GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Watanzania bhana yaani kila ukipita pamoja na Wachambuzi wenu Uchwara utasikia kuwa eti leo Taifa Stars a.k.a Makonda CCM FC huko Misri itaifunga Algeria na Kusubiria Best Loser ambapo Tanzania inaweza Kupita. Yaani hamna hata Aibu kwa jinsi mnavyoota mchana Kweupe kabisa huku mkijipa Moyo Kipuuzi kabisa wakati mnajua fika kuwa Mpira ni Mchezo wa Sayansi ambayo bahati mbaya ndani ya TFF na Taifa Stars hakuna Sayansi bali kuna Uswahili mtupu.
Kama jana Misri ( Wenyeji ) ambao walikuwa tayari wameshafuzu 16 ila walicheza Full Mkoko dhidi ya Uganda ndiyo mnadhani leo Algeria nao watakuja Kizembe Kizembe na wawapangieni Kikosi dhaifu? Leo tunapigwa Goli za Kutosha tu na hivi Manula na Nyoni ni Wagonjwa huku Kelvin Yondan, Hassan Kessy na David Mwantika hawachezi kwakuwa wana Kadi za Njano ndiyo tutajuta kwanini tumeenda Kushiriki AFCON na kwanini TFF imejikabidhisha rasmi kwa Mkuu wa Mkoa Makonda na CCM yake.
Naomba Mungu na leo pia Mbweha wa Jangwani ( Desert Fox ) Timu ya Taifa ya Algeria kama walivyonipa Furaha Senegal na Kenya kwa Kutufunga Tanzania basi nawaomba na Wao leo watufunge Tanzania na tena si kwa idadi ndogo ya Mabao ( Magoli ) bali yawe ni mengi sana ili tukome, tujifunze na tushike Adabu.
Bado nasisitiza kuwa nitarejea Kuishangilia Taifa Stars pale tu Kocha Emanuel Amunike atafukuzwa rasmi , Makonda akiondolewa katika Kamati kwani anaharibu, anamuingilia Kocha na anaendekeza Siasa ndani ya Timu na pia Wachezaji wangu Vipenzi ambao nina uhakika Mapengo yao yameonekana katika Kikosi Jonas Mkudena Ibrahim Ajib wataitwa Kikosini. Basi sijaona Kiungo bora wa Ukabaji nchini Tanzania kwa sasa kama Mkude na pia bado sijaona Kiungo mchezeshaji na mwenye Vitu vingi ( Udambwi Dambwi ) kama Ibrahim Ajib na nina uhakika kwa jinsi alivyo Nahodha wetu Mbwana Samatta basi nyuma yake angekuwepo Ajib huenda Samatta hadi sasa angekuwa anaongoza na Ufungaji wa Magoli.
Natanguliza pongezi zangu za dhati kabisa za awali kwa Timu ya Taifa ya Algeria ili leo watufunge vizuri na Kikatili.
Kama jana Misri ( Wenyeji ) ambao walikuwa tayari wameshafuzu 16 ila walicheza Full Mkoko dhidi ya Uganda ndiyo mnadhani leo Algeria nao watakuja Kizembe Kizembe na wawapangieni Kikosi dhaifu? Leo tunapigwa Goli za Kutosha tu na hivi Manula na Nyoni ni Wagonjwa huku Kelvin Yondan, Hassan Kessy na David Mwantika hawachezi kwakuwa wana Kadi za Njano ndiyo tutajuta kwanini tumeenda Kushiriki AFCON na kwanini TFF imejikabidhisha rasmi kwa Mkuu wa Mkoa Makonda na CCM yake.
Naomba Mungu na leo pia Mbweha wa Jangwani ( Desert Fox ) Timu ya Taifa ya Algeria kama walivyonipa Furaha Senegal na Kenya kwa Kutufunga Tanzania basi nawaomba na Wao leo watufunge Tanzania na tena si kwa idadi ndogo ya Mabao ( Magoli ) bali yawe ni mengi sana ili tukome, tujifunze na tushike Adabu.
Bado nasisitiza kuwa nitarejea Kuishangilia Taifa Stars pale tu Kocha Emanuel Amunike atafukuzwa rasmi , Makonda akiondolewa katika Kamati kwani anaharibu, anamuingilia Kocha na anaendekeza Siasa ndani ya Timu na pia Wachezaji wangu Vipenzi ambao nina uhakika Mapengo yao yameonekana katika Kikosi Jonas Mkudena Ibrahim Ajib wataitwa Kikosini. Basi sijaona Kiungo bora wa Ukabaji nchini Tanzania kwa sasa kama Mkude na pia bado sijaona Kiungo mchezeshaji na mwenye Vitu vingi ( Udambwi Dambwi ) kama Ibrahim Ajib na nina uhakika kwa jinsi alivyo Nahodha wetu Mbwana Samatta basi nyuma yake angekuwepo Ajib huenda Samatta hadi sasa angekuwa anaongoza na Ufungaji wa Magoli.
Natanguliza pongezi zangu za dhati kabisa za awali kwa Timu ya Taifa ya Algeria ili leo watufunge vizuri na Kikatili.