Jicho langu la tatu kuhusu form Mbovu ya Manchester United ndani ya Siku 8

gasto genaro

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2014
Posts
780
Reaction score
554
Na: Gasto Di Genaro

Ukimwondoa Sir Alex Ferguson, José Mourinho ndio kocha niliyetokea kumhusudu kupita maelezo katika maisha yangu ya ushabiki wa soka.

Mourinho amepata kibarua chake kama meneja wa Man Utd mwaka huu 2016. Kwa hakika, nilipata furaha hadi utosini nilipozipata habari za meneja huyo kapata kandarasi Man Utd.

Mourinho akiwa wa Man Utd, ameianza ligi ya EPL vizuri sana kwa kupata ushindi wa mechi tatu mfululizo, ukiacha ile ya ngao ya hisani ambacho Utd ilimcharaza vibaya mno Leicester city kwa goli 2-1

Lakini ndani ya siku nane zilizopita, Man Utd imekua na matokeo mabovu, na siyo matokeo mabovu pekee, bali na mpira mbovu sana uwanjani..

Ubovu huu wa matokeo ya Manchester United, naweza kusema umesababishwa na sababu mbili kuu; nazo ni Kocha na Uzembe wa baadhi ya wachezaji.

*Kocha*

Mourinho ni kocha mzuri sana, na uzuri wake unatokana na mazuri mengi aliyokwishayafanya.. Japokua ana ubora huo, kuna mambo kadhaa ambayo yamemfanya timu yake ifeli kwa mechi tatu mfululizo..

Ifike pahala Mourinho atambue ya kwamba, soka linabadilika, na mifumo ya soka inabadilika. Kitendo cha Mou kutegemea mpira wa Physic zaidi na kuutelekeza mpira wa creativity kwa kiasi kikubwa, ndicho kilichomfelisha kwenye mechi tatu mfululizo

Mourinho kwa sasa inambidi abadili mfumo na mbinu ili timuicheze kwa ubunifu zaidi na siyo nguvu. Mpira huo wa ubunifu hautopatikana kwa kumtumia mchezaji kama Fellaini,, bali wachezaji kama Carrick, Herrera, Mata and the likes.

Selection ya wachezaji kwenye Mechi tatu zilizopita, pia kimemgharimu Mou. Kitendo cha kumwanzisha Lingaard na Mkhitaryan mechi ya Man city, hakikua sahihi kwani walikua wagonjwa na ndo maana hawakufanya chochote chanya kwenye ile mechi..

Pia kitendo cha kumtegemea Fellaini kwenye moyo wa kiungo, ndiyo kunamgharimu Mourinho mara dufu. Fellaini ni mchezaji mzito, asiye na speed wala ubunifu. Pia Fellaini na Pogba wote ni box to box Midfielders yaani, wanalenda kupanda kushambulia na kuliacha eneo la kiungo wazi... Kuwachezesha viungo wa aina hii kwa pamoja, kunamgharimu timu. Kilichomfungisha chelsea ndo hicho hicho cha kutumia viungo wa aina moja i.e Kante na Matic Halafu Fabregas bench(no creativity). Kwaiyo Fellaini uzito wake ule na kukosa speed, pindi akikutana na kiungo mwenye speed(Fernandinho) anashindwa kuhimili kasi.. Kwahiyo Mou kumtegemea Felaini kumemcost.

Pia kitendo cha kuendelea kugandamana na Rooney, kinaigharimu timu. Nadhani mou aangalie namna ya kumweka Rooney bench. Kuendelea kumpa nafasi ni kosa kubwa.

Kwahiyo, selection ya line up ya wachezaji kama hao niliowataja, kumemwangusha mou kwenye mechi tatu zilizopita.

New Mourinho

Mourinho anadai kuwa anataka kuwa new Mourinho. Nahisi hapa panamfanya timu idorore zaidi. Mou wa sasa siyo yule wa kugomba timu ikizingua. Mou anatakiwa awe mkali, mchezaji ukicheza chini ya kiwango bench likuhusu. Mou wa sasa anawachekeachekea wachezaji.. Aache hilo suala na awe mkali timu itacheza poa.

*Wachezaji*

Kuna baadhi ya wachezaji wa Man Utd kama wameyasahau majukumu yao, na badala yake wanarukaruka tu uwanjani badala ya kufanya wanachotakiwa kufanya. Rooney amekuwa akicheza chini ya kiwango, Rooney huyu wa sasa, anapiga pasi fyongo nyingj, anapoteza mipira mingi, na pia haiungi timu kutoka kwenye moyo wa kiungo hadi safu ya ushambuliaji.. Huyu anatugharimu karibu asilimia 50 ya form yetu mbaya..

Fellaini kama nilivyosema hapo awali, hastahili kuanza, anarukaruka na kukimbia kama kaliwa funza miguuni, na urefu ule hata set pieces anashindwa kuziunga na matokeoye zinadondokea kwa maadui.. Kiungo gani hana ubunifu? Kwa soka la sasa, tunahitaji kiungo mwepesi(hapa utagundua kwann Guardiola amempiga chini Toure Yaya). Fellaini anampa kazi nzito sana Pogba maana utakuta pogba huyo huyo akabe, huyo huyo apandishe timu... Nadiriki kusema kwa sasa Fellaini ni Liability(Mzigo)

Martial. Huyu wa mwaka huu siyo yule wa mwaka jana. Martial anarukaruka tu siku hizi. Nadhani ana tatizo la kisaikolojia. Akalishwe chini, apigwe session ili asahau matatizo yake arudi form.

