Hakuna nchi inayoweza kutokomeza ugaidi kwa asilimia 100% ikumbukwe kwamba hawa tunaoita magaidi, kunao wanawaona kama mashujaa, na hilo tumeliona hata humu JF, kuna baadhi ya Watanzania waislamu na pia nilishangaa kuona baadhi Watanzania Wakristo pia walikesha humu wakisifia na kuchekea wakati mauaji yalikua yakiendelea. Hivyo ina maana magaidi hawawezi kutokomezwa kwa mtutu wa bunduki, hata ukiua wangapi, bado kuna wanaozaliwa na kuaminishwa hizo itikadi.
Kinachowezekana ni kupunguza matukio ya kigaidi, na hii inabidi juhudi ziongezeke za kuwahusisha jamii haswa ya Wasomali, kuwaonyesha upande wa pili wa shilingi, manufaa ya amani na nia njema, ukishinda vita kwenye mioyo ya hawa Wasomali, utakua umepunguza ugaidi pakubwa maana watatoa ushrikiano mkubwa, ikiwemo kuwafukuza wageni waliojaa kwao ambao wanahusika pakubwa kwenye ugaidi, kunao magaidi wakutoka mataifa tofauti kule Somalia, wakiwemo mamia ya Wakenya, Watanzania na hata Waarabu.
Changamoto za ugaidi Kenya sio za kawaida, hakuna nchi Afrika yenye changamoto kama za Kenya, kila mtu anayejadili kuhusu ugaidi Kenya lazima atulie na kuwaza haya hapa
- Wakenya wenye asili ya Kisomali ni zaidi ya 800,000
- Hawa hauwezi kuwatofautisha na ndugu zao kule, ni kama Mmaasai wa Kenya avae shuka na kutembea barabara za Dar, huna jinsi ya kumtofautisha na Mmaasai wa Tanzania, nimewahi kuwaona Wamaasai wa Tanzania ambao Kiswahili ni changamoto kwao, tena pale Morogoro.
- Wakenya hawa wenye asili ya Kisomali tumeingiana nao yaani hadi tumewahi kuwa na mkuu wa majeshi mwenye asili ya Kisomali. Kwa hivyo hauwezi ukaamka na kukurupuka uanze kuwabagua.
- Wamemiliki mkoa mmoja mkubwa, ambao upo kwenye mpaka na Somalia
- Mpaka wa Kenya na Somalia ni pori tupu na jangwa, ni vigumu kuendesha shughuli za usalama pale, japo serikali inawekeza kuweka ukuta, lakini kwangu mimi na kwa maoni yangu hayo ni mawazo ya kipumba tu
Kama nilivyosema hapo juu, njia rahisi ya kupunguza ugaidi Kenya ni kuwahusisha jamii, haswa hawa Wakenya wenye asili ya Kisomali, kuwafanya wawaone wale kama magaidi na sio mashujaa, maana wanajificha ndani yao, kuendelea kuwahusisha kwenye ujenzi wa taifa na kuchochea uzalendo, na pia kule Somalia, KDF wazidishe uhusiano mwema na raia walio na mtizamo wa kati.
Lakini pia viongozi wa dini wahusishwe pakubwa kwenye kuhubiri amani, maana na wao ndio wamekuwa mwiba, humo kwenye ibada ndipo wanahubiri chuki za kidini na kusababisha waumini kuiva na kuwa tayari kulipuka.
Hii ramani hapa chini inaonyesha mikoa ya Kenya, mkoa namba tano unaishi hao Wakenya wenye asili ya Kisomali na ndio mpakani mwa Kenya na Somalia, hivyo kila siku wanahusiana kwenye mambo yao, ni vigumu kuwatenganisha, ni kama Wamaasai Wakenya na Watanzania, wale huwa na undugu ambao imekua vigumu kuwatenganisha hata ukikamata ng'ombe wala nini, kila siku wanapishana kwenye mpakani na kusaidiana kwa hali na mali.
https://upload.wikimedia.org/wikipe...ed.svg/300px-Kenya_Provinces_numbered.svg.png