana kuna dosari na kasoro ndogo ndogo katika maeneo fulani fulani.

Hata hivyo,
hiyo haizuii hata kidogo zoezi kukamilika na uchaguzi kufanyika Nov27.2024.

Nadhani mpka sasa zaidi ya 70% ya waliotarajiwa kujiandikisha tayari tayari wamejiandikisha 🐒

70% au 7 %
 
Ni jukumu la viongozi pia kutafuta njia nzuri,bora na za uhakika za raia wao kujipatia kipato! kama haina hela haina tija na mipango bila pesa ni kelele!
kumbe unaelewa gentleman,

nenda kajiandikishe, ukagombee na ukapige kura kuchagua viongozi watakao tengeneza hayo mazingira bora na mazuri zaidi ya wananchi kupata hela 🐒
 
Back
Top Bottom