koba lee
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 981
- 1,606
Kwema wakuu?
Twende kwenye mada husika. Narudia jiji hili linanuka harufu ya miozo kwa sehemu nyingi. Mtu mbwa wake kadanja anamchukua anamtupa barabarani au pembezoni mwa barabara, paka, mbuzi, kuku wote vilevile.
wanatupwa sehemu ambazo ni makazi ya watu au pembezoni mwa barabara. Hii inasababisha harufu karibia mtaa mzima, iwe una kaa maeneo hayo au ni mpita njia basi ni miharufu mwanzo mwisho. Yaani ni kama mtu kashikilia switch ya kuruhusu harufu itoke au ikate, mfano umepanda gari tokea temeke unaelekea G/Mboto.
Ukifika Sokota ni harufu ya uozo, sokoni na Tazara ni utulivu, Vingunguti ni uozo, Kipawa amani tele, majumba sita uozo mwanzo mwisho, yaani unafika mwisho wa safari kichwa kinauma. Nadhani wengi wenu ni mashuhuda wa hali hii hasa wakazi wa Dar iwe una usafiri binafsi au wa jumuiya.
Hali ni tete Mtu kwa akili zako timamu huwezi tupa mzoga wa mnyama kiholelaholela tu kuna taratibu zake, na hiki kinaweza kua chanzo cha magonjwa mapya ambayo hayaeleweki. Nadhani kuna sheria ndogondogo inabidi ziundwe kudhibiti hii hali tena mabwana /bibi afya walivalie njuga hili suala.
ikitokea mwenyekiti wa mtaa, mtaa wako una harufu ya uozo basi awajibishwe kwa mujibu wa sheria. Unakuta mtu ana kibanda chake cha chips lakini katika eneo hilohilo kuna miharufu ya uozo tena yeye habari hana, huyo achukuliwe.
Nyingine kwenye daladala au mwendokasi asubuhi tu watu mnaenda kazini, unakuta mtu ananuka kama ng'onda, harufu ya kwapa, jasho ,mdomo yaani balaa. Asubuhi tu hiyo sijui jioni itakuaje.
Anyways ngoja niishie hapa lakini nadhani ujumbe umefika japo mi sio muandishi mzuri.
Wasalaam.
Twende kwenye mada husika. Narudia jiji hili linanuka harufu ya miozo kwa sehemu nyingi. Mtu mbwa wake kadanja anamchukua anamtupa barabarani au pembezoni mwa barabara, paka, mbuzi, kuku wote vilevile.
wanatupwa sehemu ambazo ni makazi ya watu au pembezoni mwa barabara. Hii inasababisha harufu karibia mtaa mzima, iwe una kaa maeneo hayo au ni mpita njia basi ni miharufu mwanzo mwisho. Yaani ni kama mtu kashikilia switch ya kuruhusu harufu itoke au ikate, mfano umepanda gari tokea temeke unaelekea G/Mboto.
Ukifika Sokota ni harufu ya uozo, sokoni na Tazara ni utulivu, Vingunguti ni uozo, Kipawa amani tele, majumba sita uozo mwanzo mwisho, yaani unafika mwisho wa safari kichwa kinauma. Nadhani wengi wenu ni mashuhuda wa hali hii hasa wakazi wa Dar iwe una usafiri binafsi au wa jumuiya.
Hali ni tete Mtu kwa akili zako timamu huwezi tupa mzoga wa mnyama kiholelaholela tu kuna taratibu zake, na hiki kinaweza kua chanzo cha magonjwa mapya ambayo hayaeleweki. Nadhani kuna sheria ndogondogo inabidi ziundwe kudhibiti hii hali tena mabwana /bibi afya walivalie njuga hili suala.
ikitokea mwenyekiti wa mtaa, mtaa wako una harufu ya uozo basi awajibishwe kwa mujibu wa sheria. Unakuta mtu ana kibanda chake cha chips lakini katika eneo hilohilo kuna miharufu ya uozo tena yeye habari hana, huyo achukuliwe.
Nyingine kwenye daladala au mwendokasi asubuhi tu watu mnaenda kazini, unakuta mtu ananuka kama ng'onda, harufu ya kwapa, jasho ,mdomo yaani balaa. Asubuhi tu hiyo sijui jioni itakuaje.
Anyways ngoja niishie hapa lakini nadhani ujumbe umefika japo mi sio muandishi mzuri.
Wasalaam.