Way foward :

Mou aache kuwatumia Fellaini na Pogba kwenye Moyo wa kiungo. Partnership hii haitokuja kuleta consistent possitives. Pogba anahitaji achezeshwe na Holding /Defensive Midfielder kama Schneiderlin / Carrick / Schweinsteiger.. Lakini zaidi Morgan Schneiderlin kwasababu, huyu ata offer long term partnership with pogba.. Carrick na Schweinsteiger siyo wa kuwategemea sana maana ni wachezaji wa wodini.

Ni wakati wa kuacha pia Mazoea na kumpiga Rooney Bench na kuweka wachezaji kama Mkhitaryan, Mata, Herrera.

Martial pia asipojirekebisha, nafasi yake ichukuliwe na Memphis Depay.

Kama ningeambiwa nimshauri Mou line up, basi ningemshauri hii

De gea

Valencia Smalling Bailly Shaw

Schneiderlin
Pogba Herrera

Rashford Mkhitaryan
Ibrahimovic

Subs: Memphis, Romero, Carrick, Rooney, Mensah etc
_______________________________

Gasto Di Genaro
Shabiki wa kufa wa Man Utd, Simba Sc, Rvp na Memphis Depay
 

Attachments

  • 1474241878848.jpg
    76 KB · Views: 44
Naunga mkono hoja kuwa aneua timu ni fellain hastahili kuwepo uwanjani. Rooney ni mzigo na pia mata muhim sana ila huyo depay naomba atuache pia maana ni kichaa martial awekwe no yake ajinafas naamin mwlm anayaoja haya
 
UTAJUAJE KAMA UMEONEWA?
1. Baada ya kufanya kazi siku 30, unafukuzwa
kazi bila mshahara.
2. Ukiwa una download kitu kwenye net, inafika
99% alafu inagoma.
3. Unaingia na kibomu kwenye pepa alafu
unashindwa kuelewa mwandiko Wako
mwenyewe.
4. Unanunua simu Leo tsh elfu sabini alafu
kesho zinawekwa kwenye promo zinauzwa elfu
thelathini.
5. Unamualika Demu mkali kwenye dinner
unaagiza samaki alfu mwiba wa samaki
unakukaba kooni.
6. Unakamata manzi alafu unazama nae getoni
alafu unashindwa kusimamisha...
7. Unavunja uhusiano na boyfriend Wako alafu
siku inayofata ananunua gari aina ya vogue ya
shilingi milioni 90.
8. Unanunua pafyumu kali lakini kwapa bado
linatema.
9. Unafanya kazi kwenye kampuni miaka 10 bila
kupandishwa cheo na kuongezewa mshahara.
10. Unamdanganya mkaba roba kuwa huna
simu alafu inaita..
11. Unagombana na mtu barabarani alafu
kufika ofisini unapokwenda kuomba kazi
unamkuta anakufanyia interview.
12. Kama gari lako linatumia muda mwingi
gereji kuliko barabarani.
13. Kwenye pepa matokeo yanatoka umefeli
mathematics na kiswahili pia!!!....
14. Unaingia kwenye pepa alafu unasahau jina
lako la kwanza.
15. Unasajiliwa kama beki kwenye timu ya
barani ulaya alafu jaribio la kwanza unapewa
kumkaba Lionel Messi.
16. Kama mtoto Wako wa pekee anajiunga na
JWTZ.
17. Kama ukikosea ukaweka super glue
machoni badala ya dawa ya macho.
18. Kama utapiga picha photoshop
lakini bado unaonekana m'baya.
19. Kama panya atakula jina lako tu, kwenye
Cheti chako muhimu.
# Kati ya zote ipi ikitokea unakua umeonewa sana??
 
Umenichekesha sana mkuu
 
Mtaandika sana mwaka huu...the Unlucky One.
 
Mtoe smalling hapo muweke Blind..
 

hamna bana unamuonea Maureen wa watu.

sababu kubwa alizozitoa yeye kama mtaalamu ni hizi 4:

1. marefa wanapendelea
2. lady luck ameisusa manure
3. Lukewarm Sha-ha-wa aliboronga kama Oscar Joshua wa timu fulani
4. yeye mwenyewe Maureen....hii aliitaja kwa herufi ndogo na sauti ya chini kabisa!
 
Ndugu mwandishi kwenye bandiko lako umeandika kuwa pogba ni box to box midfilder sasa sijui umeandika kimakosa au umekusudia ila what i know pogba si box to box midfilder
 
Ndugu mwandishi kwenye bandiko lako umeandika kuwa pogba ni box to box midfilder sasa sijui umeandika kimakosa au umekusudia ila what i know pogba si box to box midfilder
Kama siyo bix to box Midfielder, ni nani?
 
kwangu mimi matokeo yale yalikuwa psychological blow kutokana na kipigo cha Man City!!!thats all
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…