Jihadharini na wahuni wa kundi hili la Kiboko Msheli

Jihadharini na wahuni wa kundi hili la Kiboko Msheli

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Napenda kuwatahadharisha wadau wote kuwa muwe makini zaidi mkiwa barabarani hasa kwenye foleni jijini Dar kwani kuna kundi la vijana zaidi ya 30 maarufu kama 'KIBOKO MSHELI' wanaovamia magari wakiwa na mapanga,nondo na visu kwa lengo la kupora chochote ulichonacho na halikadhalika wanaua ama kujeruhi.

Maeneo hatari ni maeneo ya Jangwani- Morogoro Road,Ocean Road, Seaview, Salender Bridge, Bonde la Kigogo ukitokea Ilala kuja Magomeni, Daraja la Ubungo karibu na njia panda ya kwenda UDSM na barabara ya Mandela Road ukitokea Tazara kuja Ubungo (NDIPO ALIPOVAMIWA RAFIKI YANGU)
His Case.


Akiwa kwenye folen majira ya saa mbili usiku, ghafla lilitokea kundi la vijana kama kumi na mapanga na kuanza kupiga vioo vya gariwakitaka kuvunja, aidha waliongezeka ghafla na wakafunga barabara kama kwa dk 7 hivi wakiendelea kumshambulia (kwenye gari walikuwa watatu),kumbuka kwenye foleni huwezi kukimbia popote, Mungu aliwasaidia sana kwani milango ya gari ilikuwa imefungwa/locked, na vioo vilikuwa vimefungwa kasoro kimoja kilikuwa wazi nusu.

Baada ya mapambano na kelele za kuomba msaada,ndipo msamalia mwema aliyekuwa na silaha aliingilia kati na ndipo alipowatawanya.Kwa mujibu wa Taarifa mbalimbali, haya matukio yamekuwa yakiongezeka sana katika siku za usoni, kwa hilo nawatahadharisha msinunue vitu ovyokwenye traffic light, vioo msishushe ovyo na lock za milango ya magari mfunge, muwe makini.

Ujambazi huu unafanyika kila siku sehemu tofauti kuanzia saa 12 jioni kuendelea.
Namshukuru Mungu hakuna aliyeumizwa sana, japo walifanikiwa kupata baadhi ya vitu ikiwemo simu ya mwenye gari.Natambua unaweza kuona kama sinema,ila haya ndio yanayotokea katika jiji la Dar kwenye foleni za magari.
 
nadhani baada ya machinga kuondolewa barabarani ndo matukio yanaanza jitokeza, sio barabarani tuu, kuna mdau anakaa DSM- Boko/Magengeni njia ya kwenda jeshini. Anasema kuna kikundi cha vijana wanatembea usiku na mapanga...na wiki ilopita wamemjeruhi kijana alokuwa ametoka angalia mpira mida ya usiku. Walokuwepo karibu - bar wakinywa ulevi walitoka ndukiii baada ya tukio wakarejea kuja kumsaidia aloumizwa
 
Kiboko Msheli ni kundi la zamani sana hili.

Miaka ile ya 1980s walikuwa na timu yao ya football!
 
Pale maeneo ya keko Chang'ombe karibu na veta na upande wa darajani mpaka Gold star wapo vijana hatari wa keko machungwa wako na bodaboda kwenye vikundi si chini ya vitano wanashughulikia mikoba ya kina mama wanaokaa upande wa kushoto wa private cars na simu za watu wasiofunga vioo vya magari.
 
Askari wa doria na defender zao hua wanakuwaga wapi?

Siyo kweli...
 
Daah wanarudisha watu nyuma kimaendeleo. Sio poa
 
Kuna jirani yangu kama mwezi nyuma walimpiga panga sijui kisu mkononi kati kati ya kidole gumba na cha shahada nusu kitoke karudi usiku ana maumivu kagari kioo kimoja kimevunjika sijui ilikuwaje

Ila naye bangi kidogo kasema akipona atawatafuta mtaa kwa mtaa pia kasema hajaporwa kitu chochote zaidi kupata hasara gari yake kuweka kioo kipya
 
Hivi hawa wahuni inashindikana Nini kuwafanyia unyama Mkuu kiasi ambacho itakua breaking news ya wiki nzima?

Kinaandaliwa kikosi maalumu kikiwa kimevalia magwanda ya kiraia huku wakiwa wameficha roaded gun wakijitokeza tu wanafanyiwa massacre
Hiyo inakua operation

"Blind killer"

Mchezo unaisha mnakwama wapi wenye mamlaka kwani hizo Kodi tunazolipa si zinaenda kununua siraha Kwa ajili ya matumizi hayo au Ndio mnaziweka kuwatishia Wapinzani wa CCM nikimaanisha wafuasi wa Mbowe na CHADEMA?

Ebooooo!
☹️☹️☹️☹️
 
Back
Top Bottom