Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
JIFUNZE HISTORIA YA TANU KUTOKA MAKTABA YA MOHAMED SHEBE
Angalia umma uliokuwa unahudhuria mikutano ya TANU Mnazi Mmoja.
Nimefahamishwa kuwa shajara (diary) za Abdul Sykes zina hotuba za Nyerere (verbatim) katika short hand (hati mkato).
Bahati mbaya sana hizi shajara hadi leo hazijafunguliwa.
Niliziomba kuzisoma wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes lakini sikupewa na niliziona kwa macho yangu nyumbani kwa mwanae marehemu Kleist.
Katika picha hiyo kuna sehemu kushoto inaonekana rangi nyeusi tupu.
Hao ni wanawake wa Kiislam waliokuwa wanahudhuria mikutano ya TANU walitengewa sehemu yao maalum.
Ilikuwa kazi kubwa sana kuwatoa akina mama uani kuwaleta Mnazi Mmoja uwanjani kuja kupiga vigelegele na kuzigeuza nyimbo za lelemama kuwa nyimbo za kuhamasisha wananchi dhidi ya ukoloni.
Mama Sakina (Bi. Chiku bint Said Kisusa) mke wa Shariff Abdallah Attas alifanya kazi kubwa akishirikiana na Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee na Bi. Hawa Maftah kuwaingiza wanawake katika TANU.
Picha ya pili niliowatambua nimewaandika majina yao kwenye picha - Sheikh Suleiman Takadir, Iddi Faiz Mafungo, John Rupia, Rashid Kawawa, Said Maswanya na Robert Makange.
Picha ya tatu Julius Nyerere anasalimiana na wananchi 1956.
Picha ya nne kulia Bi. Titi Mohamed, Mama Maria Nyerere, Julius Nyerere, Rashid Kawawa na nyuma ya Nyerere ni Tewa Said Tewa.
Picha TANU ni siku ya uhuru wa Tanganyika 9 Desemba 1961.
Julius Nyerere na Prince Philip kulia kabisa anaonekana Sheikh Abdalla Iddi Chaurembo.
Angalia umma uliokuwa unahudhuria mikutano ya TANU Mnazi Mmoja.
Nimefahamishwa kuwa shajara (diary) za Abdul Sykes zina hotuba za Nyerere (verbatim) katika short hand (hati mkato).
Bahati mbaya sana hizi shajara hadi leo hazijafunguliwa.
Niliziomba kuzisoma wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes lakini sikupewa na niliziona kwa macho yangu nyumbani kwa mwanae marehemu Kleist.
Katika picha hiyo kuna sehemu kushoto inaonekana rangi nyeusi tupu.
Hao ni wanawake wa Kiislam waliokuwa wanahudhuria mikutano ya TANU walitengewa sehemu yao maalum.
Ilikuwa kazi kubwa sana kuwatoa akina mama uani kuwaleta Mnazi Mmoja uwanjani kuja kupiga vigelegele na kuzigeuza nyimbo za lelemama kuwa nyimbo za kuhamasisha wananchi dhidi ya ukoloni.
Mama Sakina (Bi. Chiku bint Said Kisusa) mke wa Shariff Abdallah Attas alifanya kazi kubwa akishirikiana na Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee na Bi. Hawa Maftah kuwaingiza wanawake katika TANU.
Picha ya pili niliowatambua nimewaandika majina yao kwenye picha - Sheikh Suleiman Takadir, Iddi Faiz Mafungo, John Rupia, Rashid Kawawa, Said Maswanya na Robert Makange.
Picha ya tatu Julius Nyerere anasalimiana na wananchi 1956.
Picha ya nne kulia Bi. Titi Mohamed, Mama Maria Nyerere, Julius Nyerere, Rashid Kawawa na nyuma ya Nyerere ni Tewa Said Tewa.
Picha TANU ni siku ya uhuru wa Tanganyika 9 Desemba 1961.
Julius Nyerere na Prince Philip kulia kabisa anaonekana Sheikh Abdalla Iddi Chaurembo.